Msekwa: CCM firm due to grassroots base

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,007
Monday May 11, 2009
Local News

Msekwa: CCM firm due to grassroots base

JAPHET SANGA in Johannesburg, 11th May 2009

Ruling Chama Cha Mapinduzi (CCM) party Vice-Chairman (Tanzania mainland) Mr Pius Msekwa has said his party is still firm because it was not built on personality clout but on grassroots support. Mr Msekwa, who was here to attend the investiture of President Jacob Zuma on Saturday in Pretoria, said yesterday that its members could squabble but the party would not tremour.

He cited past cases where some influential persons like the late Oscar Kambona and the current Chairman of Tanzania Labour Party, Mr Augustine Mrema, defected and people thought CCM would crumble only to be proved wrong.

The vice-chairman was reacting to concern that CCM was likely to go the African National Congress (ANC) way whose internal friction has seen the creation of Congress of the People (COPE) by some ANC defectors.

"Ours is a party molded on grassroots support and, unlike the ANC, we transcend tribal divides," explained Mr Msekwa. He described last weekend's inauguration of President Zuma as yet another opportunity to solidify ties between CCM and the ANC, saying the ties were destined for greater heights than before.

"President Zuma is a close friend to CCM, an amity that spans many years ago. I was here to witness his installation as the ANC President in December 2007 and he came to the CCM congress in Kizota, Dodoma. Therefore, this closeness is set to solidify our ties even further," said Mr Msekwa.

The vice-chairman, who was flanked by the party's Ideology and Publicity Secretary, Mr John Chiligati, said the purpose of their attendance at the inauguration was to cement relations and share experience with the ANC.

"CCM has vast experience in government leadership since 1961 (then Tanganyika African National Union -- TANU) while the ANC swept into government in 1994. So they have something to learn from us much as ANC was established in 1912," explained Mr Msekwa.The Ideology and Publicity Secretary, Mr Chiligati, described last Saturday's inauguration in Pretoria as a milestone in showing the spirit of reconciliation within the ANC.

"Initially most of us thought former President Thabo Mbeki would not attend the ceremony given the hassles that prevailed between Mr Mbeki and Mr Zuma but the former came to the inauguration and they hugged. "That's how African politics should go. They really showed maturity," said Mr Chiligati.

President Jacob Zuma becomes South Africa's fourth post apartheid president after Saturday's investiture attended by about 5,000 dignitaries and invited guests.Some 29 heads of state and government, including President Jakaya Kikwete were here to witness the installation.
 
Thanks for the rubbish Mr. Msekwa. CCM days are numbered, Old dog can never be taught new tricks. We need a Change!
 
"Ours is a party molded on grassroots support and, unlike the ANC, we transcend tribal divides," explained Mr Msekwa.

Huyu clown anaongea hivyo ndani ya South Africa. Wazee wengine wangepumzika tu, wameshapoteza goroli.

Mgeni wa ANC huwezi kuikosoa ANC ndani ya South Africa. Wazee vipi hawa?
 
Nachukia mizee inayoporomosha pumba....kwanini asikae kimya akaficha aibu yake? Nadhani ameacha ukweli hapa CCM firm due to grand corruptions...ningemwelewa!
 
His words are ugly.....but they might be true.

Ndio lakini sio kila ukweli unaropokwa. Kuna kitu kinaitwa tabasuri, au tact.

Ukiropoka "ANC kuna ukabila" na wenyewe wanaweza kukwambia mbona kwenu mpaka Kamati ya Maadili ya CCM ina wala rushwa? Kwenye diplomasia you don't go around playing god like that, its called hegemony.

January Makamba nae karopoka...oooh, hatutaki kuwa kama Nigeria kuna foleni za mafuta. Nigeria hata kwenye rear view mirror yao hawatuoni, tuko mbali nyumba sana kwa kila kitu, kuanzia uchumi mpaka uchawi, mpira mpaka elimu. Mpaka Majaji wa Mahakama Kuu tumeenda kuazima Nigeria. Halafu Ikulu ya Bongo inatoa vi un-diplomatic statements vya kukosoa wengine eti mnasema ni ukweli.

Nilikokulia, hatukuwa na world class diplomats mtaani, lakini ilijulikana kwamba sio kila ukweli unasemwa. Ukitoa maneno uliyoyashuhudia kwa Mama Athumani ukayapeleka mtaa wa pili kwamba leo kina Athumani wamekula kauzu, huo ni ukweli lakini ni umbea. Utaambiwa sawa, wao wamekula kauzu, nyinyi kwenu mwapika gongo. Kwa nini wewe ndio kimungu-mtu?

Msekwa, na deputies wengine kwenye misafara ya Kikwete wajifunze diplomatic tact.
 
This is the Msekwas Grass roots
Diwani wa CCM anaswa akidaiwa kununua shahada

Na Frederick Katulanda,Busanda



WAKATI kampeni za uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Busanda zikiendelea kushika kasi, hali imekuwa mbaya kwa CCM, baada ya diwani na mabalozi wake wawili kunaswa wakidaiwa kuorodhesha majina ya watu wenye shahada kwa lengo la kuzinunua.


Tukio hilo limetokea siku chache baada ya naibu katibu mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe na msimamizi wa uchaguzi wa CUF, Maole Kuchilongulo kuituhumu CCM kuwa ilikuwa ikijiandaa kuendesha hujuma ya kununua shahada za wapiga kura kwa lengo la kupunguza kura za upinzani.


Tukio hilo lilitokea juzi katika kijiji cha Shilungule, kata ya Busanda kati ya saa 2:30 na saa 3:00 usiku baada ya mwenyekiti wa Chadema wa kata hiyo kubaini kikao cha siri cha wajumbe wa nyumba kumi kilichokuwa kikiongozwa na diwani wa kata hiyo, Alphonce Matonange (CCM).


Inadaiwa kikao hicho kilikuwa na ajenda ya kuorodhesha shahada za wapiga kura.

Kamanda wa polisi wilayani Geita (OCD), Shabani Kimei alithibitisha kukamatwa kwa watu hao na kusema jeshi lake limewakamata kutokana na malalamiko ya Chadema na kwamba wanalifanyia uchunguzi wa kina tukio hilo.


"Sisi kazi yetu ni kupokea malalamiko kama hivyo tumepokea na sasa tunafanya uchunguzi. Tumewaita watu wa Chadema wametoa maelezo na tunaendelea na uchunguzi ukikamilika tutawasiliana na msimamizi wa uchaguzi kwa ajili ya hatua zaidi ikiwa ni pamoja na kuangalia sheria za uchaguzi zinasemaje juu ya hatua hiyo," alieleza.


Akizungumzia tukio hilo, mkurugenzi wa oganaizesheni ya mafunzo wa Chadema ambaye pia ni kamanda wa kampeni za uchaguzi wa Busanda, Singo Benson Kigaila alisema mara baada ya kupata taarifa hiyo, walituma gari na kuwasiliana na polisi ambao walifika na kumtia mbaroni diwani huyo na balozi mmoja huku wengine wakikimbia.


Sambamba na mjumbe huyo kukamatwa na diwani, mjumbe mwingine wa nyumba kumi amekamatwa jana asubuhi katika Kijiji cha Musasa kilicho kata hiyo ya Busanda akidaiwa kuendesha zoezi hilo la kuorodhesha majina ya wananchi wenye shahada pamoja na namba zake.


"Baada ya kupata taarifa hiyo tulipeleka timu yetu, wakati inafika tu diwani na wajumbe wengine ambao walikuwa katika zoezi hilo walikimbia baada ya kuona mwanga wa taa za gari, mjumbe mmoja ambaye alikuwa na shahada alinaswa na baada ya kuhojiwa alikiri kuendesha zoezi hilo," alieleza.


