Msaidieni rafiki yangu

Maria Roza

JF-Expert Member
Apr 1, 2009
6,797
1,567
Habari zenu, Wiki kadhaa zilizopita nilirudi nyumbani kumkuta mume wangu na mjomba wake wakiwa wanazungumza.Nilitulia sehemu nikawasikiliza kiasi,nilichanganyikiwa.Nikaondoka, badae nikarudi nikajikausha kama hamna nilichosikia.Mume wangu alikuwa anamueleza mjomba wake mpango wa kuoa tena, na mjomba wake alikuwa akimsupport.Sisi wakristo,tulifunga ndoa ya kanisani.Mume wangu alisisitiza kuwa itabidi amuoe huyo mwanamke maana anampenda sana, na mwanamke amesema bila ndoa yeye anataka waachane,hawezi kukubali kuwa hawara.Nanukuu "Hata hivyo sijapata kukutana na mwanamke tukapendana naye kama yule".Maneno haya yanatoka kwenye kinywa cha mume wangu wa ndoa,na baba wa mtoto wangu.Kwa ufupi plan ilikuwa inapangwa namna ya kufanya hili jambo kwa utulivu na makini.Naomba ushauri, mana sijui pa kuanzia, kumbuka haya mambo alikuwa anayaongea na mjomba wake,na mjomba aliongea kama mtu anayemjua kabisa huyo mwanamke anayeongelewa.
Michango yetu ni msaada mkubwa!
 
Nivizuri ameusikia ukweli mwenyewe, sasa aangalie mbele, maana kama asingefahamu still yangemkuta na angeeseka zaidi.yote ni madhara ya kukurupuka kufuata akili maana kwenye hili la kutamani akili huusika zaidi.
Mpe pole sana ila aishi kwa kuujua ukweli.
 
i see Maria Roza ngoja kwanza nipate coffee ndo nirudi hapa pagumu mwenzio akinyolewa .......:coffee::coffee:
 
Kama hamna ugomvi muombe mwende mahali patulivu mkishapiga stori zikakolea muulize kwa upole kama kweli anakupenda kwa dhati. Akisema anakupenda mwambie umepata taarifa za uhakika kwamba ana mpango wa kuoa. Atakurupuka kukuuliza nani kakwambia, mwambie unataka kusikia toka kwake. Hapo ndo pa kuanzia.......

Na akisema hakupendi muombe aweke wazi sababu za kutokupenda. Baadae mnaweza kuwashirikisha wazazi kadri ya ugumu wa issue. Pole
 
i see Maria Roza ngoja kwanza nipate coffee ndo nirudi hapa pagumu mwenzio akinyolewa .......:coffee::coffee:

nadhani mumeo ni mtu makini,kama ataweza kukuletea mwenzio wa kukusaidia co mbaya,tena umesikia akisema anampenda sasa tatzo liko wapi? We tulia kama umesikia ni kusubiri utekelezaji.
 
ye atulie, aulize kwa upole kama huyo mume ana plan gani na yeye, mwisho ataamua pa kuanzia na kuchukua maamuzi sahihi
 
Dah!Kweli wanaume wengine ni hatari!Well kama amemsikia akiyasema hayo mwenyewe kilichobaki ni kujulishwa ili awe na uhakika!Kwanza ajiandae kupokea jibu lolote!Akusanye nguvu za kuweza kupokea na kukabilia na chochote kile atakachoambiwa!Ni ngumu ila kama mumewe kaamua kweli then amchukue mwanae wakatafute maisha yao mbele kwa mbele!Akimng'ang'ania mwanaume asiyempenda na anaeweza kua amemchoka ataishia kunyanyasika tu!Pole yake!
 
Dah!Kweli wanaume wengine ni hatari!Well kama amemsikia akiyasema hayo mwenyewe kilichobaki ni kujulishwa ili awe na uhakika!Kwanza ajiandae kupokea jibu lolote!Akusanye nguvu za kuweza kupokea na kukabilia na chochote kile atakachoambiwa!Ni ngumu ila kama mumewe kaamua kweli then amchukue mwanae wakatafute maisha yao mbele kwa mbele!Akimng'ang'ania mwanaume asiyempenda na anaeweza kua amemchoka ataishia kunyanyasika tu!Pole yake!

Hapo kweenye Blue tunatofautiana kidogo mpaka muomba msaada atufafanulie yafuatayo;
1. kabla ya kusikia maongezi hayo mahusiano yake na mumewe yalikuwaje?
2. Alifunga ndoa kanisani, lakini je, kati yao kunaaliye badili dini kwa minajili ya hiyo ndoa?
3. Anaumri gani 20's au 30's
 
nadhani mumeo ni mtu makini,kama ataweza kukuletea mwenzio wa kukusaidia co mbaya,tena umesikia akisema anampenda sasa tatzo liko wapi? We tulia kama umesikia ni kusubiri utekelezaji.

Si rahisi kama unavyofikiria!!!!!!!
 
