Msekwa atinga Igunga kwa kishindo; Akomba vigogo wa CHADEMA

mkuu, CDM hawatakuwa hivyo, ni watu makini na ndiyo maana hata watu makini hapa jamvini na kwengineko nchini huwaunga mkono...,
angalia gazeti ya TANZANIA DAIMA lilivyo na balance newz ingawa linamilikiwa na Chairman wa CDM!
Taarifa zilzopo ni kwamba Tanzania Daima linapendwa kuliko hilo la Uhuru, hata state house na taasisi nyingine ktk govt, Tanzania Daima linapendwa sana kuliko Uhuru...., hata JK ni mpenzi na msomaji mkubwa wa Tanzania Daima....!

U dont see a big picture. Inawezekana hata Uhuru kuna wasomi na wazoefu wazuri sana. Bora makad wa chama ndio waanzishe hivy vyombo lakini chama uanzisha gazeti au TV au hata radio haifai

Kwanza ni kuua demokrasia wazi wazi na na chama kuwa na gazeti basi hicho chombo sio huru na haiwezi kuwa reliable. Beter nisome Tanzania daima ya ya Mbowe japo najua ni kada wa CDM au Nitazame star Tv ya Dailo wa CCM lakini hata siku moja siwezi kusikiliza , kusoma au uatazama TV ya inayomilikiwa na chama.

Ukisema Tanzania Daima ni tofauti na Uhuru. Tanzania daima linamilikiwa na kada wa CDM na uhuru llinamilikiwa na chama. Mimi nawashauri CDM watafute mbinu za kuendela kujijenga bila kuanszisha vyombo vya habari. Kama kuna umuhimu basi makada wao ndi waanzishe lakini visimilikwe na chama. Utakuwa mzigo na hata mapato vitashindwa kujiendesha kwa faida.

Kama CDM wako makini wanatakiwa ku lobby na kuwa ridhisha wahiriri wa magazeti ili magazeti kama mwanahalishi kuwa pro CDM.

Kama wana mpango huo mi nasubiri nione mwanzo wake na mwisho wake.
 
Ujinga wa gazeti la uhuru ni kuwa huwa hawanagalii upepo ukoje, au kuangalia kwenye mitandano kuwa kipi kinajiri. Hivi kweli hili gazeti wan internet ofisini kwao kweli maana kila kitu pumba tu, au magamba yamekata internet. angalau tbc1 huwa wanatembelea JF. lakini hawa ni hovyo hovyo kabisa.
 
Wanajisumbua hawa wanaongea hisia zao. Laiti wangekuwa Arusha jana wasingekuwa na uso wa kumtazama mtu. Hisia za wananchi nyingine kabisa bado wamelala na ukiritimba. Hao mamluki waliochukua huko Singida ni saleouts katika siasa na njaa kali inawasumbua, katika mapambano yoyote ni lazima kuna wengine wachovu na wabovu wanashindwa kuhimili kishindo upepo ukija tu unawasomba.

Nguvu ya wananchi inatetemesha watawala. Si siri wabiunge wachache kiasi hicho kambi ya upinzan wanawapeleka puta wabunge lukuki wa CCM. Kama anavyosema MCh. Msigwa bungeni wamebanwa na mtaani wamekabwa. Walizopea kutumia uelewa mdogo wa wananchi kujitafutia fursa ya kuongoza na kula.
 
uhuru sio gazeti.hata mleta habari anaogopa kutaja source yake.juzi nililisoma hili gazeti karibu nitapike.

Wenye akili zetu tunaliamini gazeti la Uhuru kama tunavyoliamini gazeti la Tanzania Daima!
 
Thursday, 11 August 2011 20:28

uhuru
newsroom


amsekwa.jpg





Mbona habari yenyewe haina mtiririko unaoeleweka? imeandikwa kiushabiki zaidi.

Kawaida ya magamba.
 
Kun watu wanaasema uhuru sio gazeti alafu hao hao wanasema chadema ianzishe gazeti na TV yake . Muelewe CDM wakiazisha gazeti litakuwa kama uhuru tu........

Inatege mea sera ya uendeshaji wake, sio lazima liwe kama uhuru, gazeti la kirusi.
 
Kichwa cha habari (inaonesha imeandikwa tar 11/8/2011 Kama sikosei) kinaonesha kuwa Msekwa keshatinga Igunga na kukomba viongozi huko, lakini ukweli ni kuwa wakati habari hizo zikiandikwa alikuwa hajafika Igunga, amefika Igunga leo 12/8/2011.

Kama alikomba mamluki wake huko Singida basi ni hukohuko ambako hakuna uchaguzi kwa sasa. Hapa Igunga mjini alipofikizia, ni CDM kwenda mbele, ushahidi ni kuwa hata Diwani wa hapa Kamanda Vincent ni wa Chadema ambae pamoja na kuwepo nguvu za Rostam katika uchaguzi mkuu uliopita alishinda kwa kura 19,000 dhidi ya Mama Ngese wa CCM alieambulia kura 800 tu!

Watoa habari tujitahidi kuwa wakweli tusipotoshe wenzetu walio mbali, tutapoteza Credibility yetu.
 
