Msaada Tafadhali, Hali mbaya-ofisi chungu!

You are right. Sehemu ya health and safety is psychosocial issues. Kuna subtopic ya personal issues zinapoingilia kazi. Ila asikudanganye kumuambia mtu one on one ni ngumu sana. Ana dada zake na kaka zake na wachumba pia! Hao wangetosha kum'badilisha. Na hao coaligues wa zamani woote hakuna wa kumuambia hadi ukaseme wewe? Uzuri wa pua inaadapt to mazingira haraka. Jidunge uturi wa maana, achana nae bana!
Is this really an HR matter? zaidi naweza kusema ni Health and Safety...
 
Duh! Distance urself! Aisee kuna mtu ananuka hadi ukikaa nae tumbo lako linajaa gesi! I can imagine! Tafuta airy space ofisini, walau karibu na mlango! Chewing a gum might help, ila kama hakuna njia mi ningesaka kazi nyingine kabisa! Hebu fanya arrangement ya Health and Safety umuite Mwali amdadavulie hii.

Kuna wanakua na kucha ndefu afu chafu. Really stuffed and oki-packed! Afu mkienda lunch anakula na mkono! Grrrhhh! Unatamani umpakue kwa kisu!
Nimepatikana si kidogo aisee, jamaa hana hata wasiwasi, kanunua laptop kaomba awe anakaa pembeni yangu nimfundishe autocad software!
 
Last edited by a moderator:
Huenda ana tatizo la "anal discharge"au fecal incontinence -i.e his anal sphincter is leaky. deodorant au perfume etc hazitasaidia na badala yake zitaongezea hiyo harufu kuwa mbaya zaidi. Air freshner ni suluhisho la muda mfupi na ni ghali kiafya na kipesa kama utatumia kila siku. Hilo tatizo linatibika. Hakuna njia rahisi ya kumwambia mtu kwamba ana tatizo kama hilo na hasa ikiwa mwenyewe hajitambui na uliowakuta hawajawahi kumwambia kitu kama hicho. Je, hapo kuna wafanyakazi wengine wanaokerwa na harufu hiyo zaidi ya wewe? Kama ni wewe tu ndiye unakerwa na harufu hiyo basi mkuu wangu inabidi utafute njia nyingine ya kuivumilia.
 
Mkuu,
Mwambie ukweli tu. Kwa sababu ukikaa kimya wakati unateseka Unakuwa haujitendei Haki. Inawezekana kabisa yeye muhusika hajui Kama ana tatizo hilo.

Kuna jamaa mmoja ninafanya nae kazi, yeye amezoea kuchokonoa pua lake halafu huwa anaangalia kile kinachotoka puani. Yaani huwa anajisahau kabisa akiwa busy kuchokonoa pua lake. Mbaya zaidi anapenda sana kushika watu mikono na kuonja vyakula vya watu bila ridhaa...utamsikia anasifia hawa kuku wa leo wanaonekana kabambe..ukishtuka keshachukua paja la kuku. Niliamua kumtolea uvivu siku yake ilipofikia kwangu. Nikamweleza ukweli kiutu uzima na tunaheshimiana mpaka leo.

Suluhisho ni kumuweka wazi.
 
Duh... Pole sana
Nimewaza kuna mtu niliwahi kukaa nae kama dk kumi tu ile harufu yani kifua chote kilibana na tumbo linacheza. mtihani huo
Nadhani ungejaribu kuuliza kwanza huenda wengine walishajaribu kumwambia ndio anawaepuka anaona bora kuwa karibu na wewe kwa kua anaona hujali kuhusu harufu yake au anaona wale walimwambia kwa chuki.
 
Jamani natumaini mko salama kabisa na wale waungwana waliofunga kwa dhati basi rehema za mwenyezi Mungu ziwatangulie na toba zao zisikike. ndugu yenu nina tatizo moja na linakuwa serious kila muda unavyozidi kwenda. Nimeanza kazi mahali sina muda mrefu sana kuna bwana mmoja subordinate kwa level kama 2 chini ananuka sana wakuu, ninashindwa kumwambia na hata wenzake hawamwambii.

