Msaada Gharama za Umeme

Goodrich

JF-Expert Member
Jan 29, 2012
2,091
1,177
Naomba msaada wa kueleweshwa gharama za umeme (Electricity Tariffs).
Nimejaribu kupitia jedwali hapa chini lakini sijaelewa.
i.e viwango vilivyowekwa ni kwa muda gani ?
mtu anayetumia wastani wa 150 kwh kwa mwezi anakuwa kundi gani ?

Tariffs ni hizi hapa:

Electricity Charges

Ukitoa msaada wa kuelewesha utakuwa umetusaidia wengi tunaohangaika na bili za tanesco Natanguliza shukrani
 
Ukweli hata mimi nahitaji sana kujua kuhusu utozaji wa gharama za umeme wa Tanesco.
Maana kuna wanaolipa fedha nyingi, na wengine wanalipa kidogo kwa matumizi yanayofanana.
Tujuzeni kuhusu haya magroup ya tariff.
Nasubiri mwenye ubinadamu aje atoe elimu fupi.
 
Ukweli hata mimi nahitaji sana kujua kuhusu utozaji wa gharama za umeme wa Tanesco.
Maana kuna wanaolipa fedha nyingi, na wengine wanalipa kidogo kwa matumizi yanayofanana.
Tujuzeni kuhusu haya magroup ya tariff.
Nasubiri mwenye ubinadamu aje atoe elimu fupi.

Tujuzeni japo kwa ufupi
 
Mimi navyoelewa kwa wewe unayetumia 150Kwh per month upo kwenye category T1 ambapo unit moja ni Tsh 221 na service charge ni Tsh 3,841 gharama zote hizo bila VAT. Kwa ufupi wewe utakuwa unatumia kwa mwezi kati ya Tsh 40,000 mpaka 50,000 kwaajili ya umeme tu. Bei ya umeme Tz ipo juu kwakweli
 
Asee kwakweli umeme huu nitatizo kubwa sana sisi imelazimika tutumie umeme usiku tu mchana mzima tunazima menswech nabado tunalipa uwastani wa 140000 kwa mwezi na hapo nyuma tulikuwa tunatumia umeme wa shilingi 30000 kwamwezi, nyumbani hatuna chochote zaidi ya freji2 na TV2. zaid ya hapo ni mapangaboi tumelalamika Tanesco wanadai gharama zimepand hakuna hitilaf ya mita. sijui hili tatizo ni letu tu au kunawengine wanalo
 
Asee kwakweli umeme huu nitatizo kubwa sana sisi imelazimika tutumie umeme usiku tu mchana mzima tunazima menswech nabado tunalipa uwastani wa 140000 kwa mwezi na hapo nyuma tulikuwa tunatumia umeme wa shilingi 30000 kwamwezi, nyumbani hatuna chochote zaidi ya freji2 na TV2. zaid ya hapo ni mapangaboi tumelalamika Tanesco wanadai gharama zimepand hakuna hitilaf ya mita. sijui hili tatizo ni letu tu au kunawengine wanalo

Mkuu hiyo kwenye nyekundu kwa matumizi uliyotaja haiwezekani kabisaaaaaaaaaaaaaaaa! Utafikiri una kiwanda? Au nyumba ni ya wapangaji wengi na kuna wanaotumia umeme umeme kufanyia welding wakati wa mchana mkiwa kazini? Au Kuna mpangaji ana kijibwawa cha samaki (Aquarium)?. Mimi napikia umeme, nachemshia maji birika la umeme, natumia pasoi ya meme, friji iko on masaa 24, TV iko on almost masaa 16 kwa siku, taa 4 (tube light) zinawaka kuanzia saa 1 jioni mpaka saa 12 asubuhi na bill yetu kwa mwezi haizidi 50,000. Kama ni kweli na unatumia mita za Tanesco kuja kusoma kila mwezi, fanya mpango fasta ufunge LUKU.
 
Mkuu hapa natumia LUKU na hii imefungwa baada ya zoezi lao la miwisho sasa sijui tatizo nini na nyuma nayoishi mpangaji ni mimi na mwenyenyumba anakaa upande wa pili nayeye hana kitu chochote ndani mwake zaidi ya Jokofu na TV pasi tunapiga maramojamoja sana mkuu ni mgum kuamini lakini ntascan stakabazi za malipo niwawekee hapa muone tarehe zinavyo fatana sijui lakufanya mpaka sasa mwenyenyumba nimeongea nae marakibao ameenda tanesco wanasema mitayao ipo ok haina tatizo mkuu sijui inakuwaje
Mkuu hiyo kwenye nyekundu kwa matumizi uliyotaja haiwezekani kabisaaaaaaaaaaaaaaaa! Utafikiri una kiwanda? Au nyumba ni ya wapangaji wengi na kuna wanaotumia umeme umeme kufanyia welding wakati wa mchana mkiwa kazini? Au Kuna mpangaji ana kijibwawa cha samaki (Aquarium)?. Mimi napikia umeme, nachemshia maji birika la umeme, natumia pasoi ya meme, friji iko on masaa 24, TV iko on almost masaa 16 kwa siku, taa 4 (tube light) zinawaka kuanzia saa 1 jioni mpaka saa 12 asubuhi na bill yetu kwa mwezi haizidi 50,000. Kama ni kweli na unatumia mita za Tanesco kuja kusoma kila mwezi, fanya mpango fasta ufunge LUKU.
 
Back
Top Bottom