Papizo
JF-Expert Member
- Feb 24, 2008
- 4,944
- 1,431
Habari jamani...Nadhani hapa nitapata majibu mazuri na ya maana kuhusu hili swala.....Problem ni kwamba hapa nilipo nina demu wa kigambia ambaye nilikutana nae hapa ninapoishi,kukutana tulikokutana ni kwamba sio mimi nilimtongoza bali yeye alikuwa na interest na mimi toka mda mrefu sana ila alikuwa anashindwa kuniambia saa zingine tukikutana face to face huwa ananichekea na kuniuliza maswali tofauti ila nilikuwa sijajua zaidi sasa ikafikia kipindi akamuuliza rafiki yangu kuhusu mimi tabia yangu na nipoje....sasa siku nipo break baada ya kazi akanikuta nimekaa mahali akaanza kuniuliza wapi nimetokea I mean nchi gani vitu kama hivyo....Mimi sikumchelewesha pale pale kwa sababu nilishajua nini anataka nikaweka mambo sawa usiku wa hiyo siku nikawasiliana nae kwenye simu nikaongea nae sana na tukafahamiana zaidi na mapenzi yetu yakaanza hapo,Sasa kitu ambacho nashindwa kuelewa ni kwamba amebadilika ghafla na tulikuwa tunakwenda out tunafurahi pamoja lakini sasa hivi hataki tena nikimuomba tuonane analeta mambo mengi bora tusionane ...Na alivyokuwa na problem mimi nilikuwa mwepesi sana kumsaidia pamoja alikuwa haniombi hela pia yeye bado yupo university na anafanya kazi part-time.Sasa katika mazungumzo yangu nimewahi kumgusia kama mara 3 kuhusu mambo fulani nadhani hapo mmeelewa vizuri....Sasa sikujua kabisa yeye huwa hapendi hayo mambo na nikajiuliza je mapenzi ni nini?Nikashangaa sana sasa akaja kumwambia rafiki yangu kwamba eti mapenzi sio pesa wakati huwa namsaidia muda mwingine hata hela ya bus pass ya kwendea shule au kununulia bidhaa ndogo ndogo huwa anakosa inabidi nitoe nimpe,pia yeye anasema kwamba hatopenda kufanya hicho kitendo kutokana na ex-bf wake alivyomfanya maana alimkamua then akaingia mitini so hatoamini tena wanaume,ila hicho kitendo hajakataa kufanya atafanya lakini mpaka atakapo niona msimamo wangu upo vipi, alianza kunibadilikia simu akawa hapigi tena,messeg hatumi tena na mawasiliano kapunguza kabisa ila sikujua zaidi problem ni nini mpaka baada ya kusikia kwa rafiki yangu ndio nikajua..Pia nilivyomuona yupo vile nilimuuliza whats wrong lakini akasema ohh hamna kitu.Sasa mimi nikamuomba msamaha kwa sababu kwanza nampenda na ametulia sana nikawambia kwamba nipo tayari kuwa na wewe bila hicho kitendo ila naona mwenzangu bado kama hahitaji mawasiliano na mimi na hata nikimtumia messeg hata 15 kwa siku basi atajibu 2 au 1 na ukiangalia hapo anasimu ya contract sasa wadau mnanishauri vipi??Niachie ngazi pamoja nitaumia au nimshaurije mwenzangu aweze kurudi katika hali ya kawaida kama zamani?Maana najaribu kuwa karibu nae sana tena sana lakini naona mwenzangu hana interest...Sasa wadau mnanishauri nifanye nini??
N.B nahitaji ushauri please sio utani ndugu zangu!
N.B nahitaji ushauri please sio utani ndugu zangu!