Vipi wakuu! Naombeni msaada wa jinsi ya kuuweka ujumbe wangu ili uweze kusomeka hapa chini kila ninapoandika post au ninapojibu post za wenzangu, ntatoa mfano kama sijaeleweka maana kiswahili kigumu jamani. Utakuta ukisoma baadhi ya posts humu ndani, mwisho wa ile post mlengwa ameambatanisha ujumbe wake kuhusiana na mtazamo wake, bila shaka nimeeleweka.