Nyati
JF-Expert Member
- Mar 6, 2009
- 2,489
- 1,813
Wakuu heshima mbele
Mwanzoni mwa mwezi septemba nilikuwa na sherehe ya harusi. Kama ilivyo kawaida watoa huduma mbali mbali walijitokeza kuomba kutoa huduma katika sherehe hiyo. Walijitokeza wanne katika huduma ya Video na picha za mnato. Bei kati ya 400,000 wachini na wa juu 900,000/=.
Wajumbe walikubaliana kuwa yule wa 900,000/- apewe kwa jinsi alivyojinadi kuwa yeye ni professional, pia walidai kuwa gharama ina-determine ubora ya kitu. Alihahidi pia kutoa huduma ya picha za mnato kama offer. Aliahidi kuleta screen mbili ukumbini (live) na kutoa DVD na VHS tapes baada ya wiki moja tu, ahadi zote hizi zilitolewa kwa maneno.
Jamaa akapewa tender bila kuwa na written agreement. Siku ya harusi alifika na kupiga picha za video kama alivyoahidi na screen mbili pia alizileta, picha za mnato alipiga mtu mwingine aliyeletwa naye. Ndani ya wiki moja hivi jamaa alileta picha za mnato ( Yule wa pili). Lakini DVD na VHS zikaanza kuwa hadithi za alinacha, mara hivi mara vile. Mara zote amekuwa akiahidi atatoa siku fulani na siku ikifika ni hadithi kwa kwenda mbele.
Akawa anafuatiliwa ofisini kwake maeneo ya Sea view mara kwa mara. Mara ya mwisho akadai kuwa yeye yupo Zanzibar, ndipo mmoja wa vijana pale ofisini kwao akanitaarifu kuwa huyu jamaa alipata tender siku ya pili ya harusi husika, na baada ya kukosa tapes akafuta overwrite moja ya tape za harusi yetu, na hivyo kupoteza matukio yote muhimu ya kanisani , na pia ukumbini kama vile utambulisho wa wazazi wa pande zote mbili, kutoa nasaha n.k. Hivyo yeye anayo tape aliyoweka baada ya ile ya kwanza kwisha ambayo ina matukio ya kutoa zawadi, kufungua muziki tu na kuondoka ukumbini. Mtoa taarifa alihadharisha kuwa kuna uwezekano na hiyo akaifuta pia kwani ndizo zake. Yule kijana akalaumu kwa nini alilipwa pesa yote, akasema kuwa huyu ukishamlipa basi umeumia kwani uwa hakujali tena na vile vile ni mtoto wa kigogo hivyo umeumia. Akadai watu wengi kwa kutokujua huwa wanajuta. Taarifa hii sikuiamini hata kidogo, kwani haiingii akilini, lakini siku zinavyozidi kwenda naanza kupata wasi wasi hivi sasa ni karibu mwezi wa pili bado anapiga chenga.
Sasa naomba ushauri kama kuna sheria yeyote inayoweza kutumika dhidi yake (Ikitokea ikawa ni kweli) kwani kama nilivyoeleza pale juu hakukuwa na mkataba wa maandishi, bali makubaliano ya maneno tu ingawa kuna mwanakamati aliyempigia debe kwa sana. Na sasa amesema asimpigiwe simu wala nini bali yeye akiwa tayari atalete hivyo vitu. Naomba ushauri hiki kitu ni cha kweli kabisa wana jamvi.
Mwanzoni mwa mwezi septemba nilikuwa na sherehe ya harusi. Kama ilivyo kawaida watoa huduma mbali mbali walijitokeza kuomba kutoa huduma katika sherehe hiyo. Walijitokeza wanne katika huduma ya Video na picha za mnato. Bei kati ya 400,000 wachini na wa juu 900,000/=.
Wajumbe walikubaliana kuwa yule wa 900,000/- apewe kwa jinsi alivyojinadi kuwa yeye ni professional, pia walidai kuwa gharama ina-determine ubora ya kitu. Alihahidi pia kutoa huduma ya picha za mnato kama offer. Aliahidi kuleta screen mbili ukumbini (live) na kutoa DVD na VHS tapes baada ya wiki moja tu, ahadi zote hizi zilitolewa kwa maneno.
Jamaa akapewa tender bila kuwa na written agreement. Siku ya harusi alifika na kupiga picha za video kama alivyoahidi na screen mbili pia alizileta, picha za mnato alipiga mtu mwingine aliyeletwa naye. Ndani ya wiki moja hivi jamaa alileta picha za mnato ( Yule wa pili). Lakini DVD na VHS zikaanza kuwa hadithi za alinacha, mara hivi mara vile. Mara zote amekuwa akiahidi atatoa siku fulani na siku ikifika ni hadithi kwa kwenda mbele.
Akawa anafuatiliwa ofisini kwake maeneo ya Sea view mara kwa mara. Mara ya mwisho akadai kuwa yeye yupo Zanzibar, ndipo mmoja wa vijana pale ofisini kwao akanitaarifu kuwa huyu jamaa alipata tender siku ya pili ya harusi husika, na baada ya kukosa tapes akafuta overwrite moja ya tape za harusi yetu, na hivyo kupoteza matukio yote muhimu ya kanisani , na pia ukumbini kama vile utambulisho wa wazazi wa pande zote mbili, kutoa nasaha n.k. Hivyo yeye anayo tape aliyoweka baada ya ile ya kwanza kwisha ambayo ina matukio ya kutoa zawadi, kufungua muziki tu na kuondoka ukumbini. Mtoa taarifa alihadharisha kuwa kuna uwezekano na hiyo akaifuta pia kwani ndizo zake. Yule kijana akalaumu kwa nini alilipwa pesa yote, akasema kuwa huyu ukishamlipa basi umeumia kwani uwa hakujali tena na vile vile ni mtoto wa kigogo hivyo umeumia. Akadai watu wengi kwa kutokujua huwa wanajuta. Taarifa hii sikuiamini hata kidogo, kwani haiingii akilini, lakini siku zinavyozidi kwenda naanza kupata wasi wasi hivi sasa ni karibu mwezi wa pili bado anapiga chenga.
Sasa naomba ushauri kama kuna sheria yeyote inayoweza kutumika dhidi yake (Ikitokea ikawa ni kweli) kwani kama nilivyoeleza pale juu hakukuwa na mkataba wa maandishi, bali makubaliano ya maneno tu ingawa kuna mwanakamati aliyempigia debe kwa sana. Na sasa amesema asimpigiwe simu wala nini bali yeye akiwa tayari atalete hivyo vitu. Naomba ushauri hiki kitu ni cha kweli kabisa wana jamvi.