Akili Unazo!
JF-Expert Member
- Feb 18, 2009
- 3,930
- 4,893
Nina rafiki wa kaka yangu ambaye ana umri wa miaka 45 na ameoa na kubahatika kuwa na watoto wanne,wa kwanza ana miaka 18 kwasasa na wa mwisho ana mitano.Baada ya kupata hao watoto wote kwa pamoja walikubaliana kuwa idadi ya watoto walio nao inatosha hivyo wasiendelee na zoezi la uzazi tena.Hivyo wakawa wanatumia Contrception ya sindano kwa muda wa miaka minne sasa.
Sasa katika kipindi kisichotegemea huyu ndugu mkewe mwenye miaka arobaini sasa amepata/conceive na mimba yake kwa sasa ina miezi minne.
Kinachomtatiza huyu ndugu ni kwamba haikuwa mategemeo yake kupata mtoto mwingine kwa sasa na hayupo tayari kabisa,wakati huohuo mama yake mzazi anafurahia kwa mkwe wake kubeba mimba na kusema ni baraka kutoka kwa mwenyezi mungu.
Ndugu huyu amechanganyikiwa na kushindwa kuamua nini cha kufanya aache mkewe azae au aitowe.Kwa maamuzi yote hayo yanamchanganya kwa sababu alikuwa amepangilia kila kitu kwa ajili ya kusomesha watoto wake hao wanne na ndo nguvu nyingi alikuwa amezikweka huko kwa kila kitu.Amuzi la pili la kutoa mimba anachanganyikiwa kwa kuwa ndani ya miaka ishirini ya ndoa yake hajawahi kusikia wanandoa kutoa mimba hivyo uamuzi kuwa mgumu zaidi,na endapo ataamua kuendeleza uamuzi wa pili mama yake mzazi atamchukuliaje endapo akisikia kuwa mkwewe hana mimba tena?
WanaJf nawasilisha kwa ushauri na mawazo.
Sasa katika kipindi kisichotegemea huyu ndugu mkewe mwenye miaka arobaini sasa amepata/conceive na mimba yake kwa sasa ina miezi minne.
Kinachomtatiza huyu ndugu ni kwamba haikuwa mategemeo yake kupata mtoto mwingine kwa sasa na hayupo tayari kabisa,wakati huohuo mama yake mzazi anafurahia kwa mkwe wake kubeba mimba na kusema ni baraka kutoka kwa mwenyezi mungu.
Ndugu huyu amechanganyikiwa na kushindwa kuamua nini cha kufanya aache mkewe azae au aitowe.Kwa maamuzi yote hayo yanamchanganya kwa sababu alikuwa amepangilia kila kitu kwa ajili ya kusomesha watoto wake hao wanne na ndo nguvu nyingi alikuwa amezikweka huko kwa kila kitu.Amuzi la pili la kutoa mimba anachanganyikiwa kwa kuwa ndani ya miaka ishirini ya ndoa yake hajawahi kusikia wanandoa kutoa mimba hivyo uamuzi kuwa mgumu zaidi,na endapo ataamua kuendeleza uamuzi wa pili mama yake mzazi atamchukuliaje endapo akisikia kuwa mkwewe hana mimba tena?
WanaJf nawasilisha kwa ushauri na mawazo.