Msaada plz; zuia hii abortion!!

Paddy

JF-Expert Member
Sep 22, 2010
462
304
Habari zenu wana MMU!

Kuna binti rafiki yangu nimeonana nae jana anasema ana mimba ya miezi mitatu na jamaa yake hana mpango nae na kashakimbia bongo hii. Yeye anasema hawezi kurudia makosa aliyowahi yafanya mama yake miaka hiyo alipomzaa yeye hivyo hiyo mimba lazima itoke.

Pia anasema huyo mtoto hawezi kumpenda na mama yake hana kipato cha uhakika kwa sasa. Mama yake pia ni mkali sana atamfukuza nyumbani akijua na yeye hana pa kwenda.

Ndugu zangu wapenda maisha tunaweza kuzuia hii mimba ambayo imepangwa KUTOLEWA IFIKAPO JUMATATU? Doctor ameshapatikana na kapewa advance ya kutosha. Wale wote ma pro-life tusaidiane ktk hili. Mi binafsi naumia sana kwa mauaji haya yanayoenda kutokea.

Hints:
1. Ashawahi taka kunywa sumu akaghairi
2. Doctor aliyekubali ni wa ile ile hospitali maarufu kwa abortion bongo - Mwananyamala.
3. Kama umeguswa, nini kifanyike?
 
Mi siwezi mzuia. Ila nataka akitoa mimba wacha itoke na kizazi kabisa. Ili akikosa mtoto baadae na kila atakapoona hana mtoto akumbuke alitoa mimba ikatoka na uzazi.
 
Mi siwezi mzuia. Ila nataka akitoa mimba wacha itoke na kizazi kabisa. Ili akikosa mtoto baadae na kila atakapoona hana mtoto akumbuke alitoa mimba ikatoka na uzazi.

Usisahau pia kuwa hiyo mimba ni ya tangu mwezi wa kumi (miezi 3) inaweza ikamuondoa kabisa duniani akitoa. Anasema yuko tayari kufa, nilipoongea nae alitoa machozi kabisa.

Mbali na yeye, tunaofahamu huu mpango ni mimi na rafiki yake wa kike ambaye ndo anaesuka deal la kutoa. Nitawezaje kuzuia hili?
 
Kwani Hali yake ya maisha alikua haijui alipokwenda kumvulia huyu bwana nguo bila kinga? Matangazo ya condom mpaka kwenye maguzo ya umeme kusoma hajui hata picha haoni? Mwambie asitoe mimba mama yake alimzaa yeye hakumua vp yeye a toe mimba?
 
Ungeweza kumuoa wewe na kulea hiyo mimba (fuatilia hadithi ya mange kimambi, ndo maana anampaisha sana babu)
Hongera kwa kuwa na moyo thabiti. All in all muambie anafanya kosa la mama yake kila siku, NGONO NZEMBE!!! Atatoa mimba ngapi kama anateremsha kyupi ovyo?
 
Lagaly, since alitaka ku commit suicide kama wakipatikana madaktari regstered 2 wanaweza kukata ushauri ikiwa ni ajili ya kuokowa hali ya kisakologia na uhai wa mwenye mimba. Hii ni sababu hata akizaa anaweza kufanya infanticide. GOODLUCK.
 
Kwani Hali yake ya maisha alikua haijui alipokwenda kumvulia huyu bwana nguo bila kinga? Matangazo ya condom mpaka kwenye maguzo ya umeme kusoma hajui hata picha haoni? Mwambie asitoe mimba mama yake alimzaa yeye hakumua vp yeye a toe mimba?

Swali zuri hili, huyu binti ni kati ya wale kina dada ambao hawawezi kuwazuia wanaume kufanya wayatakayo. Yeye alikua anajua cku hiyo ni hatari akamwambia mtu wake, ila akalazimishwa kufanya mapenz bila yeye kushiriki. Thanks 4ur contribution
 
Ungeweza kumuoa wewe na kulea hiyo mimba (fuatilia hadithi ya mange kimambi, ndo maana anampaisha sana babu)
Hongera kwa kuwa na moyo thabiti. All in all muambie anafanya kosa la mama yake kila siku, NGONO NZEMBE!!! Atatoa mimba ngapi kama anateremsha kyupi ovyo?

Good point. Thanks!
 
Ungeweza kumuoa wewe na kulea hiyo mimba (fuatilia hadithi ya mange kimambi, ndo maana anampaisha sana babu)
Hongera kwa kuwa na moyo thabiti. All in all muambie anafanya kosa la mama yake kila siku, NGONO NZEMBE!!! Atatoa mimba ngapi kama anateremsha kyupi ovyo?

Mimi nimeoa tayari. Nitafuatilia hiyo story, thanks. Alishindwa kuzuia ngono zembe alilazimishwa na huyo bf.
 
mwambie mama yake atamsaidia sana. Hakuna mzazi anaua mtoto wake kwa kupata ujauzito.

Sasa alipanda bangi akitegemea kuotesha mchicha?
 
Lagaly, since alitaka ku commit suicide kama wakipatikana madaktari regstered 2 wanaweza kukata ushauri ikiwa ni ajili ya kuokowa hali ya kisakologia na uhai wa mwenye mimba. Hii ni sababu hata akizaa anaweza kufanya infanticide. GOODLUCK.

