Msaada nimeshindwa kesi mara mbili kutokana na kukosea taratibu!

alovera

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
220
173
Naomba kulileta kwenu,ni hivi Mzee wangu (Marehemu) alikuwa na Shamba ekari 50,kati ya hizo ekari 20 zimevamiwa,tulifungua kesi kijijini lakini kijiji hakitukupa ushirikiano hivyo tukaenda Baraza la Kata tukashinda,Mpinzani wangu akaenda Baraza la Ardhi la Wilaya akakata rufaa na akatushinda sababu kubwa aliyefungua kesi hakuwa na uhalali,sababu tulikuwa hatujafungua mirathi mahakamani (Hapa ndipo tuliposhindwa kwa mara ya kwanza).
Mara ya pili tulifuata taratibu zote za kufungua mirathi,na msimamizi wa mirathi nikawa mimi tukafungua kesi Baraza la Ardhi ya wilaya,tukawashtaki aliyevamia pamoja na Serikali ya Kijiji ,tukawapa kijiji notice ya siku 30. Kilichotokea kesi ilivyoendelea ilipofika hearing Serikali ya Kijiji na Mvamizi na Serikali ya kijiji ilitetewa na wakili Mmoja na maajabu kuwa notice tuliyowapelekea walikana kuwa hawakuipokea na tena haikuonekana mahakamani pamoja na kuwa tuliwapelekea na risiti ya kulipa mahakamani tulikuwa nayo. Hivyo wakili wao akaomba shauri litupiliwe mbali na kweli likatupiliwa mbali kwa kuwa tulishindwa kuithibitishia mahakama kuwa notice haikupelekwa kijinini (nikashindwa mara ya pili).Hivi sasa tunapanga kufungua kesi baraza la ardhi la wilaya kwa mara nyingine tena
Msaada ninaomba kutoka kwenu wana Jamvi
1. Je ni sawa kijiji kutetewa na wakili Binafsi pamoja na Mtuhumiwa (Mvamizi)?
2.Utaratibu wa kuishtaki serikali ya kijiji ukoje
3.Naomba ushauri kwa ujumla jinsi ya kudai haki yetu ili tusije shindwa tena kwa technicalities?
Nawasilisha!
 
1. Ni sawa
2. Toa notisi ya siku 30 kwa kijiji ie Serikali ya kijiji-afisa mtendaji wa kijiji na kopi kwa mwenyekiti. Yaani barua ni kwa Afisa mtendaji wa s. Kijiji
3. Toa notisi walau ya siku 14 kwa mvamizi
4. Kama wote hawatakujibu kafungue mashtaka
5. Awamu hii notisi hakikisha wamesaini kua wamepokea unaweza tumia njia yeyote ya kupata ushaidi. Sishauri kamera, japo si mbaya
 
Anapatikana Mkoa upi na anapatikanaje?
Suala lako lingekuwa mkoa alipo ilikuwa rahisi kukushauri kama anatekeleza majukumu yake, lakini nje ya Mkoa wake (kituo chake cha kazi) atakuhudumia kama mwanasheria
 
1. Ni sawa
2. Toa notisi ya siku 30 kwa kijiji ie Serikali ya kijiji-afisa mtendaji wa kijiji na kopi kwa mwenyekiti. Yaani barua ni kwa Afisa mtendaji wa s. Kijiji
3. Toa notisi walau ya siku 14 kwa mvamizi
4. Kama wote hawatakujibu kafungue mashtaka
5. Awamu hii notisi hakikisha wamesaini kua wamepokea unaweza tumia njia yeyote ya kupata ushaidi. Sishauri kamera, japo si mbaya
Dispatch yenye maelezo ya kutosha kama "BARUA YA KUSUDIO LA KUISHTAKI SERIKALI YA KIJIJI" isainiwe na tarehe iandikwe itaweza kusaidia sana
 
Naomba kulileta kwenu,ni hivi Mzee wangu (Marehemu) alikuwa na Shamba ekari 50,kati ya hizo ekari 20 zimevamiwa,tulifungua kesi kijijini lakini kijiji hakitukupa ushirikiano hivyo tukaenda Baraza la Kata tukashinda,Mpinzani wangu akaenda Baraza la Ardhi la Wilaya akakata rufaa na akatushinda sababu kubwa aliyefungua kesi hakuwa na uhalali,sababu tulikuwa hatujafungua mirathi mahakamani (Hapa ndipo tuliposhindwa kwa mara ya kwanza).
Mara ya pili tulifuata taratibu zote za kufungua mirathi,na msimamizi wa mirathi nikawa mimi tukafungua kesi Baraza la Ardhi ya wilaya,tukawashtaki aliyevamia pamoja na Serikali ya Kijiji ,tukawapa kijiji notice ya siku 30. Kilichotokea kesi ilivyoendelea ilipofika hearing Serikali ya Kijiji na Mvamizi na Serikali ya kijiji ilitetewa na wakili Mmoja na maajabu kuwa notice tuliyowapelekea walikana kuwa hawakuipokea na tena haikuonekana mahakamani pamoja na kuwa tuliwapelekea na risiti ya kulipa mahakamani tulikuwa nayo. Hivyo wakili wao akaomba shauri litupiliwe mbali na kweli likatupiliwa mbali kwa kuwa tulishindwa kuithibitishia mahakama kuwa notice haikupelekwa kijinini (nikashindwa mara ya pili).Hivi sasa tunapanga kufungua kesi baraza la ardhi la wilaya kwa mara nyingine tena
Msaada ninaomba kutoka kwenu wana Jamvi
1. Je ni sawa kijiji kutetewa na wakili Binafsi pamoja na Mtuhumiwa (Mvamizi)?
2.Utaratibu wa kuishtaki serikali ya kijiji ukoje
3.Naomba ushauri kwa ujumla jinsi ya kudai haki yetu ili tusije shindwa tena kwa technicalities?
Nawasilisha!
acha kichwa ngumu tafuta wakili
 
Back
Top Bottom