Msaada wa kuandika madai ya BIMA

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,810
15,398
Wakuu heshima kwenu.
Ninaomba mwenye utaalamu wa kuandika madai ya Bima anisaidie. Nilipata ajali ya kugongwa na gari Octoba mwaka jana na hatua zote za kipolisi zimetimia. mpaka sasa bado kesi haijaenda mahakamani baada ya dereva kukimbia. hivyo nimepewa nakala zote za shauri hilo na Polisi makao makuu ambazo zinaniwezesha kuanza mchakato wa madai yangu ya Bima. lakini tatizo nililo nalo ni kwamba sina utaalamu wa kundika madai hayo.
Nilivunjika mkono wa kulia karibu na kiganja.

Habari ya ajali yangu iliwahi kuandika hapa na memba mwenzangu kwa kuisoma waweza kubofya hapa:

https://www.jamiiforums.com/mahusia...mtambuzi-wa-jf-amepata-ajali-asubuhi-hii.html

Natarajia kupata msaada wenu.

pamoja Daima
 
Kwa kuanzia tu ni lazima uwe unajua mpaka sasa umetumia kiasi gani nikimaanisha uwe na ushahidi wa gharama zote tangu ulipogongwa eneo la ajari hadi matibabu yake. Ukishaweka sawa vitu hivyo ni lazima ujue hiyo daladala bima yake ni ya kampuni gani ili uweze kwenda kudai fidia ya hasara uliyoipata. Hata kama dereva wa gari alikimbia ninaamini kuwa hiyo gari inajulikana ni ya nani kwa hiyo hapo sioni ni kwa nini kesi haijaenda mahakamani kwani mmiliki wa gari ni lazima awajibike pia. Anyway cha msingi ni kwenda kampuni aliyokatia bima na kisha utapewa form ya madai ili uweze kufuatilia malipo yako.
 
Kwa kuanzia tu ni lazima uwe unajua mpaka sasa umetumia kiasi gani nikimaanisha uwe na ushahidi wa gharama zote tangu ulipogongwa eneo la ajari hadi matibabu yake. Ukishaweka sawa vitu hivyo ni lazima ujue hiyo daladala bima yake ni ya kampuni gani ili uweze kwenda kudai fidia ya hasara uliyoipata. Hata kama dereva wa gari alikimbia ninaamini kuwa hiyo gari inajulikana ni ya nani kwa hiyo hapo sioni ni kwa nini kesi haijaenda mahakamani kwani mmiliki wa gari ni lazima awajibike pia. Anyway cha msingi ni kwenda kampuni aliyokatia bima na kisha utapewa form ya madai ili uweze kufuatilia malipo yako.
Gharama zote za matibabu zimelipwa na mwajiri wangu. Kwa hiyo ina maana hakuna nitakacholipwa?
 
Wakuu heshima kwenu.
Ninaomba mwenye utaalamu wa kuandika madai ya Bima anisaidie. Nilipata ajali ya kugongwa na gari Octoba mwaka jana na hatua zote za kipolisi zimetimia. mpaka sasa bado kesi haijaenda mahakamani baada ya dereva kukimbia. hivyo nimepewa nakala zote za shauri hilo na Polisi makao makuu ambazo zinaniwezesha kuanza mchakato wa madai yangu ya Bima. lakini tatizo nililo nalo ni kwamba sina utaalamu wa kundika madai hayo.
Nilivunjika mkono wa kulia karibu na kiganja.

Habari ya ajali yangu iliwahi kuandika hapa na memba mwenzangu kwa kuisoma waweza kubofya hapa:

https://www.jamiiforums.com/mahusia...mtambuzi-wa-jf-amepata-ajali-asubuhi-hii.html

Natarajia kupata msaada wenu.

pamoja Daima

polee sana ndugu ila ninavyojua hauwezi kushinda kesi ya bima mpaka yule dereva aliyekugonga apatwe na kosa la jinai, therefore among the requirement to win insurance case is through production of judgment which hold the driver liable for criminal offence connecting with ur case, ukikutana na advocate anayejua mambo ya insurance vizuri atakupiga preliminary objection na mchezo unaishia hapo
 
polee sana ndugu ila ninavyojua hauwezi kushinda kesi ya bima mpaka yule dereva aliyekugonga apatwe na kosa la jinai, therefore among the requirement to win insurance case is through production of judgment which hold the driver liable for criminal offence connecting with ur case, ukikutana na advocate anayejua mambo ya insurance vizuri atakupiga preliminary objection na mchezo unaishia hapo
Kwa hiyo ndio imekula kwangu?
 
Kwa hiyo ndio imekula kwangu?

Anza na kutambua uhalali wa gari iliyokugonga, Kama mamba iko sahihi hatua ya pili nenda kwenye regulatory authority ya bima kwani kila gari lazima iwe na cover at least third party, hapo Utajua owner wa gari na insurer. Ukiwajua hao unalala nao mbele, in case of third party insurance nakala ya traffic case sio muhimu, cha muhimu ni kuwa, at the time of the accident the insurance was valid. Kazi itakayobaki ni kuthibitisha negligence au recklessness.
 
Anza na kutambua uhalali wa gari iliyokugonga, Kama mamba iko sahihi hatua ya pili nenda kwenye regulatory authority ya bima kwani kila gari lazima iwe na cover at least third party, hapo Utajua owner wa gari na insurer. Ukiwajua hao unalala nao mbele, in case of third party insurance nakala ya traffic case sio muhimu, cha muhimu ni kuwa, at the time of the accident the insurance was valid. Kazi itakayobaki ni kuthibitisha negligence au recklessness.
Ahsante mkuu, document zote ninazo na hata owner wa gari nimeshaonana naye tatizo tu ni derevaambaye amekimbia na mmiliki wa kampuni ya Bima niliwahi kuonana naye kwenye function fulani na nilipomueleza alinipa business card yake na kunishauri niandike claim ya madai nikieleza kwa nini nataka nilipwe then ataangalia kama madai yangu yana mashiko. alinitahadharisha kwamba si lazima nikipata ajali nilipwe hiyo itategemea na athari niliyoipata kama ina mashiko then watalipa.

Tatizo langu mimi sio mtaalamu wa kuandika madai ya Bima ninachohitaji ni muongozo.
 
Pole mkuu......nadhani ukianzia IFM pale wana walimu wanafundisha hii kozi ya Insurance na consultancy ni sehemu ya kazi ya mwana taaluma yoyote. Ni matumaini yangu kuwa ufumbuzi wa kitaalamu waweza kupatikana kuanzia pale. Na yawezekana humu pia tunaweza kupata links zao au wao wenyewe

Wish you all the best
 
Fanya yafuatayo:
1. Hakikisha unayo "Insurance Cover note" ya Gari iliyokugonga
2. Nenda na hiyo cover note kwa Bima ya Gari iliyokugomga, waambie unataka wakupatie " Claim Form"
3. Jaza Claim form yako na uweke viambatanisho vyako vyote vya madai unayotaka wakulipe.
4. Baada ya kujaza Claim Form irejeshe kwenye kampuni ya Bima ulikoichukulia.
5. Waombe wakupatie Claim number ya fail lako.
6. Waulize kama kuna uthibitisho/maelezo mengine yoyote wayohitaji
7. Waombe wakupatie contact person utakaekuwa unawasiliana nae.
8 Endelea kuatilia majibu yako

Wasalaam,
 
Wakuu heshima kwenu.
Ninaomba mwenye utaalamu wa kuandika madai ya Bima anisaidie. Nilipata ajali ya kugongwa na gari Octoba mwaka jana na hatua zote za kipolisi zimetimia. mpaka sasa bado kesi haijaenda mahakamani baada ya dereva kukimbia. hivyo nimepewa nakala zote za shauri hilo na Polisi makao makuu ambazo zinaniwezesha kuanza mchakato wa madai yangu ya Bima. lakini tatizo nililo nalo ni kwamba sina utaalamu wa kundika madai hayo.
Nilivunjika mkono wa kulia karibu na kiganja.

Habari ya ajali yangu iliwahi kuandika hapa na memba mwenzangu kwa kuisoma waweza kubofya hapa:

https://www.jamiiforums.com/mahusia...mtambuzi-wa-jf-amepata-ajali-asubuhi-hii.html

Natarajia kupata msaada wenu.

pamoja Daima
Mku. WCF vipi.
 
Back
Top Bottom