Msaada wataalam na wenye uzoefu, nisaidieni mwenzenu tafadhali

Msema yote

JF-Expert Member
Mar 19, 2013
448
298
Poleni na shughuli za kutwa wana jamii bila shaka mu wazima wa afya, kwa upande wangu ni mzima kiafya ila kimawazo ni tatizo.

Naombeni nianze hivi, nina mchumba wangu alie mjamzto sasa kila atachokula yeye ni kutapika tu, kiukweli nashindwa kuelewa nifanyeje na hii hali inanichanganya sana, nimezungumza nae ili kujua kwa nini inatokea hivo anadai mwenyewe haelewi, hvo nikaamua nimtafute jamaa yangu mmoja hiv anipe ushaur nilivo mweleza akanambia hiyo ni hali ya kawaida kwa wajawazito nikasema ok (kwa sababu sina utaalam na mambo ya mimba), sasa jana mchumba wangu kanambia alienda hospitali kiukweli alionambia yameniogopesha na kunishtua, anadai wamemwambia kwa mwili alio nao ni lazima ajifungue kwa oparesheni, pia wamemwambia akiwa na mawazo sana anaweza pata kifafa cha mimba kitu ambacho kinaweza sababisha either mama au mtoto kufariki, vilevile anadai wamemshauri aitoe kwani kwa umbo lake ( mfupi japo si sana) si sahihi kwa sasa kubeba mimba.
Kiukweli napata maswali mengi kichwani bila majibu, maswali kama haya(chini) yananipa shida sana

**Sasa najiuliza ni umbo lipi lilo sahihi kubeba mimba
**Ni kwanini anatapika(mara kwa mara) kila anapokula chochote
**Je ni sahihi atoe hiyo mimba eti mpaka umbo litaporuhusu japo anamiaka 22(umri ambao sina hakika kama atakuwa tena)
**Je ni kweli atajifungua kwa oparesheni kama walivo mwambia.

NAOMBENI MNISAIDIE MAJIBU YA MASWALI YANGU HAPO JUU WAKUU, KIUKWELI SINA AMANI KABISA KWA HILI, TAFADHALI MZAA SI MAHALA PAKE, ASANTENI.
 
Sikiliza mzee sio kila hospitali ni wakweli wengine ni makanjanja wanaweza kukusababisha upate presha cjajua uko mkoa gani ila kama upo dar na kama upo vizuri financially nenda hospitali kubwa watakupa ushauri mzuri tu ukifika hizo hospitali ulizia kama wanae gynacoligist ni madaktari wakina mama na utapata taarifa nzuri tu ambazo hazikukwaza pia wanaweza kukupa na dawa ambayo inazuia kutapika kwani hta mke wangu kua anakutwa na hali hyo ila wanampa dawa kutapika kunasimama so do that.lakini pia hta kama upo mkoani nenda hospitali za mkoa uwaone hao wataalamu wa mambo ya kike na mambo yatakua poa.dont panick do tht na mwenyewe utaona
 
  • Umbo lake lipoje?Naomba ufafanuzi,je ni mnene?na kama ni mnene kiasi gani nahitaji kilos!
  • Kutapika au kichefchef ni hali ya kawaida kwa wajawazito..linaisha na jinsi ujauzito unavyokua
  • Kama wamemwambia atajifungua kwa operation lazima wamempa sababu nazo zaweza kuwa

  1. Ana fupa la pelvic jembamba/dogo na mtoto mkubwa
  2. Mtoto ana maji kwenye kichwa
  3. Ana matatizo kwenye njia ya uzazi,fuko la mtoto(placenta)linaziba njia au fuko linaweza kupasuka haraka kuliko matarajio
  4. Groups tofauti za damu zinaweza kuchangia mtoto azaliwe mapema kuliko matarajio n.k
 
  • Umbo lake lipoje?Naomba ufafanuzi,je ni mnene?na kama ni mnene kiasi gani nahitaji kilos!
  • Kutapika au kichefchef ni hali ya kawaida kwa wajawazito..linaisha na jinsi ujauzito unavyokua
  • Kama wamemwambia atajifungua kwa operation lazima wamempa sababu nazo zaweza kuwa

  1. Ana fupa la pelvic jembamba/dogo na mtoto mkubwa
  2. Mtoto ana maji kwenye kichwa
  3. Ana matatizo kwenye njia ya uzazi,fuko la mtoto(placenta)linaziba njia au fuko linaweza kupasuka haraka kuliko matarajio
  4. Groups tofauti za damu zinaweza kuchangia mtoto azaliwe mapema kuliko matarajio n.k

*Ni mwembamba ana kilo 42
*Sababu za kujifungua kwa oparesheni wamemwambia wenye maumbo kama yake nyonga znaweza kuwa na tatzo
 
Sikiliza mzee sio kila hospitali ni wakweli wengine ni makanjanja wanaweza kukusababisha upate presha cjajua uko mkoa gani ila kama upo dar na kama upo vizuri financially nenda hospitali kubwa watakupa ushauri mzuri tu ukifika hizo hospitali ulizia kama wanae gynacoligist ni madaktari wakina mama na utapata taarifa nzuri tu ambazo hazikukwaza pia wanaweza kukupa na dawa ambayo inazuia kutapika kwani hta mke wangu kua anakutwa na hali hyo ila wanampa dawa kutapika kunasimama so do that.lakini pia hta kama upo mkoani nenda hospitali za mkoa uwaone hao wataalamu wa mambo ya kike na mambo yatakua poa.dont panick do tht na mwenyewe utaona