Good point, ila cha muhimu ni kuokoa maisha ya wote wawili mama na mtoto. Miezi mitatu ukitumia ultra sound unasikia heart beats za mtoto. Well inawezekana ethics za madaktari zakaruhusu mimba itolewe kwa hali hii ila mimi napenda wote waishi. Huyo mtoto anaweza akawa our great leader
 
mwambie mama yake atamsaidia sana. Hakuna mzazi anaua mtoto wake kwa kupata ujauzito.

Sasa alipanda bangi akitegemea kuotesha mchicha?

Good point, nitaprint hii thread na kumpa asome ushauri wa wadau. Thanks!
 
Mwambie, akiitoa mimba hiyo, itamhaunt na hatapata amani kamwe (from the experience). Ila akizaa, she will never feel lonely (from the experience too).

Mungu hakupi mzigo ambao anajua huwezi beba! Na huyo mtoto ni blessing sio laana; amzae na kumpenda atampenda tu sana. Ila akiitoa atakuwa amejilaani mwenyewe, hata akitubu mara ngapi, bado atakuwa anajihukumu mwenyewe!

Sina jinsi ya kumshauri asifanye hicho kitendo! She will never know peace n true happiness, that l much l can say!
 
Mwambie, akiitoa mimba hiyo, itamhaunt na hatapata amani kamwe (from the experience). Ila akizaa, she will never feel lonely (from the experience too).

Mungu hakupi mzigo ambao anajua huwezi beba! Na huyo mtoto ni blessing sio laana; amzae na kumpenda atampenda tu sana. Ila akiitoa atakuwa amejilaani mwenyewe, hata akitubu mara ngapi, bado atakuwa anajihukumu mwenyewe!

Sina jinsi ya kumshauri asifanye hicho kitendo! She will never know peace n true happiness, that l much l can say!

Thanks kwa ushauri mzuri, nitaufikisha. Japo yeye anasema ni bora aishi na hiyo guilty ya kutoa mimba kuliko kuiacha. eti mama yake atamwua akijua hivyo. Kwani kama mama yake alipatiwa mimba akaachwa, yeye ndo imeandikwa hawezi kukosea kama mama yake?
 
Thanks kwa ushauri mzuri, nitaufikisha. Japo yeye anasema ni bora aishi na hiyo guilty ya kutoa mimba kuliko kuiacha. eti mama yake atamwua akijua hivyo. Kwani kama mama yake alipatiwa mimba akaachwa, yeye ndo imeandikwa hawezi kukosea kama mama yake?

Do u think ni rahisi kuua kihivyo? Who is a girl to u? Mama yake wamfahamu?
 
pls if u don't mind, ongeza details; how old is a girl, anafanya nini na mama yake anafanya nini pia!
 
Good point, nitaprint hii thread na kumpa asome ushauri wa wadau. Thanks!

Mtafutie mtu wa kumshauri cha zaidi mshirikishe mama yake maana huku ni kutafuta laana na hata ukinyamaza akitoa akafa we hutakaa kwa amani dhamira yako itakusuta. mimi nimeweza kuzuia mimba kutoka wk iliyopita nilichokifanya niliwaambia watu wake wa karibu japokuwa alikataa nisimwambie mtu akajua imejulikana akaona soo akaacha
 
pls if u don't mind, ongeza details; how old is a girl, anafanya nini na mama yake anafanya nini pia!

This girl nimemfahamu kwa miezi zaidi ya sita kupitia online chat platforms. She is jst a friend na so far simfahamu mama yake. she is 22 yrs old. hafanyi kazi kwa sasa, aliwahi kuwa librarian somewhere akaacha cz boss alikua anamtaka kimapenzi. mama yake alikua na some good business ila kwa sasa anaumwa biashara zimesimama hadi atakapopona.
 
Mtafutie mtu wa kumshauri cha zaidi mshirikishe mama yake maana huku ni kutafuta laana na hata ukinyamaza akitoa akafa we hutakaa kwa amani dhamira yako itakusuta. mimi nimeweza kuzuia mimba kutoka wk iliyopita nilichokifanya niliwaambia watu wake wa karibu japokuwa alikataa nisimwambie mtu akajua imejulikana akaona soo akaacha

Thanks mkuu kwa ushauri mzuri. nitajaribu kutekeleza japo niko busy sana hii wkend. itabidi pia nitafute namba ya mama yake kwenye cmu yake. wazazi wengine wanaweza kusupport itolewe bt nitajaribu hii option ya kumtafuta. bt je ctakua nimesababisha afukuzwe nyumbani? ataenda wapi?
 
Paddy; inaonekena anakuamini sana kwa jinsi alivyofunguka kwako; kwa kutumia trust hiyo hiyo l am sure. Unaweza msaidia kwani kwa kusoma post zako naona u r also a pro-life believer na pia una busara sana; u don't need us!

So do the needful, mpe council ya kutosha na support if u can! Kuna mtu alishauri umuoe it was a good one if u were not married. Support kubwa ni council yake na mama yake, lkn pia ni kumfanya aweze jitegemea. 22yrs ni mdada mkubwa tu!
 
Back
Top Bottom