Habari zenu wana jamii forum,
Mimi nimetumwa kwa niaba ya familia yetu nijiunge humu ili kunusuru ndugu yetu aliye katika hatari ya kupoteza maisha.
Mkasa wenyewe uko hivi;
Tuna mdogo wetu aliyevushwa na Dada mmoja kwenda Kenya kumfanyia kazi za ndani. Baada ya kufika huko wakakorofishana na huyo Dada akamfukuza huyo ndugu yetu bila kumpa nauli ya kurudi huku Tanzania.
Sisi kama ndugu tumejaribu kufuatiria kwa jamaa yake na huyu Dada anayeishi hapa Dar es salaam, lakini akatukatisha tamaa kwa kutuambia kuwa huyo Dada anamdharau sana hawezi kumwambia kitu akafanya, hivyo tutafute namna nyingine ya kumsaidia mdogo wetu.
Tukaona kupitia hapa pengine tunaweza kupata msaada, kwa kuomba mwenye uwezo wa kutuelekeza tunaweza kuchukua hatua gani ukizingatia kuwa sisi hatuna uwezo wa kufika Kenya kutokana na hali ya kiuchumi kuwa si nzuri. Je kuna hatua gani za kisheria zinaweza kutusaidia?
Ahsante kwa kusoma ombi letu.
Mimi nimetumwa kwa niaba ya familia yetu nijiunge humu ili kunusuru ndugu yetu aliye katika hatari ya kupoteza maisha.
Mkasa wenyewe uko hivi;
Tuna mdogo wetu aliyevushwa na Dada mmoja kwenda Kenya kumfanyia kazi za ndani. Baada ya kufika huko wakakorofishana na huyo Dada akamfukuza huyo ndugu yetu bila kumpa nauli ya kurudi huku Tanzania.
Sisi kama ndugu tumejaribu kufuatiria kwa jamaa yake na huyu Dada anayeishi hapa Dar es salaam, lakini akatukatisha tamaa kwa kutuambia kuwa huyo Dada anamdharau sana hawezi kumwambia kitu akafanya, hivyo tutafute namna nyingine ya kumsaidia mdogo wetu.
Tukaona kupitia hapa pengine tunaweza kupata msaada, kwa kuomba mwenye uwezo wa kutuelekeza tunaweza kuchukua hatua gani ukizingatia kuwa sisi hatuna uwezo wa kufika Kenya kutokana na hali ya kiuchumi kuwa si nzuri. Je kuna hatua gani za kisheria zinaweza kutusaidia?
Ahsante kwa kusoma ombi letu.