kisu
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 1,003
- 381
Salam wana JF. Mimi ni mhasibu katika kampuni ya kimataifa hapa ughaibuni. Kabla hajaja bosi wa pili, huyu bosi wa kwanza (Resident Manager) na pia anamiliki 35% ya local branch na ana power of attorney (anaweza kusaini cheki na mambo mengine) nilikuwa nampelekea Ripoti za kila mwezi (outstanding invoices na Income Statement). Alipokuja bosi wa pili hata yeye ana power of attorney (March 2011) ku replace nafasi ya bosi wa kwanza (Resident Manager) na bosi wa kwanza kuwa (Advisor) kwa mapendekezo ya partners, mimi niliendelea kuwapa ripoti za mwezi wote wawili. Karibu miezi miwili iliyopita bosi wa pili alinikataza kumpa ripoti za mwezi bosi wa kwanza na ripoti zote zipitie kwake, lakini bosi wa kwanza hataki na anataka nimpe ripoti directly (anasema company law inamruhusu) bila kupitia bosi wa pili. Nna waheshimu mabosi wote wawili, na inaonyesha wana uhasimu hapo kazini. Tafadhalini msaada kwa anaejua sheria. Asanteni.