Fanya na fata hatua zifuatazo, taratibu na kwa amani kabisa:
1. Anzisha Chama cha Maendeleo ya Kanda ya Ziwa (MKAZI). Jina si neno, muhimu upate wanachama kutoka Tanzania nzima (kwa mujibu wa sheria za Tendwa.
2. Ukipata kiti kimoja tu bungeni anza kumwaga sera zako za kutaka kujitenga kutokana na kupuuzwa kwa Kanda ya Ziwa kimaendeleo. Serikali itaogopa na kuanza kuleta maendeleo au wakiendelea kuwapuuza tayari MKAZI kitakuwa kimeshapata umaarufu.
3. Pigania ianzishwe kura ya maoni kama ile ya Sudani kusini. Utafanikiwa kwani unaloliona wewe wameliona Watanzania wengi katika maeneo yao. Hatimaye Tanzania itagawika (Kanda ya Pwani, Kanda ya Kusini, Kanda ya Kaskazini na Kanda ya Zanzibar, kama ilivyogawika Urusi au Yugoslovakia).
Ikishindikana yote hayo kwa njia ya amani, ingia msituni.
Mkuu.
Andamana kama CHADEMA au unga mkono CHADEMA.
Bei zimeshuka tayari baada ya maandamano ya CDM?
Au huko uliko hazijashuka?
Unataka kuanzisha nchi, kusanya sahihi za wakaazi wa hiyo sehemu unayotaka iwe nchi halafu, uwapatie wabunge wa hiyo sehemu wapeleke bungeni,, ukiwakatia 10% mkuu soon utapata mkataba wa kuanzisha nchi yako!
Lazima upatikane utaratibu ili kila kanda ijitahidi kuhakikisha hiyo rasilimali iliyoko kule inafaidisha.
Pwani kuna bahari kubwa, uvuvi unalipa jamani matokeo yake hakuna kinachoendelea baharini kisa madini.
Zikipatikana japo kanda tano au sita halafu zikatilia mkazo viwanda huko huko hata kama mtaamua iwe Tanzania federation hapatakuwa na huu msongamano kila mtu kwenda Dar.
Hii nchi kila sehemu kuna resources nina uhakika usimamizi umeshindikana chini ya kichaka cha wezi (Si C Em)
Dah....... Nilijua ni mimi tu mwenye wazo kama hilo, mkoa wangu wa mara ni noma, hata maji ya ziwa victoria lililo hatua kadhaa hatuna. Ila wanajeshi kanda ya ziwa wapo kibao waliostaafu so washika mitutu wapo na jeshini karibia nusu ni kanda ya ziwa kwahiyo ipo day huyu bwana atatoka kimabavu
Naipenda Tanzania. Nataman Tanzania ingekuwa na uwezo wa kuichukua Kenya na Uganda iwe sehemu ya Tanzania. Nawapinga wote wanaotaka kuipunguza Tanzania. Tanzania ikiwa ndogo na rasilimal pia zitapungua, posho za wabunge zitapungua. Viongoz wetu wataish kwa tabu sana. We tulia umuombe mungu, ipo siku mtakumbukwa.
Waelimishe watu wote wa maeneo yako na yale
yanayowazunguka kwamba wachague CHADEMA tu
ndicho chama pekee kitakachoweza kuwafanya mnunue mfuko
wa cement kwa bei ya shs.6,000/=. Usipate tabu ya kuunda nchi yako.
Chagua CHADEMA, chagua MAENDELEO.
Ingia tu msituni tena hamna hata kuleta Jwtz utakuja kutolewa na askari wa wanyama pori kama jangili wa kuua wanyama coz huko porini im sure mtaua swala na pundamilia ili mpate msosi.
USifanye mchezo na maporini kasome wasifu wa Che Guevara wenzako walishindia kula miwa porini.
Kigoma walianza wakidai nchi huru kumbe somo liliwaingia, Mtwara nako kimenuka.
Ila bado kanda ya ziwa wanaibypass, wapi kiwanda cha Cement shy_wapi Int. aiport Mwanza
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.