Msaidieni rafiki yangu

Duh hapo ngoma nzito amuulize mumewe kwa taratibuuu ataelewa ni nini

Desidii hujambo rafiki.

Ahsante kwa kuendelea kuikipu promisi yako.

Huwezi jua navofarijika na kuongezeka pumzi. We ni mtu mwaminifu sana.
 
huyu dada ajitahidi kuwa karibu na mumewe kuliko siku nyingine.na amuelezee ni jinsi gani anampenda,na ataumia akisikia ana mtu mwingine.pia amuulize ni kipi anapenda amfanyie ili aishi kwa furaha asiwe na mwingine.ila asije kujaribu kumwambia kwamba amesikia anataka kuoa noooo.
iwe ni kila siku awe anamsisitizia anampenda na pia maisha yao wawe karibu ili walee mtoto.mawazo ya kuoa kwingine yaweza potea.
 
Matendo ya huyo mume je yakoje? yanaonyesha hampendi wala kumjali? huyo dada ana hisia au hata fununu kuwa mumewe ana nyumba ndogo? kuna mabadiliko ndani? akae atulie kama hajui kitu kinachoendelea huko aki-keep close eye na yanayoendelea, akiona mabadiliko na aulize mumewe kinachoendelea na apate msimamo wa huyo mume.
 
Mtu akishaamua,je kutetea ndoa utaweza??Si anaenda tu bomani wanaoana!!kupiga chabo nako kubaya,bora angekuwa ajui.aletewe tu watoto
 
So true...as i said please think abt this guys kabla hamjatoa advice bc as we all know wanaume ni kama watoto they never know what they want....i think she have a right to stand for her married n never let it fall apart bc u as a woman ndo unadicide when to end ur married..if u love your husband please fight for ur married otherwise......the choice is urs end of the day n u have to bare the coinsenqunsys of ur choices

mmmmhhh
 
Asanteni wapendwa nitafikisha michango yenu kwa muhusika kuhusu ndoa yake wanaishi vizur tuu na wamebarikiwa watoto 3, Mungu atamsaidia katika kipindi hiki kigumu kweli shetani ana majaribu mengi. Asanteni sna
 
Aaagh eebana eeee hii kali, mama muage mumeo kwa upendo kabisa beba mwanao rudi kwenu kwa wazazi maana huyo akiletwa humo na hivi anapendeka sana na mumeo ujue utaambulia vioja vya ajabu kabisa!
Si una kwenu na hukufukuzwa aga vzr rudi kwenu endelea kumuomba mungu atakusaidia kabisa! Kila jambo linalotokea duniani lina maana yake na huwezi kuijua sasa hv ila utaijua baadaye kabisa. Kumbuka mawazo ya mungu ni tofauti na ya binadamu na yameachana kwa umbali mkubwa mnoooo!

Mh!!!! Haya pia maneno
 
Michango yetu ni msaada mkubwa!

MmmmmmmmmmmmmHhhhh!!!!!!!!!!!!! Pole, hapo ulichokosea ni kuchukua ushahidi, ninamaanisha ungem-record kwa cm, lakini kwa kuwa ulisikia maongezi yao wewe mwenyewe, haukuambiwa na mtu, wewe endelea kuwafuatilia nyendo zao kwa ukaribu na umakini sana, utajua hiyo siku ya ndoa, aidha ukaipinge au wewe mwenyewe utaona kama ni sawa kuipinga au utamwachia Mwenyezi Mungu awahukumu. Uwe unapitia pitia kwa mkuu wa wilaya (Bomani) kuangalia matangazo ya ndoa cause its obvious ndoa itafungiwa huko, kwa sababu tayari mnayo ya kanisani (samahani nimeandika kama ni wewe though wewe ulisema ni rafiki yako) nilisahau nikawa nimeweka wewe moja kwa moja. Nadhani sijakukwaza.

Kwa upande wangu mimi kwa kweli ningemwomba tupumzishane, yeye aende kwa mwanamke wake anayempenda, halafu tupeane talaka, kwani mapenzi hayahitaji huruma achukue hasini zake na kama ameona huyo mwanamke ndo furaha yake basi na aendelee naye, na mimi nichukue time na maisha yangu na mwanangu.
 
funga kwa maombi, Muombe Mungu akuonyeshe njia. Akupe hekima ya maamuzi sahihi, yote yawezekana kwa imani. Muombe Mungu akutendee = = na mapenzi yake. Kilichofungwa na Mungu mwanadamu hawezi kukitenganisha. Huyo mjomba,mumeo, na macho kodo washindwe ktk jina la Yesu.
 
Kama hamna ugomvi muombe mwende mahali patulivu mkishapiga stori zikakolea muulize kwa upole kama kweli anakupenda kwa dhati. Akisema anakupenda mwambie umepata taarifa za uhakika kwamba ana mpango wa kuoa. Atakurupuka kukuuliza nani kakwambia, mwambie unataka kusikia toka kwake. Hapo ndo pa kuanzia.......

