Msanii Naseeb Abdul (Diamond) aswekwa mahabusu kwa kupiga mwandishi wa habari

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,883
6,884
DSCF5975.JPG
DSCF5980.JPG


Msanii Naseeb Abdul a.k.a Diamond akiwa chini ya ulinzi wa mashabiki uwanja wa Samora Iringa baada ya kushindwa kufanya show katika uwanja huo. Msanii huyo na wenzake wamekamatwa na polisi Iringa baada ya kumpiga na kuharibu vifaa vya kazi vya mmiliki wa mtandao wa Francis Godwin Mzee Wa Matukio Daima kama njia ya kupinga kuhojiwa na vyombo vya habari.

Msanii Diamond ameruhusiwa kudhaminiwa leo majira ya saa 6 mchana na kuondoka kuelekea jijini Dar es Salaam kufanya uzinduzi wa Albamu yake,msanii huyo aliwekwa mahabusu ya kituo cha polisi mjini Iringa kwa tuhuma za kumpiga na kuharibu vitendea kazi vya mmiliki wa mtandao huu wawww.francisgodwin.blogspot.com uwanja wa Samora mjini Iringa
 
Hii imetokea lini na kwanini iwekwe leo Januari mosi? Juzi usiku (tar 30 kuamkia tar 31) saa sita kasoro usiku Diamond alikuwa Live EATV akiwa na hard Mad (au man sina hakika na jina) wakizungumzia onesho la leo hii. Sasa huyu blogger atakuwa alikuwa na picha hizo before ijumaa lakini ameamua kutuwekea hapa leo Jpili kitu ambacho kimepitwa na wakati!
 
huyu nae amempiga mtu? au karateka? Au mwandishi nae anavunja biskuti kwa goti
 
Dogo amejisahau sana, amuulize Mr. Nice saizi anatii matakwa ya Cameroon ili aishi mjini toka kwenye u SuperStar.
 
kweli jamaa anatangaza tu hako kablog, hivi diamond anaweza kumpiga mtu kweli zaidi ya wema? au huo mwandishi ni binti?
 
Back
Top Bottom