Sokwe Mjanja
JF-Expert Member
- Jul 16, 2009
- 576
- 297
Jamani natumaini mko salama kabisa na wale waungwana waliofunga kwa dhati basi rehema za mwenyezi Mungu ziwatangulie na toba zao zisikike. ndugu yenu nina tatizo moja na linakuwa serious kila muda unavyozidi kwenda. Nimeanza kazi mahali sina muda mrefu sana kuna bwana mmoja subordinate kwa level kama 2 chini ananuka sana wakuu, ninashindwa kumwambia na hata wenzake hawamwambii.
Siku hizi ameanzisha mchezo wa kupenda kujifunza kazi sasa muda wote anataka awe pembeni yangu! Ninapata shida hasa, mwanzoni nilidhani alijisahau akajisaidia ndani ya nguo ila naona ni kila siku na hali inazidi kuwa mbaya. Nguo zake kwa nje sio chafu sana ajabu!
Nashindwa kumwambia maana kwanza ni mgeni mimi kisha ni mtu mzima kanizidi umri na mwenye familia yake huko street. Ninahisi nikimwambia atajisikia vibaya sana na atachukia kazi. Anapenda mno kuendesha gari inapotokea kazi ya nje anakimbilia funguo sasa humo ndani ya gari na vioo vimefungwa kwa kuwasha AC ni balaa, mazingira ya kazi ni muhimu kufunga vioo vya gari kila mara, hadi ninahisi nikishuka kwenye gari ninakuwa na mimi nimeambukizwa harufu!
Nifanye nini wakuu?
Siku hizi ameanzisha mchezo wa kupenda kujifunza kazi sasa muda wote anataka awe pembeni yangu! Ninapata shida hasa, mwanzoni nilidhani alijisahau akajisaidia ndani ya nguo ila naona ni kila siku na hali inazidi kuwa mbaya. Nguo zake kwa nje sio chafu sana ajabu!
Nashindwa kumwambia maana kwanza ni mgeni mimi kisha ni mtu mzima kanizidi umri na mwenye familia yake huko street. Ninahisi nikimwambia atajisikia vibaya sana na atachukia kazi. Anapenda mno kuendesha gari inapotokea kazi ya nje anakimbilia funguo sasa humo ndani ya gari na vioo vimefungwa kwa kuwasha AC ni balaa, mazingira ya kazi ni muhimu kufunga vioo vya gari kila mara, hadi ninahisi nikishuka kwenye gari ninakuwa na mimi nimeambukizwa harufu!
Nifanye nini wakuu?