Msaada wa Anti-vir

Gurta

JF-Expert Member
Sep 17, 2010
2,234
531
Nilikuwa na avast 5 kwenye lappy yangu, nikai-uninstall na kuweka Avira premium. Sasa nikienda kwenye registry nakuta values za avast na kila nikijaribu kuziondoa inanikataza as if zipo kwenye running program.

Nikaona isiwe tabu, nikang'oa ile Avira na kutaka kuweka tena avast 6, kinachotokea ni kwamba hai-install kabisa. Inaonesha ina-extract files prepping for installation then nothing happens.

Nimeharibu wapi?
 
Kiongozi Antivirus nyingine michosho tu, tafuta KASPERSKY au AVG hizo ndizo za ukweli ndugu yangu ni PM nikutumie KAV 2011
 
mkuu ulichofanya ni kuwa, wakati laptop yako ilipokuwa na avast 5, inaonyesha ili fanya scanning ya virus basi baada ya kumaliza ikakamata labda kirusi au spyware . na kawaida ya anti-virus zote ni kuwa zinachukua lile faili lililoharibika kwa kirusi na kulibadilisha kwa kulipa jina lingine wanati huo huo kulifanya liwe linaweza kutumiaka( hii ni kwa system files tu) ndio kusema badala ya kuwekwa kwenye program files, huwa zinahifadhiwa kwenye anti-virus husika ili kufanya system isiweze ku crush(system hault).hivyo uliweza kuendelea kutumia laptop yako kama kawaida.baada ya wewe kuamua kuitoa hiyo anti-virus yako,ukawa umeondoa hadi hilo faili muhimu kwa ajili ya kuendesha system ya computer yako,na jinsi ulivyofuta, huku futa kwenye uninstall or change a program, kwa maana nyingine umefuta baadhi ya faili tu,au imekulazimisha kufuta faili hizo tu, sasa kila ukitaka ku unstall yote ,inakataa, kila unapotaka kuweka avast 5 mpya inakataa kwasababu kawaida inahitajika kwanza ufute kila kitu kinachohusu antivirus husika ili uweze kuweka upya,kumbuka, ukifuta kila kitu, huenda computer ika CRUSH..!! na pia ,kuweka antivirus mbili kwenye computer moja itafanya ugomvi pia,kwani kila mmoja anafikiria kuwa mwenzake ni kirusi!!!!kuwa muangalifu,ingekuwa rahisi kwako, ningekushauri kuweka new operating system,na uchague anti-virus nyingine,kama alivyosema mkuu hapo juu, pia ningekushauri kutumia AVG,kwani ni ndogo lakini inaweza kuhimili mikiki ya virus sana tu, unachotakiwa ni ku update mara kwa mara.
nategemea umepata jibu sawia.
 
Mkuu Muhsein ameeleza yote na mimi kwa kuongezea ni kwamba kama unafanya un-installation ya program kama hizo za Anti-Virus inabidi pia ufanye search kwenye HDD kwa ku-type jina au herufi ambayo inaanzia na neno kama Avast na hata kwenye HDD yenyewe utafute folder yoyote ambayo imehifadhi files za Avast.

Baada ya kuzipata files zote hizo uhakikishe unazifuta kwa kubonyeza kitufe cha Delete na pia kwenye pipa la Recycle ambalo litakuwa limehifadhi files hizo.

Yaani pasiwepo Anti-Virus ingine kwenye laptop yako wakti ukitaka ku-install program ingine endapo unahitaji kubadili.

Halafu siku za hivi karibuni microsoft wametoa program yao maalum iitwayo microsoft security essentials ambayo inasaidia kulinda komputer dhidi adhari kama za Malware na virus zingine na piqa kutoa "real-time scanning" wakti ukiwa online.

Kwahio enenda kwenye website ya microsoft kupitia link ifuatayo na ujaribu program hio ya bure.

http://www.microsoft.com/security_essentials/?WT.mc_id=MSCOM_HP_US_F_113LMUS004198
 
Kiongozi Antivirus nyingine michosho tu, tafuta KASPERSKY au AVG hizo ndizo za ukweli ndugu yangu ni PM nikutumie KAV 2011

Mkuu nilikuwa nayo hiyo KWENYE PC moja miezi miwili tu nimetupa jalalani Oops ipo kwenye kabrasha ni bomu kama una uwezo tumia Norton ni nzuri wakati mzuri wa kununua kama upo Ulaya ni Dec baada ya X-mass hadi Jan 15 kwa sababu inakuwa half prize about £20.00 na ni kwa mwaka ukichelewa hapo jiandae kulipa £50 - 60. UTAKUWA NA AMANI.

Kama unahitaji Kaspersky ni pm nitakupatia free.
 
Nilikuwa na avast 5 kwenye lappy yangu, nikai-uninstall na kuweka Avira premium. Sasa nikienda kwenye registry nakuta values za avast na kila nikijaribu kuziondoa inanikataza as if zipo kwenye running program.

Nikaona isiwe tabu, nikang'oa ile Avira na kutaka kuweka tena avast 6, kinachotokea ni kwamba hai-install kabisa. Inaonesha ina-extract files prepping for installation then nothing happens.

Nimeharibu wapi?
8hYjzUieOQcAAAAASUVORK5CYII=

Avast_AntiVirus_5_1_861_With_License
 
NODE 32 ndiyo mwisho wa matatizo na hizi nyingine zinaiga tu. Tumia Nod 32 na Windows FireWall yako hakikisha iko up-to-date hiyo itakusaidia sana.
 
Nilikuwa na avast 5 kwenye lappy yangu, nikai-uninstall na kuweka Avira premium. Sasa nikienda kwenye registry nakuta values za avast na kila nikijaribu kuziondoa inanikataza as if zipo kwenye running program.

Nikaona isiwe tabu, nikang'oa ile Avira na kutaka kuweka tena avast 6, kinachotokea ni kwamba hai-install kabisa. Inaonesha ina-extract files prepping for installation then nothing happens.

Nimeharibu wapi?

kwa matatizo yako nakushauri tumia hizi program 2 kuondowa hayo mafaili yaliyobaki kwenye hiyo registry na unaweza Ku download tena Bonyeza hapa Download Revo Uninstaller Freeware - Free and Full Download - Uninstall software, remove programs, solve uninstall problems na hii bonyeza hapa CCleaner - Free software downloads and software reviews - CNET Download.com
 
kwa matatizo yako nakushauri tumia hizi program 2 kuondowa hayo mafaili yaliyobaki kwenye hiyo registry na unaweza Ku download tena Bonyeza hapa Download Revo Uninstaller Freeware - Free and Full Download - Uninstall software, remove programs, solve uninstall problems na hii bonyeza hapa CCleaner - Free software downloads and software reviews - CNET Download.com

Asante mkuu ila hizi zote ninazo na ninazitumia a infact nilitumia Revo wakati wa kufanya uistallation ya ile avast 5

Kuhusu CCleaner, nimeitumia kwa muda tangu ikiwa v2 hadi v3 lakii nachelea kusema inazidiwa uwezo na kitu inaitwa Glary Utilities, zuri sana hii.

By the way thanks
 
revo uninstaller haishindwi ki2 kwa sababu ina huwezo wakuscan registry values zinazokua zimebaki if failled uki2mia kwenye safemod itakubali kwa sabaBU antivirus nying hazi2miki kwenye safe mode......ukishindwa kupata left over we install tena avast ukimaliza 2mia revo uninstaller kuichomoa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom