Keynes
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 533
- 89
Ndugu wana JF.
Kwa muda mrefu tumekua tukipiga makelele ya ufisadi bila kutoa muafaka au solution.
Kutokana na uongozi wa nchi kuonekana kua umeshindwa kurudisha maliasili zilizoibiwa na mafisadi na kufichwa nje ya nchi kwa mantiki kwamba katika kila dili la ufisadi ni viongozi wengi wa serikali wameshiriki kiasi kwamba wanashindwa kujiwajibisha wenyewe.
Ukiangalia swala la EPA kama ni kuwajibishwa viongozi ingebidi mpaka rais ajiuzulu maana serikali nayo imeshiriki direct kupitia kagoda na meremeta. Je tunaweza kushinikiza serikali yote ijiuzulu? Jibu ni hapana maana wakijiuzulu wote nani atampeleka mwezake mahakamani? Na je ikijiuzulu hizo hela walizoficha nje ya nchi tutazipataje? Maana kuna viongozi wengi wenye fedha nyingi nje lakini hakuna ushahidi kua walizipataje au waliziiba wapi!!
MY POINT
Kwa sababu mafisadi wamekua wakiiba fedha na kuficha nje ya nchi ambapo uchumi wa tanzania umezidi kuzorota kutokana na capital flights wakati nchi za nje ambazo ni matajiri kama Uswiss wananchi wao wanakopa hizo hela walizoficha mafisadi huko na kuzitumia kama mitaji.
Je mwaonaje serikali ikitangaza msamaha kwa mafisadi wote walioficha hela nje ya nchi na kuwataka waje kuwekeza tanzania then tukaanza upya??
Pili usalama wa taifa ungefanya utafiti wa akiba zilizopo nje na wenye hela zote nje zirudishwe kwenye mabank ya tz na wahusika waruhusiwe ku invest ndani ya nchi ili kukuza ajira.
Angalieni mfano mdogo wa ile bilion mzee wa vijisent aliyoficha nje kule inafaidisha wengine wakati tz watu hawana mitaji.
Tatu baada ya hayo yote kufanyika sheria ya takukuru iimarishwe ili rushwa na kujilimbikizia mali kwa viongozi kusijirudie tena.
TUKI KOMAA NAO SANA KUWAFUNGA HATUWEZI NA HELA ZINAZIDI KUPOTEA
Yangu ni hayo karibuni!!
Kwa muda mrefu tumekua tukipiga makelele ya ufisadi bila kutoa muafaka au solution.
Kutokana na uongozi wa nchi kuonekana kua umeshindwa kurudisha maliasili zilizoibiwa na mafisadi na kufichwa nje ya nchi kwa mantiki kwamba katika kila dili la ufisadi ni viongozi wengi wa serikali wameshiriki kiasi kwamba wanashindwa kujiwajibisha wenyewe.
Ukiangalia swala la EPA kama ni kuwajibishwa viongozi ingebidi mpaka rais ajiuzulu maana serikali nayo imeshiriki direct kupitia kagoda na meremeta. Je tunaweza kushinikiza serikali yote ijiuzulu? Jibu ni hapana maana wakijiuzulu wote nani atampeleka mwezake mahakamani? Na je ikijiuzulu hizo hela walizoficha nje ya nchi tutazipataje? Maana kuna viongozi wengi wenye fedha nyingi nje lakini hakuna ushahidi kua walizipataje au waliziiba wapi!!
MY POINT
Kwa sababu mafisadi wamekua wakiiba fedha na kuficha nje ya nchi ambapo uchumi wa tanzania umezidi kuzorota kutokana na capital flights wakati nchi za nje ambazo ni matajiri kama Uswiss wananchi wao wanakopa hizo hela walizoficha mafisadi huko na kuzitumia kama mitaji.
Je mwaonaje serikali ikitangaza msamaha kwa mafisadi wote walioficha hela nje ya nchi na kuwataka waje kuwekeza tanzania then tukaanza upya??
Pili usalama wa taifa ungefanya utafiti wa akiba zilizopo nje na wenye hela zote nje zirudishwe kwenye mabank ya tz na wahusika waruhusiwe ku invest ndani ya nchi ili kukuza ajira.
Angalieni mfano mdogo wa ile bilion mzee wa vijisent aliyoficha nje kule inafaidisha wengine wakati tz watu hawana mitaji.
Tatu baada ya hayo yote kufanyika sheria ya takukuru iimarishwe ili rushwa na kujilimbikizia mali kwa viongozi kusijirudie tena.
TUKI KOMAA NAO SANA KUWAFUNGA HATUWEZI NA HELA ZINAZIDI KUPOTEA
Yangu ni hayo karibuni!!