Wadau habari,nilikua naomba msaada wenu jinsi ya kuweza kupata mikopo midogo midogo ambayo ina masharti nafuu kwa ajili ya biashara hasa ya kilimo,chakula na ufugaji!mimi ni kijana niliegraduate miaka minne iliyopita,na nimekata tamaha na kupata ajira,hivyo nimedhamiria kujiajiri/kua mjasiriamali!nataka nitumie mkopo huo kama mtaji wa kuanzishia biashara,ila kikwazo kwangu ni dhamana,maana sina nyumba wala kiwanja,nina pori tu la heka mbili lililopo maeneo ya Mikese Morogoro ambalo nina hati za kimila!nataka pori ilo liwe ndio mkombozi wangu kiajira!naombeni ushauri wenu wadau!