VUVUZELA
JF-Expert Member
- Jun 19, 2010
- 3,103
- 785
Nawasalimu tena kwa mara ya pili wakubwa shikamooni wadogo habari zenu.
Wakubwa naombeni msaada wenu wa mawazo,kuna mdada rafiki yangu na jirani yangu pia mumewe yuko nje ya nchi mie sikujua kumbe ana mwanaume anacheat nae,na ktk uhusiano wao mdada amepata mimba anataka aitoe ili kunusuru ndoa yake,alipomshirikisha jamaa anaecheat nae kuwa waitoe hy mimba jamaa kamjia juu sana na kumwambia hakuna kutoa na wala hajawahi kufanya hivyo! Ajabu sasa jamaa nae ana mke na watoto wanne!kwa sasa jamaa amesitisha mawasiliano yote ya simu na email hadi facebook kablock kisa hataki mimba itolewe,huyu mdada kachanganyikiwa alifanya siri lkn juzi kati hapa ilibidi anishirikishe kutaka ushauri,naombeni mawazo yenu juu ya huu utata wa hawa wenye ndoa.
Sasa kwani hata akitoa hiyo mimba si ataendelea ku-cheat tena.
Halafu kibaya zaidi yeye ni mke wa mtu ancheat bila condom!
Ushauri: Asitoe hiyo mimba na akawe mke wa pili wa huyo anayecheat nae kwani kuua ni dhambi kubwa sana. Ameshaisaliti ndoa yake kwa kucheat. Kaazi kwelikweli wanawake!!:coffee: