Prodigal Son
JF-Expert Member
- Dec 9, 2009
- 1,067
- 700
Ningeomba mnishauri ndugu zangu nafasi ya hawa watu kama mtu anataka kuoa au kuolewa. SHANGAZI, BABA MDOGO/MKUBWA PAMOJA NA WATOTO WAO.
Kwa kifupi Baba ameshatangulia mbele ya haki na kwa mila za huko kwa akina XPIN mtoto wa kwanza wa kiume ndo anatakiwa achukue nafasi ya Ubaba,ndio nilikabidhiwa ubaba.
Niliowataja hapo juu baba ndo aliwasaidia saana wao hata na baadhi ya watoto wao,familia yetu hatuna ule ukaribu nao since walikuwa hawampendi mama, na walikuwa wanamwogopa saana mzee, majuzi tu dada mkubwa akanifuata ( kama baba yake) akaniambia anataka afunge ndoa ikabidi nimpe mama taarifa, Ikabidi yeye awatarifu hao wandugu niliowataja hapo juu, kwa sasa hakuna amani kabisa kila mtu anaongea lake wanamlazimisha dada aende kijijini wazee wa ukoo wakambiwe, wapewe pombe, mahari ilipwe na mambo kibao.
Dada kanifuata ananiambia sasa afanyeje nikamwambia anipe muda kidogo, Baada ya kuwaza saana nimefikia maamuzi haya hatuendi Kijijini,,,, hatutafanya sherehe ya kumwaga badala yaka tutaandaa chakula tu cha jioni na kuepusha maneno harusi yake ataenda wadogo zake tu wa kike,,hao mashangazi na watoto wao nimeona ni jambo la busara kuwa ignore
Naamini hapa Jamvini wapo wazee ( namaanisha watu wenye busara ) naomba ushauri wenu kabla sijamjulisha dada maamuzi niliyofikia.
natanguliza shukrani