Msaada pls; medical officers

Anfaal

JF-Expert Member
Jan 19, 2010
1,154
113
Ndugu wanajamvi;
Naomba kufahamu application kwa vyuo vyenye kozi za medical ofiicers hufanyika wakati gani?
Na je, hufanyika wizara ya Afya au kwenye chuo husika?
Vyuo kama KCMC, BUGANDO na MUHIMBILI wanatoa kozi hizo?
Na entry qualification kwa aliyemaliza na form six zikoje?
Na ada zake huwa ni kiasi gani.
Shukrani!
 
Nenda pale wizara ya Afya idara ya Training watakupa maelezo yote.KCMC,BUGANDO hawatoi CO bali wanatoa AMO pia Ifakara wanatoa AMO.CO ni Bumbuli,Kilosa,Kibaha,Lindi,Kigoma,Sengerema nk
 
Nilifikiri unaongelea jinsi ya kupunguza madeni yetu
 
Ndugu wanajamvi;
Naomba kufahamu application kwa vyuo vyenye kozi za medical ofiicers hufanyika wakati gani?
Na je, hufanyika wizara ya Afya au kwenye chuo husika?
Vyuo kama KCMC, BUGANDO na MUHIMBILI wanatoa kozi hizo?
Na entry qualification kwa aliyemaliza na form six zikoje?
Na ada zake huwa ni kiasi gani.
Shukrani!


mkuu kwa muhimbili nadhani ungeenda kwenye website yao ina kila kitu ukiiperuzi vizuri inakuelekeza fungua hiyo link hapo chini itakupeleka muhas

Muhimbili University of Health and Allied Sciences -MUHAS - Home
 
Nenda pale wizara ya Afya idara ya Training watakupa maelezo yote.KCMC,BUGANDO hawatoi CO bali wanatoa AMO pia Ifakara wanatoa AMO.CO ni Bumbuli,Kilosa,Kibaha,Lindi,Kigoma,Sengerema nk
Ndugu asante saana kwa msaada. Unajua tatizo wengine tunaishi Nyampulukano. Ukijaribu kupiga simu ofisini hapo Dar majibu huwa hayaeleweki. Yaani ofisi zetu zimezoea manual vitu automated haviwezekani. Hiivi kuweka info kama hiyo kwenye mtandao kuna shida gani? Asante pia kwa maelezo ya vyuo hivyo, lakini sijaelewa kidogo. Nini tofauti kati ya Clinical Officers, Medical Officers na assistant Medical Officers? Nani anaweza kujiunga na MD katika hao straight bila longolongo?
 
Mkuu clinical officers ndio wale medical assistants, kama sikosei wengi wao walikuwa ni form IV ambao wana certificate ya miaka mitatu ya medicine, wakati assistant medical officers wana diploma ya miaka mitatu. Medical officers ndio MD ambao wana degree ya medicine kwa angalau miaka mitano.
Muhimbili hawatoi course za clinical officers au assistant medical officers, bali wanatoa degree ya medicine kwa wanafunzi waliofaulu vizuri kidato cha sita. Hawachukui wanafunzi wanaojiendeleza tokea hizi cadre za chini za clinical officers au AMO bali huchukua wanafunzi fresh toka shule. Muhimbili kuna ushindani mkubwa, na angalau mtu unatakiwa uwe na point 5 kwa masomo ya fizikia, biologia na Chemia.
Vyuo kama vya IMTU, Kairuki, KCMC, UDOM na Bugando wanapokea wanafunzi wa sifa kama hizo juu, ila pia wanapokea hata wale wanaojiendeleza (sina uhakika na Bugando, na UDOM). Ila applications za degree ya medicine kwa vyuo vyote yafanyika kupitia TCU.
 
Mkuu clinical officers ndio wale medical assistants, kama sikosei wengi wao walikuwa ni form IV ambao wana certificate ya miaka mitatu ya medicine, wakati assistant medical officers wana diploma ya miaka mitatu. Medical officers ndio MD ambao wana degree ya medicine kwa angalau miaka mitano.
Muhimbili hawatoi course za clinical officers au assistant medical officers, bali wanatoa degree ya medicine kwa wanafunzi waliofaulu vizuri kidato cha sita. Hawachukui wanafunzi wanaojiendeleza tokea hizi cadre za chini za clinical officers au AMO bali huchukua wanafunzi fresh toka shule. Muhimbili kuna ushindani mkubwa, na angalau mtu unatakiwa uwe na point 5 kwa masomo ya fizikia, biologia na Chemia.
Vyuo kama vya IMTU, Kairuki, KCMC, UDOM na Bugando wanapokea wanafunzi wa sifa kama hizo juu, ila pia wanapokea hata wale wanaojiendeleza (sina uhakika na Bugando, na UDOM). Ila applications za degree ya medicine kwa vyuo vyote yafanyika kupitia TCU.
Asante kwa kunijibu medical officers nadhani kuna tofauti na MD maana nijuavyo MD ni medical doctors. Kuna miaka ya nyuma nadhani vyeo vilibadilishwa kwa bahati mbaya si professional yangu kwahiyo ndio maana nikaomba ufafanuzi. Pia asante kwa maelezo mengine ingawa kuhusiana na fees sijaona maelekezo yake. Lakini pia nimefanikiwa kuipata porspectus ya muhimbili wanatoa diploma nyingi ila hiyo haipo na kuingia kwa equivalent qualification inawezekana. Ila nimechoka kitu kimoja inamiss some info yaani inatakiwa uende ofisini ndio watajibu baadhi ya maswali.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom