Mwanantala
Senior Member
- May 13, 2010
- 130
- 26
Heshima mbele wakuu! Naleta mbele yenu maombi yangu ya mwongozo wa kisheria juu ya mwenendo sahihi wa mashtaka katika hili: Jirani yangu aliomba nimkopeshe shilingi laki moja na nusu mnamo Juni mwaka huu na aliahidi kuzirejesha mara baada ya mshahara kutoka wa mwezi husika kutoka. Nilimpatia pesa hizo kama alivyohitaji. Muda ulipowadia hakutimiza ahadi na badala yake akanidanganya kwamba ameomba mkopo nmb benki na hivyo nimpe laki nne na nusu ili akamilishe taratibu za huo mkopo ambao angetumia sehemu yake kunilipa jumla ya laki sita nilizomkopesha. Nikampa. Cha kusikitisha toka nimpe hela zangu ameanza kuonyesha kunitapeli. NAOMBA WAKUU MNIELEKEZE JINSI YA KUPATA HAKI YANGU.