Aaagh eebana eeee hii kali, mama muage mumeo kwa upendo kabisa beba mwanao rudi kwenu kwa wazazi maana huyo akiletwa humo na hivi anapendeka sana na mumeo ujue utaambulia vioja vya ajabu kabisa!
Si una kwenu na hukufukuzwa aga vzr rudi kwenu endelea kumuomba mungu atakusaidia kabisa! Kila jambo linalotokea duniani lina maana yake na huwezi kuijua sasa hv ila utaijua baadaye kabisa. Kumbuka mawazo ya mungu ni tofauti na ya binadamu na yameachana kwa umbali mkubwa mnoooo!
 
Kama hamna ugomvi muombe mwende mahali patulivu mkishapiga stori zikakolea muulize kwa upole kama kweli anakupenda kwa dhati. Akisema anakupenda mwambie umepata taarifa za uhakika kwamba ana mpango wa kuoa. Atakurupuka kukuuliza nani kakwambia, mwambie unataka kusikia toka kwake. Hapo ndo pa kuanzia.......

Na akisema hakupendi muombe aweke wazi sababu za kutokupenda. Baadae mnaweza kuwashirikisha wazazi kadri ya ugumu wa issue. Pole
Naungana na wewe kabisa ambassador, hebu apate muda wa kumuambia anachokijua then amsikie kwa mdomo wake anasemaje?
Na amuhakikishie anajua mpango mzima wa lengo lake la kutaka kuoa.
 
Jamani huyo dada asikurupuke kuondoka, sikuhizi kuna siasa za maji taka, watu wanakuchanganyia unakimbia kwa mihasira yako, mwisho wa siku unagundua mchezo mambo yanakuw ndio basi tena. wanasema ukiona manyoya keshaliwa huyo.... aangalie sio kukimbiakimbia:roll:
 
Mhh jamani nyie hebu tuchukue second tufikirie kabla ya kuandika chochote maana...si mambo marahisi haya
na kila ushauri tunaompa lazima tufikiri kuwa matokeo yake anaweza kuyahandle?ameomba msaada wa ushauri..please lets think kidogo..si unajua kwanza mapenzi yanauma?
Ngoja nifikiri then i will advice
 
Huyo anayetaka kuolewa hafahamu kama kuna mwenzake ndani ya ndoa? Anang'ang'ania kuingia nyumba ya mwenzake, afahamu mwenzake alipendwa kama yeye na iko siku naye atatafutiwa mwingine. Ndugu yangu penzi likishachuja kunakuwa hakuna tena raha ya kuishi pamoja, kama unaweza ondoka na mwanao mkaanze maisha na Mungu atakuwezesha kwa kila namna. Nimeweza.
 
Lakini huyu mwanaume hajasema kuwa hampendi mke wake wa sasa! Japo nahisi walikuwa wana mtest huyu mke wa sasa maana walijua anatabia za kuchungulia na kunyatia mazungumzo!
 
Lakini huyu mwanaume hajasema kuwa hampendi mke wake wa sasa! Japo nahisi walikuwa wana mtest huyu mke wa sasa maana walijua anatabia za kuchungulia na kunyatia mazungumzo!


UTAFANYA WATU WAJINYONGE :laugh:
 
UTAFANYA WATU WAJINYONGE :laugh:


So true...as i said please think abt this guys kabla hamjatoa advice bc as we all know wanaume ni kama watoto they never know what they want....i think she have a right to stand for her married n never let it fall apart bc u as a woman ndo unadicide when to end ur married..if u love your husband please fight for ur married otherwise......the choice is urs end of the day n u have to bare the coinsenqunsys of ur choices
 
Hiyo ndoa ya pili itafanyika wapi? kwa ukristo nadhani haiwezekani, nawe una haki ya kikanisa na kikatiba pia kupinga ndoa hiyo. hata kama ameonekana kumpenda huyo mwanamke, usikubali aoe kirahisi tu, tetea ndoa yako mama. Je mahusiano yenu yakoje? yamebadilika?
 
Jamani huyo dada asikurupuke kuondoka, sikuhizi kuna siasa za maji taka, watu wanakuchanganyia unakimbia kwa mihasira yako, mwisho wa siku unagundua mchezo mambo yanakuw ndio basi tena. wanasema ukiona manyoya keshaliwa huyo.... aangalie sio kukimbiakimbia:roll:

Naungana nawe Elia, hivi kwa hali ya kawaida, mtu mwizi anajua kuna ndoa ya kikristo naye anataka ndoa, ndoa gani? ya kimila, kiislamu au bomani? anajiamini vipi kama si siasa za maji taka? tulia dada tetea ndoa yako mpaka tone la mwisho, huyo mwizi asipate kirahisirahisi tu, ye si kesha sema bila ndoa hataki. Huyo mume ajue si kila pendo linawezekana kama alikosea mwamnzi hana budi kuface the consequences.
 
Huyo anayetaka kuolewa hafahamu kama kuna mwenzake ndani ya ndoa? Anang'ang'ania kuingia nyumba ya mwenzake, afahamu mwenzake alipendwa kama yeye na iko siku naye atatafutiwa mwingine. Ndugu yangu penzi likishachuja kunakuwa hakuna tena raha ya kuishi pamoja, kama unaweza ondoka na mwanao mkaanze maisha na Mungu atakuwezesha kwa kila namna. Nimeweza.[/QUOTE]
Kwenye kolezo, hongera sana na pole pia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom