Sipo
JF-Expert Member
- Jul 25, 2008
- 2,139
- 91
Leo asubuhi nimeingia kwenye email address yangu kusoma email kama kawaida yangu lakini cha ajabu nimekuta contacts zote nilizokuwa nimeifadhi zimefutwa. Na kibaya zaidi kuna watu wangu wa muhimu sana tena ninaofanya nao biashara wananilalamikia kwa kuwatumia email message za ajabu. Sasa najiuliza nini kimetokea kwenye email yangu wakati hakuna mtu mwingine yeyote anayeifahamu password yangu. Am real confused maana nimepoteza contacts za muhimu sana kwenye kazi zangu za biashara ndani na nje ya nchi. Mimi natumia yahoo.com. Nisaidieni wana JF ili niju ni nini kimetokea na nifanye nini ili kuzuia hali hii isitokee tena. Asanteni