Brightman Jr
JF-Expert Member
- Mar 22, 2009
- 1,225
- 232
Habari za kuaminika nilizopata sasa hivi kutoka katika kijiji cha Matundasi wilayani Chunya Mbeya ni kwamba mwanachama mmoja wa CCM amefariki dunia kwa ajali ya gari aina lori na wengine wengi wakiwa wamejeruhiwa vibaya. Chanzo cha ajali waliokuwemo humo wanasema ni kitendo cha dreva kuongea na simu na huku akiwa ameachia usukani wa gari hilo ambalo lilikuwa katika mwendo mkali na kulikuwa na kona eneo hilo. Misafara hiyo ya wanachama ni kwa ajili ya kukutana mjini Chunya kufanya uchaguzi wa viongozi mbalimbali ambao majina yao yamepitishwa na NEC-CCM hivi majuzi.