Jamani wadau nisaidieni mwenye kujua haya mambo, ni umri upi unaoshauriwa kitaalamu kumtahiri mtoto wa kiume, na je kuna njia ngapi za kufanya hiyo kitu.
Maana kuna maneno yanasema eti ukimfanyia akiwa bado mdogo kuanzia miaka 0 hadi mmoja eti atakuja kuwa dhaifu katika ile shughuli ya kikubwa, wengine wanasema ukimfanyia kakua ndio hiyo kitu itamtokea akiwa mkubwa
Pia njia ipi ni salama zaidi mimi najua ya kukata na kushonwa naambiwa ipo nyingine yakufunga na plastiki, je ipi ni nzuri?
Nategaemea msaada wenu waungwana, maana kunasehemu nilisoma eti matatizo mengi ya wanaume kushindwa kuwatimizia wepenzi wao tohara isiyo sahihi ni moja ya sababu
Kuwahi kutahiri na hizo imani ni vitu wiwili tofauti...
Biblia inasema mtoto atahiriwe ndani ya siku 14... lakini ni vizuri akitahiriwa at least akiwa na miezi mitatu.... Hii itasaidia sana kwa sababu watoto wa kiume mara nyingi huugua sana UTI especially akianza kutambaa, na pia kwa umri huo anapona haraka sana, 7 days anakuwa amepona.
Mtoto kupata UTI ni kutokuwa makini kumbadilisha anapojisaidia. wanangu siwatahiri chini ya miaka miwili na hawajawahi kuugua UTI. Na kama mtu hauko makini utashangaa mtoto katahiriwa na bado anasumbuliwa na UTI.
Baada ya mimi kukosa jibu la kitaalamu kuhusu lini mtoto anapaswa kutahiriwa niliamua kuamini tu ushauri wa kitaani kuwa kutahiri mtoto mchanga kunamfanya awe na kibamia.
Mwanangu nimemtahiri na miaka miwili na alipona in a week. Tena nilinfanyia pale Regency wana wataalamu wazuri kuanzia wa nusu kaputi, doctor wa watoto na bingwa wa operation; hivyo hakuna mistake anakuwa amezungukwa na wataalamu.
Tena hakuwahi kuvaa kanga kama wengi niwaonavyo...yani doctor kanambia mvalishe kaptula kama kawaida...na hakulia hata kidogo zaidi ya kulia sindano ya nusu kaputi...katoka hapo kaendelea na mishe mishe zake za michezo. Baada ya wiki tukatoa nyuzi.