Hamjambo wapendwa, hope wote mmeamka bien, kwa wagonjwa na matatizo mbalimbali poleni. Leo nimepata kisa kimenitatiza kidogo naomba kushare nanyi wapendwa tumsaidie huyu ndugu. Huyu mkaka amezaa na mke wa mtu bila mume kujua na wote wanaendelea kumtunza mtoto sasa ana umri wa miaka mitano. Tatizo mdada anaogopa kusema ukweli kulinda ndoa yake, na mkaka (mwizi) anataka atambulike kwa mwanae japo na yeye ana mke.Mke wa mwizi keshaelezwa kuna mtoto nje kakubaliana na hilo japo hajui ni wapi/ kwa nani. Na familia ya mdada inajua kila kitu.Familia ya kiume na mke wa mwizi imekomaa inataka kumuona huyo mtoto. Mume wa dada hana ajualo. Nisaidieni kaka aanzie wapi, na familia ya mkaka mwizi na mdada ni marafiki toka udogoni..
Nawasilisha.
Nawasilisha.