Mrema TLP na picha ya aibu

Jamani mpeni pole kikombe cha babu kinaendelea kufanya kazi siku saba bado ana siku ya 3 now.
 
tungekuwa na waandishi 20 kama hawa TZ pamoja na vyombo vya habari vya kuchapisha kazi zao labda tungepanda nafasi 2 kutoka chini ya mstari wa umasikini duniani! Hongera sana mwandishi/mpiga picha
Nasikia kuna mbunge wa CCM kalalamika eti huyo mwandishi wa habari anae toa picha za wabunge wanao sinzia bungeni anatafuta umaarufu
 
Nadhani kusinzia inaruhusiwa ili mradi asikorome. Vinginevyo atasaini vipi posho ya kukaa Bungeni?
 
Kuna wakati huwa nashindwa kuelewa kama kweli TZ ipo siku tutakuwa na maisha safi, mawaziri wanasinzia kwenye vikao pia wabunge wenye jukumu la kuisimamia serikali wanasinzia, mrema na wabunge wa ccm yani huwezi kujua kama wamejiandaa kuchangia hoja au vipi
 
hapo yupo kwa ajili a kusign posho maana angekuw makini angeenda kupumzika kuliko kujidhalilisha kwa wapiga kura wke
 
Kama utapata gazeti la Mwananchi tarehe 30/06/2011 ukurasa wa mbele kabisa basi utakutana na picha ya muheshimiwa Augustino Lyatonga Mrema mbunge wa jimbo la Vunjo akiwa amelala na udenda ukiwa unamtoka kwenye kikao cha bajeti bungeni. Kweli kwa mtazamo wangu mimi binafsi siungi hoja ya wapiga picha kutoa picha kama hii hata kama ni uhuru wa viombo vya habari huku ni kumzalilisha mtu, gazeti la Mwananchi tena wanasema gazeti la watu makini huku sasa ni kuvuka mipaka naomba wanaJF wenzangu mimi sio mwanachama wa TLP naona ifikie wakati pale bungeni wapiga picha wawe wanapewa mipaka ya kupiga picha. Nawasilisha lakini siungi hoja picha kama hizi au tulifananishe gazeti na magazeti ya udaku?
270366_2034382311945_1615806745_1967168_2890452_n.jpg
 
Kuna wakati huwa nashindwa kuelewa kama kweli TZ ipo siku tutakuwa na maisha safi, mawaziri wanasinzia kwenye vikao pia wabunge wenye jukumu la kuisimamia serikali wanasinzia, mrema na wabunge wa ccm yani huwezi kujua kama wamejiandaa kuchangia hoja au vipi

hawa tatizo wanafakamia sana misosi wanayonunulia kwa pesa za wizi kupitia posho, ndo maana wanachama wenzake na mrema (najua mnawajua, wale wa kijani) unakuta matumbo yao yamepanda kama vichuguu au mama mwenye mim.a ya miezi nane, embu linganisheni tumbo la wasira alipokuwa amelala majuzi na lile la Obama...hii ni kwa sababu wasira ni mla posho wakti Obama ni Thinker
 
Ni aibu sijui anajisikiaje?mwenyewe amechoka sijui kwa nini asistaafu hizi kazi akabaki kuangalia vijana wanafanyaje kazi na kuwashauri na hili ndio tatizo la wazee walioko kwenye vinafasi wanadhani watoto walio walea hawajakua, wanang'ang'ania wanakufa vibaya, ni vizuri wazee wakawaacha vijana wachukue nafasi wao wabaki washauri tu. au tuseme hawakujiandaa kuwa wazee kwa hiyo bado wanatafuta maisha?

Mamzalendo, kwenye serikali ya ccm uwezo na kipimo cha kuwa mtu anaweza kufanya kazi flani ni UMRI na TUMBO KUBWA aka KITAMBI aka ugonjwa wa obesity. Ukiwa na umri mdogo - au sema damu changa (kwao miaka 30-40 ni umri mdogo eti!!!!!!!!!) na umbo dogo au jembamba wewe hufai
 
Kuna wakati huwa nashindwa kuelewa kama kweli TZ ipo siku tutakuwa na maisha safi, mawaziri wanasinzia kwenye vikao pia wabunge wenye jukumu la kuisimamia serikali wanasinzia, mrema na wabunge wa ccm yani huwezi kujua kama wamejiandaa kuchangia hoja au vipi

hizi ni mbongo zilizokwishachoka jamani, zinalazimishwa tu ili mradi posho ipatikane. ni business as usual hawa kwa hiyo hawafikiri chochote. mtu anayesumbuliwa na fikra za umaskini wa wana wa nchi anaowaongoza hawezi lala fofofo dizaini hii hadi anatapika denda utafkiri mbege ya kiraracha!!! aibu gani hii jamani kwa vizee hivi ving'ang'anizi???, wazee pumzikeni achieni vijana wajenge Tanzania, mzee kama huyu wa kiraracha heshima kwake ingekuwa kwa sasa awe na ngombe wake wa kisasa kama kumi hivi pale kiraracha anakunywa tu maziwa yake taratibu huku anatungojea vijana tumfuate kuomba ushauri. Si mjifunze hata kwa kina Mtei wa "Chama" jamani????!! [nikisema tu "Chama"(cha siasa) bila shaka naeleweka, si lazima nimalizie kabisa CHADEMA, coz chama ni kimoja tu Tanzania, hivo vingne ni megenge tu ya mafisadi na wala posho)
 
Pamoja na hayo. Ni picha mbaya ambayo itamuandama mjwahuzi (mpiga picha) hadi atajisikia vibaya. Zaidi ya huyo dada aliyetapika. Mujwahuzi ni mwanahabari asiye na maadili ya kazi wala mipaka ya kiutendaji na maamuzi. Hata huyo mhariri wa gazeti naye ana kasoro. Mbona huu ni udhalilishaji? Kuna suala la umri, maradhi, majukumu, pamoja na kukabiliana na tusiyoyajua kesho. Sasa huyu mwandishi hayaoni haya. Familia yake inajisikiaje? Nasema tena, huu ni udhalilishaji na matumizi mabaya ya maamuzi
 
Pamoja na hayo. Ni picha mbaya ambayo itamuandama mjwahuzi (mpiga picha) hadi atajisikia vibaya. Zaidi ya huyo dada aliyetapika. Mujwahuzi ni mwanahabari asiye na maadili ya kazi wala mipaka ya kiutendaji na maamuzi. Hata huyo mhariri wa gazeti naye ana kasoro. Mbona huu ni udhalilishaji? Kuna suala la umri, maradhi, majukumu, pamoja na kukabiliana na tusiyoyajua kesho. Sasa huyu mwandishi hayaoni haya. Familia yake inajisikiaje? Nasema tena, huu ni udhalilishaji na matumizi mabaya ya maamuzi
Aliyeileta humu JF ndiye mbaya zaidi. Kwenye gazeti denda hili halionekani vizuri kwa kiwango hiki.
 
Back
Top Bottom