Wadau habari,mimi ni kijana niliyemaliza form four mwaka 1998 na nilipata division 3,baada ya hapo nikakimbilia nje katika kujaribu kupigania maisha,katika kukaa kwangu kote huko!sikufanya jitihada sana za kupata elimu zaidi ya kusaka mkate ila mwaka wa mwisho kabla sijaamua kurudi nyumbani nikaamua angalau nirudi na kijicheti chochote na nikafanya kozi ya business computing ambayo ilikua ni level ya Foundation degree na ni kozi ya mwaka mmoja,sasa nimerudi nyumbani,mbali ya shughuli zangu!nahitaji kujiendeleza zaidi kielimu,sasa wadau naombeni ushauri wenu,nataka nifanye kozi ya diploma au degree hasa katika masuala ya business administration,je vijezo vyangu vitakidhi kuanza na level hiyo na siyo level ya certificate?au je nikifanya certificate ya adult education nitaruhusiwa kufanya degree?asanteni wadau na nasubiri msaada wenu