Msaada wa huyu mwenzangu please!!

Papizo

JF-Expert Member
Feb 24, 2008
4,944
1,431
Habari jamani...Nadhani hapa nitapata majibu mazuri na ya maana kuhusu hili swala.....Problem ni kwamba hapa nilipo nina demu wa kigambia ambaye nilikutana nae hapa ninapoishi,kukutana tulikokutana ni kwamba sio mimi nilimtongoza bali yeye alikuwa na interest na mimi toka mda mrefu sana ila alikuwa anashindwa kuniambia saa zingine tukikutana face to face huwa ananichekea na kuniuliza maswali tofauti ila nilikuwa sijajua zaidi sasa ikafikia kipindi akamuuliza rafiki yangu kuhusu mimi tabia yangu na nipoje....sasa siku nipo break baada ya kazi akanikuta nimekaa mahali akaanza kuniuliza wapi nimetokea I mean nchi gani vitu kama hivyo....Mimi sikumchelewesha pale pale kwa sababu nilishajua nini anataka nikaweka mambo sawa usiku wa hiyo siku nikawasiliana nae kwenye simu nikaongea nae sana na tukafahamiana zaidi na mapenzi yetu yakaanza hapo,Sasa kitu ambacho nashindwa kuelewa ni kwamba amebadilika ghafla na tulikuwa tunakwenda out tunafurahi pamoja lakini sasa hivi hataki tena nikimuomba tuonane analeta mambo mengi bora tusionane ...Na alivyokuwa na problem mimi nilikuwa mwepesi sana kumsaidia pamoja alikuwa haniombi hela pia yeye bado yupo university na anafanya kazi part-time.Sasa katika mazungumzo yangu nimewahi kumgusia kama mara 3 kuhusu mambo fulani nadhani hapo mmeelewa vizuri....Sasa sikujua kabisa yeye huwa hapendi hayo mambo na nikajiuliza je mapenzi ni nini?Nikashangaa sana sasa akaja kumwambia rafiki yangu kwamba eti mapenzi sio pesa wakati huwa namsaidia muda mwingine hata hela ya bus pass ya kwendea shule au kununulia bidhaa ndogo ndogo huwa anakosa inabidi nitoe nimpe,pia yeye anasema kwamba hatopenda kufanya hicho kitendo kutokana na ex-bf wake alivyomfanya maana alimkamua then akaingia mitini so hatoamini tena wanaume,ila hicho kitendo hajakataa kufanya atafanya lakini mpaka atakapo niona msimamo wangu upo vipi, alianza kunibadilikia simu akawa hapigi tena,messeg hatumi tena na mawasiliano kapunguza kabisa ila sikujua zaidi problem ni nini mpaka baada ya kusikia kwa rafiki yangu ndio nikajua..Pia nilivyomuona yupo vile nilimuuliza whats wrong lakini akasema ohh hamna kitu.Sasa mimi nikamuomba msamaha kwa sababu kwanza nampenda na ametulia sana nikawambia kwamba nipo tayari kuwa na wewe bila hicho kitendo ila naona mwenzangu bado kama hahitaji mawasiliano na mimi na hata nikimtumia messeg hata 15 kwa siku basi atajibu 2 au 1 na ukiangalia hapo anasimu ya contract sasa wadau mnanishauri vipi??Niachie ngazi pamoja nitaumia au nimshaurije mwenzangu aweze kurudi katika hali ya kawaida kama zamani?Maana najaribu kuwa karibu nae sana tena sana lakini naona mwenzangu hana interest...Sasa wadau mnanishauri nifanye nini??

N.B nahitaji ushauri please sio utani ndugu zangu!
 
Kwa maoni yangu naona ni bora tu umuulize muhusika. Je, kulikoni mbona umepunguza mawasiliano yetu sana ukilinganisha na siku za nyuma? Mbona hatutoki tena kama zamani ambapo wote tulikuwa tunafurahi kuwa pamoja? Kama kuna chochote nilichofanya na kukuudhi ni kipi? Na hiyo ya kumuomba samahani naona ni vizuri kuendelea nayo labda anaweza akabadilisha mawazo yake lakini kwa maoni yangu hasa ukitilia maanani kwamba unampenda ni mapema mno kuachia ngazi kabla ya kusikia kauli yake mwenyewe kuhusu nini kilichomfanya abadilike na kama kuna chochote unachoweza kufanya ili arudie tabia yake ya zamani kabka ya kubadilika. Kila la heri.
 
