Msaada tafadhali

Plato

JF-Expert Member
Aug 28, 2010
420
94
Ndugu,poleni na majukumu.mimi ni mwanafunzi wa UDSM-DUCE.niko mwaka wa tatu ambao ni wa mwisho.nakusudia kumaliza july.

Nasoma Public Administration na ualimu, somo la historia. Ni muhitaji na hulipiwa na bodi ya mikopo. Kuna tatizo kubwa limetokea, sikusaini fomu muhula uliopita na bodi waliasume sipo chuo, hivyo kuniondoa kwenye orodha ya mkopo. Nimefatilia suala hili,lakini uamuzi wa bodi umekuwa niombe upya kwa ajili ya mwaka kesho.

Nakabiliwa na hatari ya kutoona matokeo ya muhula uliopita na kukosa udahili muhula huu.ninapaswa kulipa ada ya mwaka wa mwisho ni nyingi sana. MILIONI MOJA.

Ninatafuta msaada wa mkopo wa fedha hizo. Nikimaliza chuo July naweza kulipa, ama kufanya kazi ili kulipa deni.kwa wenye shule naweza kufanya kazi kulipa deni.naweza kufundisha vizuri historia, GS, na DIVINITY. Nimesoma seminari na kusoma falsafa na teolojia, na nimewahi kufundisha masomo hayo.

Chaguo jingine kwangu ni kuandika barua ya kuahirisha mwaka kurudi nyumbani na kuomba tena mkopo nikipata nirejee kumalizia masomo. Baada ya kukwama kabisa, kabla ya kuandika barua ya kuahirisha mwaka nimeona niwaeleze kuomba ushauri na msaada.

Nitashukuru kwa kila jambo na Mungu atuweke salama, asanteni
 
waoh,
Naona unaoffer terms nzuri, take your proposal to some secondary schools mnaweza kusign deal katika terms za mshahara and long term plan issues. walimu ni issue kubwa sana nchini.

Na kama utafanikiwa please come back and share with us, sababu hiyo inaweza ikawa imefungua opportunity kwa vijana wengine.

all the best
 
Daah!
Pole ndugu yangu.
Kuhairisha mwaka nayo kazi.
Natumai atapatikana wa kuokoa jahazi.
 
Aisee,pole sana mkuu
Hapa nimejifunza sana,kumbe huwa tunaitwa ku-sign tunajivuta ishu ni serious kiasi hiki?

Ombi tu kwa moderators wasiitoe thread hii hapa maana ndipo kuna viewers wengi na wataweza kumsadia,kuipeleka kwingine kutachelewesha mambo!
 
Nimekwisha kwenda katika shule nyingi hapa dar.wamelitazama zaidi kutokea upande wao kuhitaji walimu,na wamesikitika hawawezi kunisaidia.asante
 
Aisee! Pole sana ndugu yangu.

Bodi ya mikopo ni mali ya serikali na Chuo ni mali ya serikali; kwa vile Chuo kinakutambua kama mwanachuo halali si dhani kama kuna utata, ione management, ikiwezekana uruhusiwe ufanye paper kwa mkopo; alafu baada ya hapo ndo unaweza kuingia mitaani kusaka kibarua ili uweze ku-clear hiyo ada.

Kwakweli kuhairisha mwaka eti umalizie mwaka kesho binafsi naona utakuwa umepoteza muda mwingi sana.
 
Itisha kikao kama vile vya harusi. Tujulishe. Tutafika kuja kukuchangia. Usiwasahau ndugu na jamaa zako ambao hatimaye watanufaika zaidi nawe.
 
Kabla ya kufanya chochote nimeanza na management ya chuo.kuja hapa ni namna ya mwisho kwangu kujiridhisha kuwa nimekosa namna yoyote.asante
 
Siku tatu zilizopita,nilipost thread hapa kuomba msaada.nimepata shida ambayo yaweza gharimu kuahirisha chuo au kuahirisha mwaka.natafuta mkopo wa mil.moja nimalizie masomo kisha nitalipa au fedha,au kufanya kazi.nasoma public administration na ualimu na napaswa kumaliza mwezi wa saba.
Naelewa jukwaa hili hutembelewa na watu wengi,lakini kwa siku tatu ni watu 2 pekee wamenipa ushauri.na kupitia post hii.ila issue ya prof.safari tayari imechangiwa na watu mia nne.tafadhali naomba msaada wenu kama si wa mali basi wa hali.asante kwa wote walionipa ushauri.
 
Siku tatu zilizopita,nilipost thread hapa kuomba msaada.nimepata shida ambayo yaweza gharimu kuahirisha chuo au kuahirisha mwaka.natafuta mkopo wa mil.moja nimalizie masomo kisha nitalipa au fedha,au kufanya kazi.nasoma public administration na ualimu na napaswa kumaliza mwezi wa saba.
Naelewa jukwaa hili hutembelewa na watu wengi,lakini kwa siku tatu ni watu 2 pekee wamenipa ushauri.na kupitia post hii.ila issue ya prof.safari tayari imechangiwa na watu mia nne.tafadhali naomba msaada wenu kama si wa mali basi wa hali.asante kwa wote walionipa ushauri.

Pole sana ndugu yangu,hapa JF inaonekana we mgeni wa kupost kama mimi.Lakini mimi nilikuwa msomaji wa wengine tu hadi nilipoamua kujinga. Ukitaka post isomwe na kuchangiwa labda ihusu chadema na kuwaponda waislam. Ushauri wangu kwako best ni uende Bayport financial services lakini hawa ni wezi wakubwa.Lakini ni bora uumie miaka ijayo kwa kukatwa mshahara kwa miaka5 lakin umalize masomo.Kila la kheri best.
 
Du!Pole sana mkuu. Habari yako imenifanya nijisikie kulia. Kuahirisha mwaka kwa kukosa 1M inasikitisha. Wakuu naomba tumsaidie huyu raia maana mpaka kuja kuweka hii habari hapa kweli hali ni mbaya. Tufanye kama ni kamchango ka harusi maana tunachangia nyingi na wala hatuhudhurii. Kwa vile swala lako ni nyeti weka namba yako ya simu na e mail address kwenye hii thread, usiogope. Kwa kuanza nitakusaidia USD 100 (mia moja). Tafadhali ni pm.
 
[QUOTE=Plato;1809760]Namba yangu ya cm ni 0782927100.[/QUOTE]


Ok.Iwe kwenye topic pale juu ili iwe rahisi kuonekana. Ni pm unipe jina lako or e mail.
 
Natumia cm na sijui namna ya ku pm siioni hiyo option hapa kwenye reply to topic.pia kuweka namba juu labda moderator au nipost upya.asante
 
Ok.kama unatumia simu nahisi inaweza kuwa ngumu.Ingekuwa ni computer ni simple maana ungeenda kwenye topic then edit.Pia button ya PM ungeiona.Nitakutafuta
 
rudi juu kabisa ya ukurasa wa wavuti, kuna sehemu imeandikwa user cp, bofya hapo, utaona vitufe vingi kikiwemo cha praiveti meseji. Kuhusu kuweka namba bofya kitufe cha edit chini ya postiyo. Bak to topic, pole sana kaka mkubwa, nadhani utashinda tu hilo kwazo. Bt next tym ni vema kuheshimu mamlaka, wanavyosema uje kusaini ada, they mean it. Pole sana kaka, tuko pamoja!
 
Back
Top Bottom