Wakuu naombeni msaada wenu wapi nitapata pumba za mpunga kwa wingi hapa dar. Tafadhali kama unafahamu na gharama zake utakuwa umenisaidia sana. Asanteni
Pumba kwa kawaida inapatikana mashine za kukoboa mpunga na hizi sana zipo mikoani mfano morogoro mjini. Wafanya biashara wanakoboa mpunga mikowani na kusafirisha mchele Dar kwa hivo upatikanaji wa pumba Dar utakuwa mdogo. Haya mawazo yangu tu,
Nataka kwa ajili ya kuchomea tofali ambazo nitazitengeneza kwa kutumia clay soil. Shambani kwangu nimepata bahati ya kuwa na vichuguu vikubwa viwili, so sioni haja ya kuhangaika na cement zilizo ghali kutengeneza tofali za cement.
Red clay bricks ni imara na zinapendeza sana, hudumu hadi kwa 50 yrs.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.