Mrema na Cheyo waomba CHADEMA ifutwe

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
Wadau jana mwenyekiti wa TLP Augustine Mrema na mwenyekiti wa UDP John Cheyo waliishambulia CHADEMA kwa maneno unayoweza kufananisha na matusi. Eti Mrema ameshauri CHADEMA ifutwe kwa sababu wanataka kuleta vita. Cheyo naye amesema CHADEMA wanataka kuleta mambo ya Libya na Misri.

Hivi kweli hawa ni wapinzani? Na kwanini wote wazungumze lugha moja kwa wakati mmoja. Imetokea kwa bahati mbaya? Eti Mrema anadai CHADEMA hawana uchungu na taifa hili na wanatumiwa na mataifa ya nje...
 
Wana haki ya kutoa maoni, japo ni kosa sana kutumia haki hiyo kwa kitu cha kitoto, hawa ni viongozi wa upinzani na inawauma sana kuona kwamba wananchi wanawadharau kutokana na kushindwa kabisa kui-challenge serikali.
 
Waache waifute ndipo watagundua kuwa watanzania wa leo sio mabwege tena. Wataikaribisha hali ya Libya mlangoni mwetu kwa spidi kubwa ya ajabu wakijaribu kufanya hivyo. Wanaweza kutuua kwa risasi za moto wafuasi wa CHADEMA wote lakini matokeo ya kufanya hivyo bado yatafanya wasifurahie maisha tena hasa ukizingatia muundo wa jamii za taifa letu ulivyo.
 
Umri mkuu ndo unawasumbua, hawawezi kufikiri tena. acha waendelee kuijenga cdm manake wanayoyasema kwa cdm cyo ya kweli!
 
..nafikiri ufike wakati, watanzania wapenda maendeleo ya nchi hii wawatambue viongozi wa TLP, CUF, NCCR-Mageuzi nk kwamba wote wanaganga njaa!!! wanatoa matamko kutegemea na maelekezo ya kina makamba.
 
Cheyo ndiyo m/kiti wa chama chake na ndiyo mbunge pekee wa chama chake. Hivyo hivyo kwa Lyatonga. Hawana cha kuongea. Mrema amesahau alipokuwa kwenye chati miaka ya 1995, aliweza kuzunguka nchi nzima.

Ndugu yangu "mzee wa mapesa" wa wakati huo, ajitahidi kuimarisha chama angalau kipate kufika hata Kigoma, Tanga na hata Shinyanga mjini. Aachane na chadema.

Alivyomtukana Tundu Lissu bungeni siku ile amesahau kwamba ule ni uchochezi. Huwezi kumwambia Mh Mbunge mwenzako eti :"Shut up"!! ndani ya Bunge, wananchi wa Bariadi hawajakutuma kutukana wenzako. Kwani alisema uongo kwamba chama chako kina mbunge mmoja.

Cheyo na Mrema msiogope vivuli vyenu, fanyeni kazi mliyotumwa na wapiga kura wenu, kama CDM wanvyofanya. Halafu kama mtu huna hoja, kukaa kimya kunaleta maana.
 
Wazee wale tuwasamehe!wanaganga njaa!hii movement ya sasa tena wakisikia itakua tz nzima wana ccm wanakosa usingizi kabisa!kwa sasa inatafutwa njia ya kuzuia maandamano bahati nzuri maandamano ni ya wananchi kwa ajili ya kudai haki za msingi ktk nchi yetu!hayana vurugu bali roho zinawasuta hao watawala miaka 50 nchi haina muelekeo wa ajira,elimu,afya,miundombinu,kilimo,masoko ya mazao,huduma mbovu ktk sekta ya umma haswa ardhi,polisi,mahakama.hembu fikiri makinda eti anasema mitihani ya mchujo form 4 irudiwe hiyo ni akili au?wenye migodi watoe umeme 50mw wawape tanesco huku ni kutuona hatuna akili rais mpaka leo anawaza mitambo ya kukodi
 
CCM wanatumia mbinu za kizamani sana kufikiri kuwa kuwanunua Cheyo na Mrema itatoa picha kuwa wapinzani wapo nao. Hawajui tumeshajua hao ni maajenti wao?

Walifikiri wakichakachua kura na kuwa wengi bungeni watapata likizo ya kula shushu kwa miaka mitano ijayo. Sasa wanaona hakuna kulala wananchi wamepata wa kuwazungumzia na awareness inkua kubwa.
 
Naomba maandamano yanayofuata yafanyike jimbo la Vunjo na Bariadi wapiga kura wa hao waganga njaa waelezwe makosa waliyo fanya kuwachagua wachovu namna hiyo kwenda kuwawakilisha.
 
Maskini Mrema.
Juzijuzi hapa alisema hayo madai ya Chadema ya katiba mpya aliyaanzisha yeye, leo anakuja na tuhuma kwamba chadema wanataka kupingua nchi! Kasahau kwamba na yeye alishawahi kuhojiwa na polisi akiwa NCCR Mageuzi kwa madai kama ya chadema? Zama zake zimepita, akae kimya!
 
Tuwapuuze mzee upara na huyo Lyatonga; Natapata tabu sana kumuelewa mzee upara akiongea kwani anavunja maneno sanaaaaaaaaaaa!!!!! Huyo lyatonga nadhani diabates zinamsumbua na moja ya indicators za ugonjwa huu ni kuongea pumba!!
 
Nimejaribu kutafakari movement zinazofanywa nachadema namaneno yanayotamkwa na wapinzani wenzao pamoja na serikali,kuwa chadema niwachochez.
Kwa upande wangu sikubaliani nao wanaosema hivyo ila kinachofanyika sasa ni wakati ndio unaongea, bahati mbaya hata chadema wakikaa kimya watu wataendelea kuandamana hata mioyoni mwao na ipo siku watatafuta njia mbadala.Siasa za fitna hazina nafasi ktk wakati tulionao zaidi yakusema ukweli(kijiko kiitwe kijiko) , kukifuta CHADEMA kwa sasa ni sawa nakuwaambia watu ingieni mitaani mana hakutakuwa na mtu wakuwazuia. Sina hakika kama viongozi wetu wa serikali na nccr,tlp,udp wanajua watu wanawaza nini juu yao au juu ya mustakabali wa maisha yao ya kesho, uhalisia watu wamekata tamaa zamani juu ya viongozi wao, nasema muda utatuambia wala si mbali.
 
Maskini Mrema.
Juzijuzi hapa alisema hayo madai ya Chadema ya katiba mpya aliyaanzisha yeye, leo anakuja na tuhuma kwamba chadema wanataka kupingua nchi! Kasahau kwamba na yeye alishawahi kuhojiwa na polisi akiwa NCCR Mageuzi kwa madai kama ya chadema? Zama zake zimepita, akae kimya!

Mrema ni Mtu wa kale aliyepitwa na wakati,hiki ni kizazi kipya na ulimwengu wa Technohama ulimwengu unakimbia kwa kasi sana Mrema,wewe huwezi enzi zako zilipita na laana uliyopewa na Mwalimu Bado inakuandama! Ndiyo maana hata ulipojipendekeza kwa CCM Dodoma walikukejeli tu.
 
Mbona wenzao wakizeeka wanakuwa na busara?Hawa wanazeeka vibaya au CCM wameshachezea bongo zao.
 
Back
Top Bottom