1800
JF-Expert Member
- Dec 27, 2010
- 2,215
- 603
Wadau wale wenye utaalamu wa sheria naomba msaada wenu!mimi ni mpangaji ambae mkataba wangu uliisha tarehe 10 july,mkataba wa awali ulikua wa miezi sita kwa kodi ya 720,000 kwa maana ya 120,000 kwa mwezi,baada ya mkataba kuisha niliongea na mwenye nyumba akanipa mkataba wa miezi minne yaani mpaka november 2012,na mnamo tarehe 29 july nikampatia 400,000/= na ikawa imebaki 80,000 ambayo nilimuahidi kumlipa in three weeks time!cha ajabu juzi amenigeuzia kibao,anadai anataka kukata kodi ya mwezi mmoja alafu anirudishie pesa yangu iliyobaki kwa kua anataka kumuingiza mtu mwingine!je sheria inasemaje hapa wadau,na nikitaka msaada atakapotaka kuja kunitoa ndani ya nyumba nianzie wapi ili kumzuia