Msafara wa Pinda wazua jambo Iringa
Atumia ndege mbili ikiwamo ya kukodi
na Francis Godwin, Iringa
ZIARA ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, mkoani Iringa imezua maswali mengi kuliko majibu kwa wakazi wa Mkoa wa Iringa, baada ya ndege mbili kutua katika Uwanja wa Ndege wa Nduli huku magari zaidi ya 57 yakishiriki katika msafara huo na barabara kufungwa kwa zaidi ya saa tano kwa ajili ya kusubiri msafara wake kupita.
Mbali ya ratiba ya ziara ya Waziri Mkuu kubadilishwa mara mbili baada ya awali viongozi na waandishi wa habari kupewa ratiba iliyowataka kukutana ofisi ya mkuu wa mkoa majira ya saa 2:30 asubuhi, ratiba hiyo ilibadilishwa na kuwa saa 1:30 kwa ajili ya kwenda Uwanja wa Ndege wa Nduli kwa mapokezi.
Hata hivyo, moja ya mambo ambayo baadhi ya watu waliofika kumpokea kiongozi huyo walionyesha kuhoji uwanjani hapo ni wingi wa magari, licha ya waziri mkuu kuwa mstari wa mbele kupinga kwa nguvu zote matumizi mabaya ya fedha za serikali, ikiwa ni pamoja na kununua mashangingi.
Kitendo cha msafara wake kuwa na ndege mbili, ikiwamo ndege ya serikali iliyombeba na timu yake pamoja na ndege ya kukodi kutoka nchini Kenya yenye namba za usajili 540 FLY AVITION ambayo ilitumiwa na wataalamu mbali mbali, wakiwamo waandishi wa habari na wataalamu kutoka Wizara ya Miundombinu wakiongozwa na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Omari Chambo.
Msafara wa Pinda ambao umeonyesha kuwa ni wa kihistoria ndani ya Mkoa wa Iringa uliondoka katika Uwanja wa Ndege wa Nduli majira ya saa 4:10 asubuhi kuelekea Ikulu ndogo kabla ya kuanza safari ya kuelekea Kijiji cha Mazombe, Wilaya ya Kilolo kwa ajili ya uzinduzi wa ukarabati wa barabara yenye urefu wa kilomita 150 kutoka Iyovi hadi Iringa.
Kwa muda wote huo kabla na wakati wa msafara wa waziri mkuu ukipita, mabasi ya abiria na magari yote yalikuwa yamezuiliwa kupita kwa muda wa zaidi ya saa tano, wakisubiri kumalizika kwa shughuli za uzinduzi wa barabara hiyo zilizokuwa zikifanyika pembezoni mwa barabara kuu ya Iringa - Dar es Salaam.
Pamoja na msafara wa waziri mkuu kutoka Uwanja wa Ndege wa Nduli kuwa na magari 54, yakiwemo ya watu binafsi, wabunge na viongozi wa vyama vya kisiasa, bado idadi ya magari ilionyesha kufikia 84 katika eneo la Mazombe, kwenye uzinduzi huo, baada ya magari mengine kutangulia katika eneo la uzinduzi kabla ya msafara wa waziri mkuu kufika.
Huu mzee alipochaguliwa kwenye utambulisho wake alisema yeye ni mtoto wa mkulima. Watu wengi nikiwemo tulihisi kwamba utendaji wake ungekuwa tofauti na possibly usio na gharama kubwa. Lakini mambo yake imekuwa ni kinyume kabisa.
Ziara zake nyingi ikiwemo ya Morogoro zinatugharimu pesa zetu nyingi taxpayers. Anyway binafsi sioni logic ya kutumia gharama zote hizo kuzindua ujenzi wa km 150 za barabara, sielewi kwenye kuifungua pesa ngapi zitatumika. Juzi boss wa huyu mzee ametangaza stimulus plan ya kibongobongo ambayo ina maswali mengi kuliko majibu.
Ushauri wangu ni kwamba wasiishie kwenye stimulus plan tu wapunguze pia gharama zisizo za lazima kama hii misafara ya kizamani kama hii katika credit crunch tuliyonayo. Maskini ambao ndio tunaoendesha serikali kwa kodi zetu mnatuonea jamani iweni na huruma kidogo.
Atumia ndege mbili ikiwamo ya kukodi
na Francis Godwin, Iringa
ZIARA ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, mkoani Iringa imezua maswali mengi kuliko majibu kwa wakazi wa Mkoa wa Iringa, baada ya ndege mbili kutua katika Uwanja wa Ndege wa Nduli huku magari zaidi ya 57 yakishiriki katika msafara huo na barabara kufungwa kwa zaidi ya saa tano kwa ajili ya kusubiri msafara wake kupita.
Mbali ya ratiba ya ziara ya Waziri Mkuu kubadilishwa mara mbili baada ya awali viongozi na waandishi wa habari kupewa ratiba iliyowataka kukutana ofisi ya mkuu wa mkoa majira ya saa 2:30 asubuhi, ratiba hiyo ilibadilishwa na kuwa saa 1:30 kwa ajili ya kwenda Uwanja wa Ndege wa Nduli kwa mapokezi.
Hata hivyo, moja ya mambo ambayo baadhi ya watu waliofika kumpokea kiongozi huyo walionyesha kuhoji uwanjani hapo ni wingi wa magari, licha ya waziri mkuu kuwa mstari wa mbele kupinga kwa nguvu zote matumizi mabaya ya fedha za serikali, ikiwa ni pamoja na kununua mashangingi.
Kitendo cha msafara wake kuwa na ndege mbili, ikiwamo ndege ya serikali iliyombeba na timu yake pamoja na ndege ya kukodi kutoka nchini Kenya yenye namba za usajili 540 FLY AVITION ambayo ilitumiwa na wataalamu mbali mbali, wakiwamo waandishi wa habari na wataalamu kutoka Wizara ya Miundombinu wakiongozwa na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Omari Chambo.
Msafara wa Pinda ambao umeonyesha kuwa ni wa kihistoria ndani ya Mkoa wa Iringa uliondoka katika Uwanja wa Ndege wa Nduli majira ya saa 4:10 asubuhi kuelekea Ikulu ndogo kabla ya kuanza safari ya kuelekea Kijiji cha Mazombe, Wilaya ya Kilolo kwa ajili ya uzinduzi wa ukarabati wa barabara yenye urefu wa kilomita 150 kutoka Iyovi hadi Iringa.
Kwa muda wote huo kabla na wakati wa msafara wa waziri mkuu ukipita, mabasi ya abiria na magari yote yalikuwa yamezuiliwa kupita kwa muda wa zaidi ya saa tano, wakisubiri kumalizika kwa shughuli za uzinduzi wa barabara hiyo zilizokuwa zikifanyika pembezoni mwa barabara kuu ya Iringa - Dar es Salaam.
Pamoja na msafara wa waziri mkuu kutoka Uwanja wa Ndege wa Nduli kuwa na magari 54, yakiwemo ya watu binafsi, wabunge na viongozi wa vyama vya kisiasa, bado idadi ya magari ilionyesha kufikia 84 katika eneo la Mazombe, kwenye uzinduzi huo, baada ya magari mengine kutangulia katika eneo la uzinduzi kabla ya msafara wa waziri mkuu kufika.
Huu mzee alipochaguliwa kwenye utambulisho wake alisema yeye ni mtoto wa mkulima. Watu wengi nikiwemo tulihisi kwamba utendaji wake ungekuwa tofauti na possibly usio na gharama kubwa. Lakini mambo yake imekuwa ni kinyume kabisa.
Ziara zake nyingi ikiwemo ya Morogoro zinatugharimu pesa zetu nyingi taxpayers. Anyway binafsi sioni logic ya kutumia gharama zote hizo kuzindua ujenzi wa km 150 za barabara, sielewi kwenye kuifungua pesa ngapi zitatumika. Juzi boss wa huyu mzee ametangaza stimulus plan ya kibongobongo ambayo ina maswali mengi kuliko majibu.
Ushauri wangu ni kwamba wasiishie kwenye stimulus plan tu wapunguze pia gharama zisizo za lazima kama hii misafara ya kizamani kama hii katika credit crunch tuliyonayo. Maskini ambao ndio tunaoendesha serikali kwa kodi zetu mnatuonea jamani iweni na huruma kidogo.