Siku hizi ameanzisha mchezo wa kupenda kujifunza kazi sasa muda wote anataka awe pembeni yangu! Ninapata shida hasa, mwanzoni nilidhani alijisahau akajisaidia ndani ya nguo ila naona ni kila siku na hali inazidi kuwa mbaya. Nguo zake kwa nje sio chafu sana ajabu!

Nashindwa kumwambia maana kwanza ni mgeni mimi kisha ni mtu mzima kanizidi umri na mwenye familia yake huko street. Ninahisi nikimwambia atajisikia vibaya sana na atachukia kazi. Anapenda mno kuendesha gari inapotokea kazi ya nje anakimbilia funguo sasa humo ndani ya gari na vioo vimefungwa kwa kuwasha AC ni balaa, mazingira ya kazi ni muhimu kufunga vioo vya gari kila mara, hadi ninahisi nikishuka kwenye gari ninakuwa na mimi nimeambukizwa harufu!

Nifanye nini wakuu?
Tafuta mtu mwaminifu ambaye unamfahamu halafu yeye hamfahamu, mtumie "a very descent message" kwenye simu yake , (ukimtaja jina, asije akachukulia meseji hiyo kuwa ni junk) kumweleza tatizo hilo, uwe wazi ukimwambia kuwa watu wanaogopa kumweleza sababu huwa ni vigumu kumweleza mtu pindi anapokuwa na tatizo hilo. Mwambie pia kuwa wewe ni mtu unamfahamu isipokuwa umeogopa kumwambia kwa mdomo na hivyo umeamua kutuma message kwa kutumia simu ya mtu mwingine! Asipokuelewa kwa njia hii basi atakuwa ana matatizo, na itakuwa ni halali kwake kuendelea kuwa katika hali hiyo na si bahati mbaya tena. Wala hawezi kufuatilia namba iliyomtumia meseji kama ni mwelewa!
Ukishindwa hivyo mtumie email kwa njia ya computer. Muhimi ni lazima umtaje jian ili aaweze kujua kuwa mlengwa ni yeye!
Watu wa namna hii pamoja na wanaonuka midomo kwa kweli ni shida sana, hata mimi ninao ila nilishashindwa kuwaambia, ila nahisi siku moja itabidi nifanye hivyo!
 
Nashukuru sana wakuu kwa michango yenu yoooote, hapa ninapoandika hivi yuko pembeni yangu!. Ni mtu anajituma na anawahi kazini kuliko wote. Nilijaribu leo nilipoingia ofisini tu alikuwa peke yake (Kawahi ofisini kwangu na kaingia kakaa kawasha laptop yake!) nikamuuliza 'unasikia kama kuna harufu isiyo ya kawaida hapa'? akadai hasikiii kitu basi nikawa mpole tu.
Nimefikiria nimtume mshkaji fulani immediate boss wake ila hawako close kabisa!
 
unajua mkuu kabla ya kumfesi kwanza unamsoma,unajua ni mtu wa aina gani,na huu ndio uongozi.kwanza lazima ujue je ni wote wanasikia harufu hiyo au ni wewe peke yako?kama ni wewe peke yako bas tatizo linaanzia kwako au?na yawezekana hawa wengine walisha zoea harufu ile kiasi kwamba hawaoni kama ni tatizo.kwa hiyo ukifanya reseach hayo yote then unamwambia tu,lakn unakuwa tayari kukabilia na result,anaweza kukuchukia,anaweza kukupenda,anaweza kuomba ushauli kwako pia

Kutokana na ugeni wangu nachelea kuuliza uliza watu kwa vitu personal kwa miezi hii michache mkuu, najua ni lazima wanasikia na pengine ndio maana hawako nae karibu mara kwa mara, ninamsubiri jamaa fulani ambae aliwahi kuwa boss wao zamani kabla hajabadilishwa kitengo nimuulize, yuko likizo kwa sasa.
 
Nashukuru sana wakuu kwa michango yenu yoooote, hapa ninapoandika hivi yuko pembeni yangu!. Ni mtu anajituma na anawahi kazini kuliko wote. Nilijaribu leo nilipoingia ofisini tu alikuwa peke yake (Kawahi ofisini kwangu na kaingia kakaa kawasha laptop yake!) nikamuuliza 'unasikia kama kuna harufu isiyo ya kawaida hapa'? akadai hasikiii kitu basi nikawa mpole tu.
Nimefikiria nimtume mshkaji fulani immediate boss wake ila hawako close kabisa!