Hicho ndio kilichobakia CCM,

Kichwa cha habari (inaonesha imeandikwa tar 11/8/2011 Kama sikosei) kinaonesha kuwa Msekwa keshatinga Igunga na kukomba viongozi huko, lakini ukweli ni kuwa wakati habari hizo zikiandikwa alikuwa hajafika Igunga, amefika Igunga leo 12/8/2011. Kama alikomba mamluki wake huko Singida basi ni hukohuko ambako hakuna uchaguzi kwa sasa. Hapa Igunga mjini alipofikizia, ni CDM kwenda mbele, ushahidi ni kuwa hata Diwani wa hapa Kamanda Vincent ni wa Chadema ambae pamoja na kuwepo nguvu za Rostam katika uchaguzi mkuu uliopita alishinda kwa kura 19,000 dhidi ya Mama Ngese wa CCM alieambulia kura 800 tu! Watoa habari tujitahidi kuwa wakweli tusipotoshe wenzetu walio mbali, tutapoteza Credibility yetu.
 
Hivi kweli viongozi wa CCM wanafikiri kwa kina kweli? Unawezaje kwenda kupiga kampeni kwenye jimbo liloachwa wazi na mwanachama wenu ambaye ameachia ngazi kwa sababu ya &quot;siasa uchwara&quot; na &quot;siasa za maji taka&quot;?<br />
<br />
Je, huko ni kukubaliana na maneno ya Rostam kuwa wao ni viongozi wa siasa uchwara, hivyo ni viongozi uchwara, wa chama cha siasa uchwara (yaani chama uchwara) ambacho kimeunda serikali uchwara?!!
<br />
<br /
Hapo sasa kazi umewapa .walizani wazee wa Igunga watakuwa wamesahau .Rostam alishawazoesha bahasha sasa msekwa kaenda na bahasha au maneno .Lakini kaenda kupima upepo unaovuma pale
 
Thursday, 11 August 2011 20:28

uhuru
newsroom


amsekwa.jpg



  • Akomba vigogo wa CHADEMA
  • Mbowe maji ya shingo Arusha


Na mwandishi wetu

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimeisambaratisha CHADEMA baada ya kuzoa vigogo wake wanne mkoani Singida. Vigogo hao walijiunga na Chama wakati Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Pius Msekwa, alipokuwa akiwasalimu wananchi katika kijiji cha Shelui, akiwa njiani kuelekea wilayani Igunga.



Waliojiunga na CCM ni wenyeviti wa wilaya za Iramba, Emmanuel Ntundu na Nakamia Wazaeli (Singida Mjini), Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wilaya ya Iramba, Ela Dyelu na Katibu Mwenezi wilaya ya Iramba, Enelly Kingu. Msekwa aliwapongeza viongozi hao kwa uamuzi wa kujiunga na CCM na aliwataka kutimiza ahadi yao ya kuleta wanachama wengine 90. Kwa upande wake, Katibu wa NEC, Uchumi na Fedha, Mwigulu Nchemba, alisema kitendo cha wanachama hao ni salamu kuwa CCM inakubalika. Kutoka Arusha, Lilian Joel, anaripoti kuwa, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, katika hali isiyo ya kawaida ameendelea kuwachochea wananchi kuvamia ofisi ya Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Estomii Changa.

Akihutubia mkutano wa hadhara jana katika viwanja vya NMC, Mbowe alisema baada ya siku 30 atarudi Arusha kushirikiana na wananchi kuvamia ofisi za manispaa. Mbowe alisema sababu za uvamizi huo ni kupinga kitendo cha Changa kuwatambua madiwani waliofukuzwa na CHADEMA.



"Tumesikia mkurugenzi ametamka anawatambua madiwani tuliowatimua, nawaomba wananchi, kesho tunarejea bungeni, baada ya siku 30 tutarudi kwa kazi moja tu ya kuandamana hadi katika ofisi za mkurugenzi na tutalala hapo na kushinda, alisema. Alimtaka Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha, Thobias Andengenye, kujiandaa vyema kwa kukusanya askari kutoka mikoa ya jirani siku ya maandamano hayo.



Mbowe na baadhi ya viongozi wa CHADEMA, akiwemo Katibu Mkuu wake, Dk. Willibrod Slaa na wajumbe wa kamati kuu ya chama hicho walifika Arusha kwa ajili ya kujisafisha kwa wananchi, baada ya kuwafukuza madiwani watano wa chama hicho.
Baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano huo walionyesha kutoafiki kauli na wito uliotolewa na Mbowe wa kuandamana.


Mjumbe wa kamati kuu ya chama hicho, Mabere Marando, aliwasihi madiwani waliofukuzwa wasiende mahakamani, kwa madai hakuna atakayewatetea.
Madiwani waliofukuzwa ni Naibu Meya, Estomih Mallah, ambaye ni diwani wa Kimandolu, John Bayo (Elerai), Rehema Mohamed (Viti Maalumu), Charles Mpanda (Kaloleni) na Rubeni Ngowi (Themi).




Last Updated ( Thursday, 11 August 2011 20:35 )

Labda atikise kwa kugawa rushwa na sii sera. Sera za kizee zimepitwa na wakati.
 
Back
Top Bottom