Msaada wa kuelimishwa jinsi ya kufika mkoa mpya wa katavi..

sosoliso

JF-Expert Member
May 6, 2009
8,539
9,462
Wana JF naomba mnijuze jinsi ya kusafiri na basi kutoka Dar es Salaam kwenda mkoa mpya wa Katavi.. Pia gharama za nauli.. Au mwenye contacts za mabasi yanayoenda huko na haswa Sumri.. Nimejitahidi kutafuta kwenye net nimewakosa.. So naomba kwa anaejua anisaidie kwa hili.. The sooner the better..

UPDATE
Wakuu ninashukuru kwa msaada wenu.. Nilifanikisha safari yangu kwenda Mpanda kupitia Mbeya Tunduma.. Sumbawanga mpaka Mpaka.. Kuondoka nilipita Tabora na kuunganisha mpaka Dar.. Nilichokiona huko ni kutokuwapo kwa lami kuanzia Tunduma mpaka Mpaka Mpanda.. Japo kuna makampuni yanatengeneza barabara nimeambiwa karibu mwaka sasa hakuna kipande chochote kilichokamilika.. Na vile vile kutoka Mpanda mpaka Manyoni (kupitia Tabora) kote ni barabara ya vumbi japo nako barabara inatengenezwa muda hakuna kipande ambacho kimeshakamilika..
Naambatanisha na picha za Mpanda

View attachment 68686
View attachment 68687
View attachment 68689
Hii ndio nyumba ya Mh. Waziri Mkuu pale Mpanda..

View attachment 68693
Ndio barabara yenyewe hiyo..
View attachment 68695
View attachment 68698
Kamanda anamwaga sera kwenye basi.. Hapo anasikiliza maswali toka kwa abiria.. just an ordinary guy..!
IMG00270-20121014-1030.jpg
Kweli Mpanda ni CDM kwenda mbele..
IMG00284-20121015-1339.jpg

Nawacilisha...


 
Wana JF naomba mnijuze jinsi ya kusafiri na basi kutoka Dar es Salaam kwenda mkoa mpya wa Katavi.. Pia gharama za nauli.. Au mwenye contacts za mabasi yanayoenda huko na haswa Sumri.. Nimejitahidi kutafuta kwenye net nimewakosa.. So naomba kwa anaejua anisaidie kwa hili.. The sooner the better..
Ukipita mbeya route ni ndefu sana,njia raisi panda basi Dar-Tabora,ukifika Tabora unaweza kupanda treni to Mpanda ni safari ya 12 hrs na ukitaka kuwa comfortable kata second class behewa jirani na buffet,unasafiri huku unaburudika,nauli ni aproximatelly 20,000 Tshs,kama sio siku ya treni uwa kuna mabasi toka Tabora kwenda Mpanda kupitia Ipole na Inyonga,ni safari ya masaa kama 8 hivi na nauli ni approxiamatelly 20,000 tshs.Nauli ya Dar-Tabora ni approximatelly 50,0000 tshs.Kama huna hela ya kutosha kata ticket ya treni toka Dar- Mpanda via Tabora,kwa third ni kama elfu 30 na inachukua siku 3.Lakini kama pochi yako ni nzuri unaruka na precision Dar -Mwanza,ukifika Mwanza unapanda ndege ya Auric ambayo ni shs 550,000 kufika Mpanda.UNHCR wana ndege yao kati ya Mwanza - Mpanda lakini kwa vile hawafanyi biashara kupanda hadi uwe mfanyakazi wa serikali na unasafiri kikazi,nauli ni approx laki tatu na nusu na inabidi booking ufanyie ofisi yao ya Dar.
 
Ukipita mbeya route ni ndefu sana,njia raisi panda basi Dar-Tabora,ukifika Tabora unaweza kupanda treni to Mpanda ni safari ya 12 hrs na ukitaka kuwa comfortable kata second class behewa jirani na buffet,unasafiri huku unaburudika,nauli ni aproximatelly 20,000 Tshs,kama sio siku ya treni uwa kuna mabasi toka Tabora kwenda Mpanda kupitia Ipole na Inyonga,ni safari ya masaa kama 8 hivi na nauli ni approxiamatelly 20,000 tshs.Nauli ya Dar-Tabora ni approximatelly 50,0000 tshs.Kama huna hela ya kutosha kata ticket ya treni toka Dar- Mpanda via Tabora,kwa third ni kama elfu 30 na inachukua siku 3.Lakini kama pochi yako ni nzuri unaruka na precision Dar -Mwanza,ukifika Mwanza unapanda ndege ya Auric ambayo ni shs 550,000 kufika Mpanda.UNHCR wana ndege yao kati ya Mwanza - Mpanda lakini kwa vile hawafanyi biashara kupanda hadi uwe mfanyakazi wa serikali na unasafiri kikazi,nauli ni approx laki tatu na nusu na inabidi booking ufanyie ofisi yao ya Dar.

Ahsante sana Mkuu.. Ila safari yangu bajeti yake imefinywa.. Kwa hiyo kwa usafiri wa ndege haiwezekani.. Halafu tarehe 15/10/2012 natakiwa niwe pale Katavi mkuu.. Hiyo ya tabora kama ningekuwa na muda ingekuwa njema.. Labda una ufahamu na hii nilioambiwa ya kupitia Mbeya - Tunduma.. Naomba unijuze.. Nategemea kusafiri tarehe 12/10/2012..
 
pitia tabora,dar-tabora ni sh.45,000 kwa basi la nbs,au 35,kwa airbus,unafika tabora ucku saa 4,kesho asubuhi yake unapanda basi la nbc,au airbus kwa sh.20,000 hadi mpanda unafika saa 8 mchana.kupitia sumbawanga ni njia ndefu sana na barabara zenyewe ni mbaya,na gharama yake ni kubwa zaidi.na ukitoka leo dar kesho mchana upo mpanda,usafiri wa train hauaminiki hata kidogo,mabasi tbr-mpanda ni kila cku na ni magari 2 kila cku.
 
pitia tabora,dar-tabora ni sh.45,000 kwa basi la nbs,au 35,kwa airbus,unafika tabora ucku saa 4,kesho asubuhi yake unapanda basi la nbc,au airbus kwa sh.20,000 hadi mpanda unafika saa 8 mchana.kupitia sumbawanga ni njia ndefu sana na barabara zenyewe ni mbaya,na gharama yake ni kubwa zaidi.na ukitoka leo dar kesho mchana upo mpanda,usafiri wa train hauaminiki hata kidogo,mabasi tbr-mpanda ni kila cku na ni magari 2 kila cku.

Mkuu nimekupata hapo.. Nafikiria kuufuata ushauri wako.. Kesho ntakwenda pale Ubungo kufanya mpango wa safari.. Ila ni safari ndefu sana..
 
Back
Top Bottom