Baba Sharon
JF-Expert Member
- Oct 22, 2010
- 373
- 248
Tafadhali naomba mwenye ujuzi au uelewa wa hili anisaidie.........Mwanangu amekuwa na tatizo la kuanguka na kupoteza fahamu na limekuwa na tarehe maalum ni kati ya tarehe 15 na 27 au 26 na 28 ya kila mwezi.
Kwa mfano tatizo hili lilimuanza terehe 27 ya mwezi wa Saba mwaka huu na limekuwa likiendelea hivyo mpaka jana alipoanguka tena. Mwezi wa nane alianguka mara mbili yani tarehe 16 na 28 mwezi huu hivyo hivyo. Sasa nashindwa kuelewa tatizo ni nini.......
Alipelekwa hospitali baada ya kuanguka na alipimwa daktari akasema hana kitu chochote kinachomsumbua akampatia dawa za maumivu akarudishwa nyumbani.......
Mwezi wa nane alipoanguka akapelekwa tena akaambiwa kuna uwezekano wa mtoto kuwa na degedege akapatiwa vidonge lakini cha kushangaza jana tena kaanguka na vidonge alitumia.
Tafadhali naombeni msaada wenu kama kuna yeyote mwanae aliyekumbana na tatizo hili au hata la degedege.......Kwa kweli sina uzoefu mkubwa wa kulea watoto maana huyu ndiye wa kwanza.
Na daktari anasema hili tatizo likiendelea litamletea mtoto kifafa naomba Mungu aipushie mbali hili.........
Kuna nurse mmoja aliniambia labda kuna mtu alimwangalia mtoto na jicho baya sasa nachanganyikiwa maana uhusiano wa kuangaliwa mtoto vibaya na kuanguka kwake upo wapi na kuna ukweli wowote kuhusu hili?
Kwa mfano tatizo hili lilimuanza terehe 27 ya mwezi wa Saba mwaka huu na limekuwa likiendelea hivyo mpaka jana alipoanguka tena. Mwezi wa nane alianguka mara mbili yani tarehe 16 na 28 mwezi huu hivyo hivyo. Sasa nashindwa kuelewa tatizo ni nini.......
Alipelekwa hospitali baada ya kuanguka na alipimwa daktari akasema hana kitu chochote kinachomsumbua akampatia dawa za maumivu akarudishwa nyumbani.......
Mwezi wa nane alipoanguka akapelekwa tena akaambiwa kuna uwezekano wa mtoto kuwa na degedege akapatiwa vidonge lakini cha kushangaza jana tena kaanguka na vidonge alitumia.
Tafadhali naombeni msaada wenu kama kuna yeyote mwanae aliyekumbana na tatizo hili au hata la degedege.......Kwa kweli sina uzoefu mkubwa wa kulea watoto maana huyu ndiye wa kwanza.
Na daktari anasema hili tatizo likiendelea litamletea mtoto kifafa naomba Mungu aipushie mbali hili.........
Kuna nurse mmoja aliniambia labda kuna mtu alimwangalia mtoto na jicho baya sasa nachanganyikiwa maana uhusiano wa kuangaliwa mtoto vibaya na kuanguka kwake upo wapi na kuna ukweli wowote kuhusu hili?