Pole mwana ila hiyo mbona cyo issue kama vipi na we rudi nyuma kwanza huenda umeenda haraka sana,huenda cku ulipokubaliwa urafiki then next day ukaomba game hapo huenda ndo ulipokoroga.
Ila we c mtu mzima bana angalia kile unachoweza kufanya na ufanye kurejesha hilo pendo ukishindwa kurejesha replacement inakuhusu!
 
Huyu msichana ameshastuka kwamba wewe nia yako ni kula tunda then umuuache. Kama ulivyosema alikuwa na ex-bf alikula tunda halafu akamuuacha, hivyo hiyo inamuuma sana kwa msichana mwenye msimamo.Hataki tena kurudia kosa, maana baadhi ya wanaume ndio zao anakuja na gia ya kuoa then akishapata kile kitu anaacha msichana.


Huyo msichana anakupenda ila ana msimamo wake, anataka kukupima akili yako kama unampango naye kwa future au ni part time tu. Hivyo wewe kama unampenda mwendee taratibu wala usikate tamaa, inabidi uonyeshe msimamo wako usiharakishe kula tunda.
 
Huyu msichana ameshastuka kwamba wewe nia yako ni kula tunda then umuuache. Kama ulivyosema alikuwa na ex-bf alikula tunda halafu akamuuacha, hivyo hiyo inamuuma sana kwa msichana mwenye msimamo.Hataki tena kurudia kosa, maana baadhi ya wanaume ndio zao anakuja na gia ya kuoa then akishapata kile kitu anaacha msichana.


Huyo msichana anakupenda ila ana msimamo wake, anataka kukupima akili yako kama unampango naye kwa future au ni part time tu. Hivyo wewe kama unampenda mwendee taratibu wala usikate tamaa, inabidi uonyeshe msimamo wako usiharakishe kula tunda.

"Yawezekana demu ana matatizo,wameshakula watu na kupita watu wengi hivyo imemkera sana, na anaona labda na wewe inaweza kuwa hivyo,ukamega na kupitia.Kingine nikuwa okay,vumilia lakini wanawake wa sasa hivi mambo yamebadilika sana,ku funga ndoa bila kutest tegemea mawili kuvunjika au kuwa ndoa njema,hivyo vitu lazima uvitegemee.Zamani wazazi wetu walikuwa wanatushauri mwananke wa kuoa kutoka familia fulani,kwasababu familia ile wanaifaamu kabisa ndani na nje,kama ina asiri ya born (inheritage diseases-magonjwa ya kuridhi) au la.Hivyo wanakupa ushauri kabla.Siku hizi tunaokotana mitahani kwahiyo tunabaki kubahatisha,ndio maana wanaume/wanawake wengi wanaitaji kuishi pamoja kabla ya ndoa,kudadisiana kuona walikotoka.Akina mama mara nyingi samahani wanakuwa na matatizo kadhaa ya kimwiri,mwingine hataki kufanya ngono kabla,make wao wanajijua matatizo yao niishie hapo mtajaza,mwingine akitembea na mwanaume tu, mwanaume huyo hawezi kurudi kwake tena, hapo mtajaza.Hivyo wengi akina dada wanataka mfunge ndoa ndo mle tunda kama liko bovu au safi mbelekwambele,na ndoa zinavunjika.Take care brother
 
kaka mimi nakushauri achana na huyo msichana atakuumiza sana sababu haoneshi mapenzi ya kweli,hajali feelingz zako kwa maana ya mapenzi uliyonayo kwake....kama x wake alimtenda kwa nini adhabu uipate wewe?....ni mtazamo wangu tu,uamuzi unao wewe
 
Mapenzi ya ughaibuni uongo mtupu!

Mdau usijikondeshe na hawa mademu wa kiafrika, wewe tafuta demu makaratasi ujiweke vizuri. Maisha mafupi kuhangaikia wanawake wasojua kupendwa.
 
aaah huyo msichana nae mshamba kwa nini asikwambie tu ukweli kuwa hana mpango wa kuwa na wewe kuliko ukae unaumiza kichwa kwa ajili yake
kwa mtazamo wangu mie kuna kitu kimemfanya asikupende tena kama ilivyokuwa mwanzo,ongea nae na akwambie then uanze maisha yako kwa amani kabisa akiendelea kuuchuna na wewe chuna
Kwani huwezi????
 
aaah huyo msichana nae mshamba kwa nini asikwambie tu ukweli kuwa hana mpango wa kuwa na wewe kuliko ukae unaumiza kichwa kwa ajili yake
kwa mtazamo wangu mie kuna kitu kimemfanya asikupende tena kama ilivyokuwa mwanzo,ongea nae na akwambie then uanze maisha yako kwa amani kabisa akiendelea kuuchuna na wewe chuna
Kwani huwezi????


alitegemea atatamkiwa neno ndoa, huyu binti nadhani alitegemea future na x wake kwa bahati mbaya akatendwa, anacheza kwa step sasa hv.
 
Dawa ya kuuchuna ni kumpotezea, tafuta kinanda hapo maeneo mnapoishi kula nacho good time kwa full kujiachia, kama ana nia nawe atajileta mwenyewe na kama hakupendi basi ataingia mitini moja kwa moja!
 
Kwa maoni yangu naona ni bora tu umuulize muhusika. Je, kulikoni mbona umepunguza mawasiliano yetu sana ukilinganisha na siku za nyuma? Mbona hatutoki tena kama zamani ambapo wote tulikuwa tunafurahi kuwa pamoja? Kama kuna chochote nilichofanya na kukuudhi ni kipi? Na hiyo ya kumuomba samahani naona ni vizuri kuendelea nayo labda anaweza akabadilisha mawazo yake lakini kwa maoni yangu hasa ukitilia maanani kwamba unampenda ni mapema mno kuachia ngazi kabla ya kusikia kauli yake mwenyewe kuhusu nini kilichomfanya abadilike na kama kuna chochote unachoweza kufanya ili arudie tabia yake ya zamani kabka ya kubadilika. Kila la heri.


Thans mkubwa nashukuru sana kwa mawazo yako ya maana.....Pia ni kweli nimejaribu kila njia kumuweka kadri ya uwezo lakini naona bado yupo vile vile sasa sifahamu nini kifanyike zaidi nitajaribu kuongea nae tena aniambie zaidi ila asante mkuu
 
Pole mwana ila hiyo mbona cyo issue kama vipi na we rudi nyuma kwanza huenda umeenda haraka sana,huenda cku ulipokubaliwa urafiki then next day ukaomba game hapo huenda ndo ulipokoroga.
Ila we c mtu mzima bana angalia kile unachoweza kufanya na ufanye kurejesha hilo pendo ukishindwa kurejesha replacement inakuhusu!


Mkubwa unajuwa sasa ni week ya 2 sasa najaribu kadri ya uwezo wangu na ujanja wote ila naona bado yupo vile vile so sielewi nini anahitaji ukimuuliza problem zaidi ni nini anasema hamna kitu nipo fine tu so nashindwa kabisa.....Alafu unajuwa jinsi ukiwa unajaribu kuongea na mtu alafu hana interest nadhani unajuwa inakuwaje, thanks mkubwa kwa mawazo
 
Huyu msichana ameshastuka kwamba wewe nia yako ni kula tunda then umuuache. Kama ulivyosema alikuwa na ex-bf alikula tunda halafu akamuuacha, hivyo hiyo inamuuma sana kwa msichana mwenye msimamo.Hataki tena kurudia kosa, maana baadhi ya wanaume ndio zao anakuja na gia ya kuoa then akishapata kile kitu anaacha msichana.


Huyo msichana anakupenda ila ana msimamo wake, anataka kukupima akili yako kama unampango naye kwa future au ni part time tu. Hivyo wewe kama unampenda mwendee taratibu wala usikate tamaa, inabidi uonyeshe msimamo wako usiharakishe kula tunda.


Thanks Pretty nadhani umemaliza kila kitu ni kweli hivyo ulivyosema hujakosea kabisa ni kweli msichana ana msimamo wa hali ya juu...Katika wasichana niliowaona nadhani huyu anajua nini anachokifa...ila nimekupata hapo vizuri sana ila nimemuonyesha msimamo kadri ya uwezo naona mwenzangu kawa kiziwa kabisa wala hajali kabisa anaona kama nampigia gitaa tu.....Labda inabidi nifikirie tena nini nifanye zaidi!
 
"Yawezekana demu ana matatizo,wameshakula watu na kupita watu wengi hivyo imemkera sana, na anaona labda na wewe inaweza kuwa hivyo,ukamega na kupitia.Kingine nikuwa okay,vumilia lakini wanawake wa sasa hivi mambo yamebadilika sana,ku funga ndoa bila kutest tegemea mawili kuvunjika au kuwa ndoa njema,hivyo vitu lazima uvitegemee.Zamani wazazi wetu walikuwa wanatushauri mwananke wa kuoa kutoka familia fulani,kwasababu familia ile wanaifaamu kabisa ndani na nje,kama ina asiri ya born (inheritage diseases-magonjwa ya kuridhi) au la.Hivyo wanakupa ushauri kabla.Siku hizi tunaokotana mitahani kwahiyo tunabaki kubahatisha,ndio maana wanaume/wanawake wengi wanaitaji kuishi pamoja kabla ya ndoa,kudadisiana kuona walikotoka.Akina mama mara nyingi samahani wanakuwa na matatizo kadhaa ya kimwiri,mwingine hataki kufanya ngono kabla,make wao wanajijua matatizo yao niishie hapo mtajaza,mwingine akitembea na mwanaume tu, mwanaume huyo hawezi kurudi kwake tena, hapo mtajaza.Hivyo wengi akina dada wanataka mfunge ndoa ndo mle tunda kama liko bovu au safi mbelekwambele,na ndoa zinavunjika.Take care brother


Asante sana mkubwa mimi nipo tayari kuvumilia wala sina problem kwanza maisha ya sasa ukimpata mwanamke mwenye msimamo ni raha sana,so nitajaribu kufight kadri ya uwezo ili kila kitu kiwe makini.....Then mkubwa kuowa bila kuonja tunda haiwezekana bana maana hiyo ndoa sijui itakuwaje...Thanks mkuu
 
kaka mimi nakushauri achana na huyo msichana atakuumiza sana sababu haoneshi mapenzi ya kweli,hajali feelingz zako kwa maana ya mapenzi uliyonayo kwake....kama x wake alimtenda kwa nini adhabu uipate wewe?....ni mtazamo wangu tu,uamuzi unao wewe


Point taken..Thanks mkuu ni kweli nadhani haoni feelin zangu maana hasira zake sasa naona amehamishia kwangu hataki kunielewa wala kunisikiliza..pia kitu kingine ni kwamba anajuwa nini anakifanya ndio maana.ila asante sana mkubwa nadhani inabidi nifkirie zaidi next step,Pamoja mkuu
 
Mapenzi ya ughaibuni uongo mtupu!

Mdau usijikondeshe na hawa mademu wa kiafrika, wewe tafuta demu makaratasi ujiweke vizuri. Maisha mafupi kuhangaikia wanawake wasojua kupendwa.



Thanks mkubwa me nina mda mrefu nilishajikita vizuri kimaisha,ila sema mademu wa kiafrica sijui wanakuwa vipi kwa kweli,pia mkuu point yako nimeipata vizuri sana na nitaifanyia kazi asante sana!
 
aaah huyo msichana nae mshamba kwa nini asikwambie tu ukweli kuwa hana mpango wa kuwa na wewe kuliko ukae unaumiza kichwa kwa ajili yake
kwa mtazamo wangu mie kuna kitu kimemfanya asikupende tena kama ilivyokuwa mwanzo,ongea nae na akwambie then uanze maisha yako kwa amani kabisa akiendelea kuuchuna na wewe chuna
Kwani huwezi????


Nadhani kuna baadhi ya marafiki zangu waliniambia hivi kwamba akiendelea kuuchuna na mimi niuchune,ila unajuwa napendaga sana mtu akiniambia problem yake then na mimi najuwa makosa yangu niliyofanya kuliko kukaa kimya unakuwa hujui nini kinaendelea,ila nashukuru sana kwa ushirikiano wako na majibu yako nitayafanyia kazi mpaka nipae solution.asante sana!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom