MAKOLE
JF-Expert Member
- Feb 5, 2012
- 618
- 280
Wapendwa, niling'oa jino siku ya ramadhani 3, hadi leo ramadhani 23 kidonda kinanisumbua. nilitumia dozi ya cloxaciline na flagile kwa siku 5 nikarudia siku 5 nyingine baada ya siku 4. Kidonda kinaelekea kufunga lakini kuna maumivu yapo constant, hayapungui wala hayazidi lakini kila nikiingiza pamba natoa usaha uliochanganyika na damu. nna hakika hakuna kipande ndani kwani nikiangalia jino lenyewe ambalo ni namba 18 limetoka lote ila shimo ndio lilikuwa kubwa kwani mizizi ilienda chini sana. Je hii ni hali ya kawaida? Nifanyeje ili kidonda kifunge kabisa? Nawaomba sana mniokoe mwenzenu naumia sana! jino lenyewe katika picha ya hapa chini linafanana na hilo namba 18