NiPM no yake na jina lake, mimi nimwambie kwa simu.
 
jaribu kuongeza ukaribu naye ili yeye awe free kwako nawe free kwake hapo ndio itakuwa rahisi kumchomekea mada hiyo kwani km ndio kwanza umeanza kazi mahali hapo halafu ukaanzisha mada hiyo kwake hatakuelewa atakuona km mwanga tu...muhimu fanya ukaribu naye huku ukiwa na subira, akiwa huru kuzozazoza nawewe nawe ikishakuwa hivyo kwake then mwaga sumu!!!pole sana!
 
huyo jamaa si anapitiaga JF mmmmhhh haya

sio vizuri kumsema mwenzako hivyo hata kama hujamtaja kwa jina ni heri ungemwambia ukweli akakuchukia kuliko unaumia huku unamsema kwa watu
 
Umesema wewe ndio mgeni sehemu hiyo, vipi umejaribu kujua kama watu wengine (wenyeji) nao wana mtizamo kama wa kwako juu ya harufu ya huyo jamaa? Maana kama ni wewe mgeni tu ndio unaona hilo tatizo, inaweza kuwa vigumu sana kumu-approach bila kuzua songombingo. Huyo jamaa unayesema anatokea kwenye tamaduni za namna gani? - hii inaweza kukusaidia kujua sababu ya harufu hiyo au hata namna ya kum-approach. (kwa mfano kama umewahi kukaribiana na wamasai au wamang'ati - ukiacha hawa wa mijini humu- , unaweza kujua ni kwa nini nalisema hili tamaduni).

Ni vema pia wewe binafsi ukaji-assess pia kama huna kitu kinachowakera watu lakini wanakuvumilia tu ("toa boriti, kabla ya kuwaambia wengine wana 'kibanzi'").
 
Is this really an HR matter? zaidi naweza kusema ni Health and Safety...

Niliwahi kufanya kwenye department fulani, na siku ya kwanza kazini nilipewa document za maelezo ya kazi, kwa juu kabisa kulikuwa na document kama 2 pages hivi inaelekeza mambo muhimu ya kuzingatia, and I can tell you 'Personal Hygene' ilikuwa number moja! Manager alikuwa mwanamke but the rest of the team members walikuwa wanaume. Office ilikuwa super clean, na hata mtu ukija umejipulizia perfume mshenzi (perfume zenye harufu mbaya) manager anakuambia on the spot.

Tanzania bado tuna mambo ambayo tunaona ugumu kuambiziana lakini yanaleta karaha. Mfano ni hili la personal hygene, lakini pia kuna wanawake wana-ndevu na wanaziacha kama wanaume! (horror!) Then kuna wengine (wanawake) wana minywele miguuni, haya yote ni mambo watu wanatakiwa wafundishwe wakiwa kwenye adolscence stage. Yote tisa, watu wazima, wabunge included, wanasafisha mipua yao hadharani (sick).
 
Sijawahi, maana sikuwa na tatizo hilo

Ziko compatible, tatizo zinaplot sehemu isiyo yenyewe.
Nahitaji kujua kama kuna jinsi ya kufanya transformation.

Imagine Ziwa Nyasa limeplot Tabora? Au natakiwa kukazania kinyamwezi? :)
They are not compatible my dear. Ngoja aje mwenyewe atuthibitishie. Hivi uliwahi kufungua .cad extension in earlier versions?
 
Sijawahi, maana sikuwa na tatizo hilo

Ziko compatible, tatizo zinaplot sehemu isiyo yenyewe.
Nahitaji kujua kama kuna jinsi ya kufanya transformation.

Imagine Ziwa Nyasa limeplot Tabora? Au natakiwa kukazania kinyamwezi? :)
Coordinate unaandika kwa format gani in GIS na format gani in autocad? Labda jibu liko hapo? Unatumia excel?
I think it is easier to do the job in autocad and make a map in GIS but not the other way round as GIS is poorer
 
ahahahahahhaaaaaa heheheheheeeeeeee uwiiiiiiiiiii lol nimecheka sana japo kwako ni shida aaah ila nimecheka sana hasa kukufuata as personal help umfundishe kazi lol pole ila mie kwangu burudani
 
Back
Top Bottom