Na akisema hakupendi muombe aweke wazi sababu za kutokupenda. Baadae mnaweza kuwashirikisha wazazi kadri ya ugumu wa issue. Pole

Ambassador hivi akisema hakupendi kuna haja ya kuita ndugu jamaa ama wazazi?

hahaha kama ni mapenzi honey basi yameisha zamani....
 
Hapa kuna kitu ambacho wote hamkioni, kitendo cha huyo mama kuja kwa siri na kujificha kusikiliza wanachoongea mumewe na mjomba wake kinaonesha kuwa hiyo ndoa tayari ina matatizo.. Cha msingi ni huyo mama kutafuta muda amueleze mumewe kuwa tayari anajua kuwa anataka kuoa, ingawaje si rahisi sababu it's obvious kwamba hakuna mawasiliano mazuri. Awe tayari kwa jibu baya sababu akipewa zuri ajue ni uongo na aeleze maisha baada ya kupigana chini yatakuwaje upande wa mtoto. Wakishaelewana waagane, sababu kama kakiri kwa mjomba wake anampenda sana huyo mpya ni kwamba huyu wa zamani hapendwi tena!!
 
Maria Roza nitampa true story ya ndugu yangu iwe tu changamoto kwake ingawa kwa huyu ndugu yangu hawezi jenga tena ndoa yenye afya baada ya matatizo makubwa.

Huyu dada alikuwa anaishi kwa amani na upendo na mumewe yaan aseme nini asipewe maisha yalikuwa mazuri kwa kipindi kirefu sana bila kuhisi chochote kwa mumewe.ghafla mume akabadilika akaanza kuchelewa kurudi mara harudi mwisho akatoa kali kumwambia dada sio kwamba yeye sio mzuri au hamuhudumii vizuri ila kapata msichana anaempenda sanaaaa na akamuaga anaondoka pale home akachukua briefcase yake tu yenye docs muhimu akasepa.

Baada ya muda kidogo akabadili na dini akafunga ndoa kiislam huku dada kuchanganyikiwa basi akaingia kusali sanasana maisha yakaendelea tukawa tunapishana tu na shem na mke mpya barabarani magari yote walichukua basi watoto waliozoea magari wakaanza kupanda daladala huku home mke akapangisha nusu ya jumba lao ili ajikimu maana hata ada ilikuwa shida.miaka ilikatikayule jamaa akaanza kuumwa kwa sana mpaka akalala kitandani unajua alichofanya yule mke mpya? Akampigia sister eti njoo umuuguze mumeo mie niko bize sana na majukumu mengi.

Basi mdada mbio kwa sababu ya mapenzi na mumewe uguza na wewe pika michemsho akatafuta na doctor akapata dawa nzuri jamaa akasimama akapata afya.Guess wat????alivyopona kabisa akamwambia dada asije tena pale mke wake atakasirika na kumbuka demu alishasepa kitambo alienda panga nyumba ingine.Basi demu akarudi kwa nyodo nataka hati za nyumba na gari jipya akapewa vyote maisha yakaendelea mdada akawa anajirusha tu na mabwana wengine yule baba akaanza kuwa na mawazo na hivi hapati lishe nzuri na bado anaendelea kufanya lile tendo akadhoofu sana akaumwa mbaya demu akamkimbia tena eeti kapata kazi mkoani.akaondoka kamwacha kitandani dereva wake akamfata sista kumwambia jamaa anakufa kule. dada mbio na makapu ya huduma jamani, hudumia weee akaanza dozi upya mpaka akapona

Hapo akarudi home sasa ndoa tena haikuwa ndoa sista yuko fiti haumwi jamaa ndio hivyo tena. Basi sasa hivi wanalea tu familia na yeye kuhudumiwa sista kapendeza na wala hataki mchumba wala mume mwingine. yule mumewe anaishi mle ndani kwa chumba tofauti.lile demu liko huko mkoani,anaendelea kusambaza na ni msomi ile mbaya. Si kwamba hajarudiana nae sababu anaumwa, anasema mapenzi yaliisha tena akawa anamuhurumia tu.Unaona maisha yalivyo, wanaume wanajidanganya wanapendwa kumbe inapendwa pesa tu hapo wakitetereka mtu anaonyesha makucha yake.
Ushauri wangu huyo dada aendelee na maisha yake asiruhusu kitu kama hicho cause once huyo mume keshapenda mwingine na roho ikipenda hula nyama mbichi asilazimishe kusubiri mpaka yamkute huko aruddi wakati maisha yanaendelea. Bora aishi mwenyewe na mtoto wake awe happy. kuwa na mke mwenza ni kukaribisha maradhi ya moyo ambayo utakufa na mwanao atapata shida. dah sor kwa comment ndefu
 
Wewe tulia sali sana mipango yao isifanikiwe, na tulia nyumbani kwako ukimwomba mungu. Kua naimani kwamba hakutakua na ndoa kati yao.
 
funga kwa maombi, Muombe Mungu akuonyeshe njia. Akupe hekima ya maamuzi sahihi, yote yawezekana kwa imani. Muombe Mungu akutendee = = na mapenzi yake. Kilichofungwa na Mungu mwanadamu hawezi kukitenganisha. Huyo mjomba,mumeo, na macho kodo washindwe ktk jina la Yesu.

Maombi yanasaidia ila amuombee tu huko anakoenda aishi vizuri wakati yeye akiendelea na maisha yake kama huyo sista kaombaaa mume karudi ila ndio karudi nao sasa inakuwaje hapo. mie namshauri aendelee na maisha yake tu
 
Maria Roza nitampa true story ya ndugu yangu iwe tu changamoto kwake ingawa kwa huyu ndugu yangu hawezi jenga tena ndoa yenye afya baada ya matatizo makubwa.

Huyu dada alikuwa anaishi kwa amani na upendo na mumewe yaan aseme nini asipewe maisha yalikuwa mazuri kwa kipindi kirefu sana bila kuhisi chochote kwa mumewe.ghafla mume akabadilika akaanza kuchelewa kurudi mara harudi mwisho akatoa kali kumwambia dada sio kwamba yeye sio mzuri au hamuhudumii vizuri ila kapata msichana anaempenda sanaaaa na akamuaga anaondoka pale home akachukua briefcase yake tu yenye docs muhimu akasepa.

Baada ya muda kidogo akabadili na dini akafunga ndoa kiislam huku dada kuchanganyikiwa basi akaingia kusali sanasana maisha yakaendelea tukawa tunapishana tu na shem na mke mpya barabarani magari yote walichukua basi watoto waliozoea magari wakaanza kupanda daladala huku home mke akapangisha nusu ya jumba lao ili ajikimu maana hata ada ilikuwa shida.miaka ilikatikayule jamaa akaanza kuumwa kwa sana mpaka akalala kitandani unajua alichofanya yule mke mpya? Akampigia sister eti njoo umuuguze mumeo mie niko bize sana na majukumu mengi.

Basi mdada mbio kwa sababu ya mapenzi na mumewe uguza na wewe pika michemsho akatafuta na doctor akapata dawa nzuri jamaa akasimama akapata afya.Guess wat????alivyopona kabisa akamwambia dada asije tena pale mke wake atakasirika na kumbuka demu alishasepa kitambo alienda panga nyumba ingine.Basi demu akarudi kwa nyodo nataka hati za nyumba na gari jipya akapewa vyote maisha yakaendelea mdada akawa anajirusha tu na mabwana wengine yule baba akaanza kuwa na mawazo na hivi hapati lishe nzuri na bado anaendelea kufanya lile tendo akadhoofu sana akaumwa mbaya demu akamkimbia tena eeti kapata kazi mkoani.akaondoka kamwacha kitandani dereva wake akamfata sista kumwambia jamaa anakufa kule. dada mbio na makapu ya huduma jamani, hudumia weee akaanza dozi upya mpaka akapona

Hapo akarudi home sasa ndoa tena haikuwa ndoa sista yuko fiti haumwi jamaa ndio hivyo tena. Basi sasa hivi wanalea tu familia na yeye kuhudumiwa sista kapendeza na wala hataki mchumba wala mume mwingine. yule mumewe anaishi mle ndani kwa chumba tofauti.lile demu liko huko mkoani,anaendelea kusambaza na ni msomi ile mbaya. Si kwamba hajarudiana nae sababu anaumwa, anasema mapenzi yaliisha tena akawa anamuhurumia tu.Unaona maisha yalivyo, wanaume wanajidanganya wanapendwa kumbe inapendwa pesa tu hapo wakitetereka mtu anaonyesha makucha yake.
Ushauri wangu huyo dada aendelee na maisha yake asiruhusu kitu kama hicho cause once huyo mume keshapenda mwingine na roho ikipenda hula nyama mbichi asilazimishe kusubiri mpaka yamkute huko aruddi wakati maisha yanaendelea. Bora aishi mwenyewe na mtoto wake awe happy. kuwa na mke mwenza ni kukaribisha maradhi ya moyo ambayo utakufa na mwanao atapata shida. dah sor kwa comment ndefu

Saingine binadamu hua tunafuata akili zetu, tukidhani ni upendo wa dhati kumbe ni uvumilivu wa kijinga. Kama huyo dadaako mungu hakutaka afe kwa ugonjwa maskini lakini yeye hakujua hilo. Siku zote wanaoingilia nyumba za wenzao na kuolewa wao maisha yao huisha vibaya tena kwa aibu kubwa.
 
Akae chini amwulize mume ni sababu gani zinazomfanya atake kuoa tena? Ikibidi wazee wa pande zote nao wawepo kwenye kikao cha usuluhishi, na huyo pastor aliyewafungisha ndoa ahusishwe ktk hili.
Pole sana dada. Hapo pagumu sana.
 
Akae chini amwulize mume ni sababu gani zinazomfanya atake kuoa tena? Ikibidi wazee wa pande zote nao wawepo kwenye kikao cha usuluhishi, na huyo pastor aliyewafungisha ndoa ahusishwe ktk hili.
Pole sana dada. Hapo pagumu sana.

Kaka angu unafikiri wakimwita atakubali? atakataa ila ataendelea na mpango wake. mi mambo ya wanaume kutesa wake zao yananishangaza sana kama vile walilazimishwa kuoa,aaghhhhhhhhrrrrrrrr
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom