Msaada wa kisheria juu ya eviction/upangaji

Kapuku83

Senior Member
Sep 8, 2012
146
35
Wadau mwana jamvi mwenzenu nina mzozo na mwenye nyumba yangu na ninahitaji msaada wenu wa haraka!land lord wangu nilimpatia hela ya miezi minne katika miezi sita,na hela ya miezi hiyo minne inaishia tarehe 13 October 2012,tulikubaliana kua baada ya hela yangt ya miezi minne kuisha itanipasa kuondoka na kumkabidhi nyumba yake kwa kua ahitaji tena kuendelea na mimi,cha ajabu ni kua,jana amenipigia simu na kuniambia kua ameshachukua hela ya mtu hivyo inanipasa kuhama tarehe 1 October 2012 na pesa iliyobaki ya wiki moja atanirudishia!mimi sijajiandaa kuhama mpaka tarehe 10 ndio natakiwa kuingia kwenye nyumba mpya!je wadau nifanye taratibu gani ili asije kunitoa kwa nguvu hiyo tarehe 1?natanguliza shukrani zangu
 
mna mkataba wa makubaliano ya mwanzo?kisheria nadhan hana jeuri ya kukutoa kwa style iyo.ok 2subiri wadau zaidi.
 
mna mkataba wa makubaliano ya mwanzo?kisheria nadhan hana jeuri ya kukutoa kwa style iyo.ok 2subiri wadau zaidi.

Mkataba upo wa awali ambao uliisha june,ndio nikampa hela ya miezi minne ambayo inaishia 13 october,kwa hii miezi minne hakutoa mkataba,maana yuko mkoani mbali na mimi ninapoishi
 
mna mkataba wa makubaliano ya mwanzo?kisheria nadhan hana jeuri ya kukutoa kwa style iyo.ok 2subiri wadau zaidi.

Mkuu pole sana na sakata lako,na mimi yalinisibu varangati na mwenye nyumba wangu japo ni tofauti na lako kidogo,lakini nilipata ushauri wa maana humu humu jamihi forums na nikautumia,mwenye nyumba alikua mdogo mwenyewe!naamini utapata ushauri wa kitaalamu humu na utakua in a safe side!hawa wenye nyumba ni trouble kweli kweli,na hii yote nadhani kwa kua sheria za ardhi haziko wazi
 
Sheria zipo wazi either wewe au yeye unatakiwa utoe notice ya siku 30.chini ya hapo hawezi chochote ni kelele tu za lessor
 
Pole sana chief, asikusumbue huyo cha msingi we una document ambayo mulikuabaliana mpaka 13 Oct. Au hamkuandikishiana?

Sheria inalzimu yeye kama kakatisha mkataba basi akutafutie nyumba ili uweze kumpisha maana huitaji hela na Ndo maana ulilipia mpaka hiyo 13 Oct la hasha basi awe mpole tu ila u must be strong...



founder of www.oric.co.tz, skype: alfred.kohi, 0784800989
 
Back
Top Bottom