X_INTELLIGENCE
JF-Expert Member
- Mar 25, 2014
- 9,647
- 12,212
ndugu zangu watanzania wenzangu kutokana na mwenendo mbovu wa serikali yetu yenye kutumia mabavu...serikali inayoshindwa kufuata misingi ya kidemokrasia...kwa utafiti mdogo nilioufanya nimegundua watu wa hali ya chini ndio tunao ubeba na kuupandisha uchumi wa nchi yetu...huku pakiwa na migodi mikubwa ya dhahabu...mito...na tumezungukwa na eneo kubwa la bahari bila kusahau mlima wa KILIMANJARO...ivi inakujia akilini leo mtanzania mwenye kipato cha chini kuchangia kodi ya pango...yani kwenye nchi yangu pakulala pia nipalipie? maji nilipie...umeme nilipie...sukari bei juu...chumvi nk....na kote huko tunakatwa makato...hivyo naomba vipengele muhimu vya kuzingatia ili niweze kuishitaki serikali kwani inatunyonya sana wananchi lasivyo watuambie madini wanapo yapeleka...kinachosababisha niwe na hamu ya kuishitaki hii serikali ni kutokana na mfumuko wa ushuru...hasa iki kitendo cha kulipia pango kinanikera sana...ebu angalia nimejenga nyumba kwa cement ya Tanzania...mabati ya Tanzania...misumari vyote vinatoka Tanzania sasa hiyo pango ya nini na ule ushuru niliolipia kwenye vifaa vya ujenzi umeenda wapi? nielewesheni maana hapa nilipo nimepagawa najikuta naichukia sana Tanzania nakosa amani na nchi yangu sijui nikaishi wapi maana ata nikijikwamua kwa mtaji wa nyanya na bamia bado mgambo watakuja kupiga teke bidhaa zangu...tuna mbuga kubwa za wanyama ambazo ni kivutio kikubwa sana kwa watalii fedha hizo zinaenda wapi?
wataalamu wa sheria nisaidieni sina mzaha hapo
wataalamu wa sheria nisaidieni sina mzaha hapo