Alisema akihojiwa na maofisa wa polisi mbele ya viongozi wa Chadema, mjumbe huyo wa nyumba kumi alisema walikuwa wakiorodhesha shahada hizo kutokana na maelekezo ya wakubwa wake ndani ya CCM ambao waliyatoa kupitia msimamizi wa chama chao ambaye alimweleza kuwa ni mwanamke kutoka wilayani Magu mkoani Mwanza.


Aliwataja waliokamatwa kuwa ni Diwani Alphonce Matonange wa kata ya Busanda ambaye inadaiwa baada ya kukimbia usiku huo aliwahi kupiga simu polisi akidai kulikuwa na gari la Chadema ambalo lilikuwa limeenda kijijini hapo kwa nia mbaya na kwamba lilitaka kumgonga.


Mwingine ni mjumbe wa nyumba kumi aliyefahamika kwa jina la Abdalah Ibrahimu ambaye inadaiwa alikutwa akiwa na karatasi iliyokuwa imeshaorodheshwa watu 20, ikionyesha majina na namba zao za shahada za kupigia kura.


Kigaila alisema kuwa hatua hiyo ni kosa la jinai kwa vile sheria inaeleza wazi kuwa ni kosa la jinai kuorodhesha namba ya shahada ya kupigia kura ya mtu mwingine awe mwanachama wako ama wa chama kingine na kusema hatua yao ya kwanza imekuwa ni kuwakamata na kuwakabidhi mikononi mwa polisi kuthibitisha walichokuwa wakieleza katika mikutano yao.


Alisema sasa wanasubiri kuona polisi itawafanya nini ikiwa ni pamoja na viongozi wao waliowatuma kuendesha zoezi hilo.


Wakati huo huo, wanafunzi wa shule ya sekondari ya Butundwe iliyopo katika kata ya Nyakagomba wameadhibiwa kwa viboko sita kila mmoja baada ya kuzomea msafara wa mgombea ubunge wa CCM, Lolencia Bukwimba wakati ulipokuwa ukipita eneo la shule yao kutoka kwenye kampeni.


Tukio hilo hilo limetokea Ijumaa majira ya saa 10:00 jioni wakati wanafunzi hao walipoona msafara wa mgombea huyo ukipita eneo la shule na kuzomea, kitendo ambacho kiliwaudhi baadhi ya viongozi wa CCM na kuwaagiza viongozi wa kata kufuatilia shule hiyo.


Habari toka Nyakagomba zinaeleza kuwa katika maagizo hayo katibu mwenezi wa kata hiyo, Oscar Magori, ambaye pia ni mwalimu wa Shule ya Msingi Nyakagomba, ndiye aliyekwenda kulalamika kwa mwalimu mmoja wa zamu ambaye aliamua kuwaadhibu wanafunzi wote wa kidato cha kwanza lakini baadhi ya wanafunzi waligoma na hivyo kuwaadhibu sita tu.


Mkuu wa shule hiyo Monika Mzungu alisema wanafunzi hao wameadhibiwa na mwalimu huyo kwa sababu binafsi na kwamba yeye kama mkuu wa shule hiyo hakutoa amri hiyo ya kuwachapa viboko wanafunzi.


"Mimi sikuagiza watoto hao waadhibiwe. Nilishauri wasijiingize katika siasa na waepuke kushabikia vyama bali wajitahidi katika masomo. Kama kuna mwalimu amewaadhibu amewaadhibu yeye kama yeye na sina habari na hilo," alieleza mkuu huyo. 

 
Dilunga,
Nimeipenda hii ya Nigeria kutuzidi kila kitu kuanzia uchumi hadi uchawi. Duu! Nadhani Wanigeria hawajasikia dili ya albinos Bongo. Maana wakiisikia itabidi nao waifanyie utafiti.
 
Duh, Mzee wangu mbona anachemsha jamani... wewe umealikwa nchi ya watu unakwenda zungumzia mambo ya CCM na Zuma kama vile huyu ni kibaraka wa CCM.. Hivi yeye anafikiria wagombea wengine wa ANC waliyachykulia haya maneno vipi..Au tuseme hata vyama vya Upinzani nchini humo kama COPE wamemtazama vipi Msekwa pia kuyaelewa vipi maelezo yake kama sii sawa na kusema CCM ni Utawala wa Kisultan kwani pekee ndio huwa na grassroots support..
Ni muhimu sana kwa viongozi wetu wanapokwenda nje wajaribu sana kuepuka maneno ambayo yanahusiana na kuzua ushabiki au kuleta fitna baina ya wanachama..Hakuna mwana ANC asiyefahamu CCM chini ya mwalimu imewafanyia nini.. Hawa wote kina Mrema, Lipumba, Mbowe, na wagopmbea wote walikuwa CCM anayoizungumzia na wamekuwa wapinzani sii kwa sababu wanaichukia CCM isipokuwa kuleta demokrasia na haki ya uchaguzi wa mfumo wa utawala na sii watu na chuki baina yao..Imani kama hii ndizo hujenga uhasama na chuki baina ya watu.. tunashindwa kuelewa kwamba Upinzani sii uadui hata siku moja ni imani sawa na dini..

Kama yeye ni mkristu nami Muislaam basi haiwezi kuwa sababu ya kuweka majisifu ktk imani ya Mungu wkaati hakuna kati yetu mwenye kufahamu 100% elimu ya Mungu..Na wala tofauti ya imani kati yetu haitufanyi sisi kuwa maadui ndani ya nyumba moja..Uanachama wa vyama vya Siasa vile vile, hakuna mrengo wowote duniani unaoweza kuwa 100% guarantee economic sustanability..kwa sababu ndiyo malengo hasa ya imani za chama.. Laa sivyo kote duniani tungefuata chama kimoja tu kama wengi tunavyopenda kuona dini moja tu..pamoja na kwamba kila mmoja wetu anaimani kuwa dini au mrengo wa chama chake ndio njia pekee..Na ni kutokana na fikra kama za mzee wangu ambazzo hukiuka haki za bianadamu ndio maana tukawa na watu kama Hitler, ikabidi UN watambue haki za mtu kuabudu dini anayotaka kwani bila hivyo tungekuwa maadui na hakuna kitu kingefanikiwa..

Mzee wangu Msekwa inabidi atambue kwamba Chama ni kielelezo cha mrengo na sera zake ambazo zinakwenda na mazingira yaliyopo sio swala la grassroots...Sisi sote tuna kila haki ya kufuata chama chochote kutokana na imani yetu ktk mrengo wa chama nasii swala la grassroots au kubeza wengine hasa pale usipohusika..
He better be careful...
 
Nathani alichokiongelea Msekwa ni kitu cha muhimu sana kinachotukumbusha kwamba katika Jitihada zetu za kupamabana na ufisadi hatutafanikiwa kwasababu tunagusa mtu mmoja mmjoja katika CCM na si CCM kama Chama.

Kama alivyosema , kutoka kwa kina Mrema CCM,kujiuzuru kwa Lowassa n.k hakukitikisa chama na hii ni kweli kwasababu kwasababu hawa wote ni wachache tu ndani ya system corrupt ya CCM. Nathani ufunuo alioutoa Msekwa una nafasi ya kuwakumbusha watu manaopingana na ufisadi kwamba we need to change our stragetic plan and we need to draw a new crtical Path Method.

By taking on CCM and link it Directly with UFISADI this message will reach the Tanzanian grassroot quickly and therefore it will shorten the time of casting out all of MAFISADIS.

But the way we doing it now , We will achieve very little because few MAFISADI will be fired in CCM for the sake of restoring CCM IMAGE in the grassroot and not of that of cleaning out MAFISADI.

I knew this CCM grassroot weapon for so long but it seems many are not getting it, Please people let us wake up
 
Back
Top Bottom