Junius
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 3,181
- 139
Ule wakati wa Klabu kubwa maarufu za Tanzania, Yanga na Simba, ambazo ni wababe wa soka la nyumbani huku zikiwa urojo katika medani za kimataifa unakaribia kufikia hatima.
Hatua hiyo inakuja baada ya timu ya Yanga kujikuta ikizidiwa ubavu wa kifedha na timu ya Azam FC,inayopigana kwa jeuri ya fedha kuwan'goa jangwani wachezaji wa kutumainiwa wa Yanga, Mrisho Ngassa na libero hodari wa timu hiyo,mtoto wa Kipemba, Nadir Haroub "Cannavaro".
Viongozi wa klabu hiyo kongwe katika medani ya soka la bongo wamekiri wazi kuwa hawana ubavu wa kuwazuia wachezaji hao kwa vile Azam FC, imetangaza kuwapa dau kubwa zaidi ambalo Yanga licha ya kuwa na matajiri na washabiki wengi nchini hawana uwezo nalo.
Huku hali hiyo ikionekana kuwanchanganya viongozi wa Yanga tayari Mrisho Ngasa amenukuliwa akisema kinaga ubaga kuwa hayupo tayari kubaki Yanga kwa mshahara wa 400,000, wakati Azam wametangaza kumlipa zaidi ya mara tatu ya kiasi hicho.
Habari zaidi bofya hapa.Dullonet Tanzania | Just Call it Real Solution for News and Information
Hatua hiyo inakuja baada ya timu ya Yanga kujikuta ikizidiwa ubavu wa kifedha na timu ya Azam FC,inayopigana kwa jeuri ya fedha kuwan'goa jangwani wachezaji wa kutumainiwa wa Yanga, Mrisho Ngassa na libero hodari wa timu hiyo,mtoto wa Kipemba, Nadir Haroub "Cannavaro".
Viongozi wa klabu hiyo kongwe katika medani ya soka la bongo wamekiri wazi kuwa hawana ubavu wa kuwazuia wachezaji hao kwa vile Azam FC, imetangaza kuwapa dau kubwa zaidi ambalo Yanga licha ya kuwa na matajiri na washabiki wengi nchini hawana uwezo nalo.
Huku hali hiyo ikionekana kuwanchanganya viongozi wa Yanga tayari Mrisho Ngasa amenukuliwa akisema kinaga ubaga kuwa hayupo tayari kubaki Yanga kwa mshahara wa 400,000, wakati Azam wametangaza kumlipa zaidi ya mara tatu ya kiasi hicho.
Habari zaidi bofya hapa.Dullonet Tanzania | Just Call it Real Solution for News and Information