Habari zenu wana jamvi .Naombeni msaada nimuokoe mdogo wangu ni mwaka wa pili sasa anateseka. Alianza kwa kusema anaona wadudu wanatoka ukeni..Nikaogopa nkampeleka kwa dactari wa magonjwa ya zinaa akapewa dozi ya mwezi mzima kumbe wadudu ulikuwa ni ute mzito wa njano. Baada ya dozi ile akapata mafuu ute ukawa hautoki. Baada ya mwezi hali ikarudia kwa kasi nkampeleka tena hospital kapewa dozi nyingine ya mwezi akapata nafuu lakini ikarudia tena. Akarudi tena hosptl kachomwa sindano za mshipa tano ndo kwany tatizo linaendelea. Then tukampeleka kwa specialist wa wamama. Akasema ni bacteria akamfanyia culture na kumpa vidonge dozi ya mwezi lakini dozi ilipokwisha tu hali ikarudi kama mwanzo. Kadumbukiza kila vidonge ukeni mpaka anatia huruma dalili za kupona hakuna. Naombeni msaada apone kama ni adhabu inamtosha