Msaada wakuu: Certified copies of academic certificates

Mwana Mtoka Pabaya

JF-Expert Member
Apr 22, 2012
15,118
16,470
Wakuu naomba msaada wa kuelewa wapi na nani anayecertify vyeti. Serikali imetoa tangazo kupitia sekretarieti ya ajira sasa kwenye masharti ya jumla kuna hiki kipengele (kwenye red)

GENERAL CONDITIONS
i. All applicants must be Citizens of Tanzania and not above 45 years old
ii. Applicants must attach an up-to-date current Curriculum Vitae (CV) having reliable contact postal address, e-mail address and telephone numbers.
iii. Applicants should apply on the strength of the information given in this advertisement.
iv. The title of the position applied for should be marked on the envelope; short of which will make the application invalid.
v. Applicants must attach their detailed relevant certified copies of Academic certificates:
- Postgraduate/Degree/Advanced Diploma/Diploma/Certificates.
- Postgraduate/Degree/Advanced Diploma/Diploma transcripts.
- Form IV and Form VI National Examination Certificates.
- Computer Certificate
- Professional certificates from respective boards

MASWALI YANGU:
1. Na haka kacheti kangu ka Computer nako ni Academic Certificate?
2. Nani ana certify hivyo vyeti vyenyewe? (Mamlaka iliyokitoa au mwanasheria)
3. Na ni gharama gani (estimate) ikiwa certification inafanywa na mwanasheria?

Ni hayo tu wakuu
 
sure, wanasheria, mawakili hizi ndio kazi zao, unawapelekea copy plus original ya vyeti vyako ambavyo unataka wavi certify, wanakugongea mhuri mkubwa pale kuonyesha kwamba, that is the realy copy of the original certificate, na huwa wana charge 5000 per cheti, kama upo hapa dar wapo wengi kama wahitaji nikuagizia ni PM
 
nenda mahakama ya wilaya au hakimu mkazi uwe na sh 3000 kisheria ni 1500 kwa nakala mahakani
ila kwa njaa za makarani na kama una vyeti vingi nenda na 5000
hakimu atacertify
kwa advocates wanachaji gali zaidi.
 
Nenda mahakama yeyote, onana na wale makarani watamaliza kila kitu..Ila huwa wanataja bei sana., ukiongea nao wanaeleweka manake hz pesa zinaenda mifukoni mwao. ila kwa vyeti vyote usiwape zaidi ya 5000..Ila ukienda kwa hao mawakili watakupiga bei knoma.
 
Asanteni wakuu, naona maluweluwe. Kwa hiyo kuomba kazi serikalini lazima uwe na mtaji. Kwanza niwe na nauli ya kutoka Mkoreha mpk Tandahimba mahakamani (5000 kwa boda boda) then niwape vyeti vyangu 6 halafu nisikilizie upepo watanitwanga ngapi, baada ya hapo nijumlishe 1500 ya stamp ili bahasha yangu ifike mjini.

Ili upate kazi inalazimu utume maombi mara kadhaa manake saa nyingine hata kuitwa huitwi...bora tuyaache. Asanteni sana
 
Asanteni wakuu, naona maluweluwe. Kwa hiyo kuomba kazi serikalini lazima uwe na mtaji. Kwanza niwe na nauli ya kutoka Mkoreha mpk Tandahimba mahakamani (5000 kwa boda boda) then niwape vyeti vyangu 6 halafu nisikilizie upepo watanitwanga ngapi, baada ya hapo nijumlishe 1500 ya stamp ili bahasha yangu ifike mjini.

Ili upate kazi inalazimu utume maombi mara kadhaa manake saa nyingine hata kuitwa huitwi...bora tuyaache. Asanteni sana

pole mkuu, nch inahtaji mapinduzi..
 
Wakati nchi nyingine ku-Certify vyeti au documents yoyote ni bure hapa kwetu tumefanya ndio biashara. Nchi kama South Africa ku-certify cheti unaweza kwenda Police, Posta ofisi, Ofisi za Serikali au hata kampuni za watu binafsi ili mradi uwe na Original certificate wanafanya hivyo.

Kwanini hizo Office za Serikali wasi-certify? Kila kitu Tanganyika ni pesa, kweli nchi ipo pabaya
[h=2]
[/h]
 
Its better ukaenda mahakama ya mwanzo au hata ya wilaya uliyo karibu nayo!!
Kawaida gharama yake kwa kila cheti ni TSH 1500/= na unatakiwa upewe receit!!
Lakini sasa kwa kuwa watu hatujui unakuta ukienda pale wanakupiga cha juu!!
FANYA HIVYO KAKA!!
Hata cheti cha Computer nacho ni part of academic certificates!!
Wewee nenda na copy za kila cheti pamoja na original zake then huyo hakimu atadeal na copy tu huku akilinganisha na original!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom