Wadau mwana jamvi mwenzenu nina mzozo na mwenye nyumba yangu na ninahitaji msaada wenu wa haraka!land lord wangu nilimpatia hela ya miezi minne katika miezi sita,na hela ya miezi hiyo minne inaishia tarehe 13 October 2012,tulikubaliana kua baada ya hela yangt ya miezi minne kuisha itanipasa kuondoka na kumkabidhi nyumba yake kwa kua ahitaji tena kuendelea na mimi,cha ajabu ni kua,jana amenipigia simu na kuniambia kua ameshachukua hela ya mtu hivyo inanipasa kuhama tarehe 1 October 2012 na pesa iliyobaki ya wiki moja atanirudishia!mimi sijajiandaa kuhama mpaka tarehe 10 ndio natakiwa kuingia kwenye nyumba mpya!je wadau nifanye taratibu gani ili asije kunitoa kwa nguvu hiyo tarehe 1?natanguliza shukrani zangu