Nashukuru mkuu, niko mkoa kesho ntajitahdbnifanye hvo
 
*Ni mwembamba ana kilo 42
*Sababu za kujifungua kwa oparesheni wamemwambia wenye maumbo kama yake nyonga znaweza kuwa na tatzo
wamemchecki nyonga ili kugundua ina matatizo au ni blah blah?nakushauri uende kwenye hospitali nyingine akachekiwe...na kama ana matatizo anatakiwa afanyiwe check up often na inshallah atajifungua salama...mpaka vimbilikimo wanazaa na ni wafupi.,..
 
wamemchecki nyonga ili kugundua ina matatizo au ni blah blah?nakushauri uende kwenye hospitali nyingine akachekiwe...na kama ana matatizo anatakiwa afanyiwe check up often na inshallah atajifungua salama...mpaka vimbilikimo wanazaa na ni wafupi.,..

Hawajamcheki, ameniambia wamemuangalia tu kwa macho bila kugusa wala kufanya vipimo. Asante sana kwa ushauri, ubarikiwe
 
Mambo haya ya ujauzito yasikie tu, me nmejifunza.

Mkuu tulia na MUNGU atakuwa pamoja nanyi.
 
huenda hakuenda hospital alienda kwa mganga wa kienyeji ndio akampa huo ushauli muhoji vizuri nilazima alienda kwa sangoma
 
Vipi mzee ulifanikiwa kwenda hospital for vipimo?

Ndio mkuu nilienda, nilipata faraja kubwa sana na walinieleza mengi mazuri ambayo kwa hakika yamenipa matumaini makubwa mnoo, sasa naamini tunaweza mpata mwanetu akiwa salama
 
Poleni na shughuli za kutwa wana jamii bila shaka mu wazima wa afya, kwa upande wangu ni mzima kiafya ila kimawazo ni tatizo.

Naombeni nianze hivi, nina mchumba wangu alie mjamzto sasa kila atachokula yeye ni kutapika tu, kiukweli nashindwa kuelewa nifanyeje na hii hali inanichanganya sana, nimezungumza nae ili kujua kwa nini inatokea hivo anadai mwenyewe haelewi, hvo nikaamua nimtafute jamaa yangu mmoja hiv anipe ushaur nilivo mweleza akanambia hiyo ni hali ya kawaida kwa wajawazito nikasema ok (kwa sababu sina utaalam na mambo ya mimba), sasa jana mchumba wangu kanambia alienda hospitali kiukweli alionambia yameniogopesha na kunishtua, anadai wamemwambia kwa mwili alio nao ni lazima ajifungue kwa oparesheni, pia wamemwambia akiwa na mawazo sana anaweza pata kifafa cha mimba kitu ambacho kinaweza sababisha either mama au mtoto kufariki, vilevile anadai wamemshauri aitoe kwani kwa umbo lake ( mfupi japo si sana) si sahihi kwa sasa kubeba mimba.
Kiukweli napata maswali mengi kichwani bila majibu, maswali kama haya(chini) yananipa shida sana

**Sasa najiuliza ni umbo lipi lilo sahihi kubeba mimba
**Ni kwanini anatapika(mara kwa mara) kila anapokula chochote
**Je ni sahihi atoe hiyo mimba eti mpaka umbo litaporuhusu japo anamiaka 22(umri ambao sina hakika kama atakuwa tena)
**Je ni kweli atajifungua kwa oparesheni kama walivo mwambia.

NAOMBENI MNISAIDIE MAJIBU YA MASWALI YANGU HAPO JUU WAKUU, KIUKWELI SINA AMANI KABISA KWA HILI, TAFADHALI MZAA SI MAHALA PAKE, ASANTENI.

kulingana na hali ya mchumba wako nilitegemea swali lako liwe ni umbo gani si sahihi kubeba mimba,kutokana na maelezo na hali ya mchumba wako ni sahihi kubeba mimba kwa umri alionao,shida inakuja kuwa...
....kama ni mfupi sana inakuwa vigumu kuzaa kwa njia ya kawaida inaaminika kuwa wanawake wafupi sana chini ya cm 150 na size ya kiatu 2 kwenda chini, nyonga zao mara nyingi zinakuwa ndogo japo si wooooote kabisa,kwa hivyo kichwa cha mtoto kupita kwenye nyonga inakuwa vigumu kitaalamu tunaita CPD(cephalo pelvic disproportion) kunakuwa hakuna uwiano wa kichwa cha mtoto na nyonga ya mama.Huenda ndo maana wakakwambia hivyo.

.....kwamba akiwaza sana atapata kifafa cha mimba hii ni kutokana tu kwamba kama atawaza sana anaweza kupanda presha ya kupata,prsha inapokuwa inapanda wakati wa uja uzito ni dalili za kupata kifafa cha mimba kama presha isipodhibitiwa.

.....kwamba ni sahihi kuitoa mimba siyo sahihi sababu kama aktashindwa kujifungua kawaida atafanyiwa operation,ni jambo la kawaida tu,huhitaji kumpoteza kiumbe huyo.
.........kutapika ni mabadiliko ya hormone lakini baadaye inaweza tulia kadri mimba inavyokua au kutumia dawa za kuzuia kutapika.
 
Back
Top Bottom