Mrema alilia posho ya kustaafu

Dingswayo

JF-Expert Member
May 26, 2009
4,019
2,923
[FONT=ArialMT, sans-serif]Mbunge wa Vunjo (TLP), Augustine Mrema, ametoa malalamiko bungeni akiitaka serikali kumlipa posho zake za kustaafu cheo cha Naibu Waziri Mkuu alichopewa na Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi katika miaka 1990.[/FONT]

[FONT=ArialMT, sans-serif]Mrema, alitoa malalamiko hayo alipokuwa akichangia mjadala wa bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, bungeni, mjini hapa jana.[/FONT]

[FONT=ArialMT, sans-serif]Alisema ili aweze kuwa mdau mzuri wa kutetea amani ya Tanzania ana kila sababu ya kulipwa stahiki zake kutokana kuwa na cheo hicho.[/FONT]
“[FONT=ArialMT, sans-serif]Asilimia 80 ya mafao yako, nipeni basi hata asilimia 20,” alisema Mrema na kusababisha karibu ukumbi mzima wa Bunge kulipuka kwa kicheko. [/FONT]

[FONT=ArialMT, sans-serif]Alisema kuna hoja zinazojaribu kutolewa kutaka kuzuia apewe stahiki yake hiyo kwamba, cheo cha Naibu Waziri Mkuu alichopewa na Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi, hakimo kwenye Katiba ya nchi.[/FONT]

[FONT=ArialMT, sans-serif]Mrema, ambaye amewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani sambamba na cheo hicho na baadaye Waziri wa Kazi na Maendeleo ya Vijana katika serikali ya awamu ya pili ya Mwinyi, alisema anavyofahamu ni kwamba, Rais ndiye anayeanzisha cheo hivyo, hoja za watu hao hazina msingi.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]
Alisema anashangaa kuona posho za majenerali wa jeshi zinapojaribu kuguswa kunakuwa ‘hapakaliki’ na kuhoji “Kwanini Mrema mkimnyima mnaona sawasawa?”. [/FONT]

“[FONT=ArialMT, sans-serif]Msije mkaona Simba amenyeshewa mkafikiri nyani. Nyinyi mmenifundisha mambo mengi najua vitu vingi. Sasa kwanini haki zangu hamnipi?” alisema Mrema.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Aliongeza: “Kwa hiyo, naomba serikali hii na hasa Waziri Mkuu ili niendelee kutetea mambo mengi ya nchi hii, naomba haki yangu mnipe.”[/FONT]

CHANZO: NIPASHE
 
Si mnakumbuka aliwahi kusomewa itqaf wakati fulani huyu chizi fresh? Basi sasa ndiyo yametimia.
 
Hao ndiyo viongozi wa kitanzania. Maslahi ya wana Vunjo mbona hayapigii debe? Maslahi ya watanzania hawataki kuyasikiliza, wabunge wa CDM wakidai kwa niaba ya wananchi wanawabeza na kusema wanayamezea mate. Wamejaza mawazo ya maslahi yao binafsi. Inasikitisha sana!!!
 
Si mnakumbuka aliwahi kusomewa itqaf wakati fulani huyu chizi fresh? Basi sasa ndiyo yametimia.

Hahahaha mkuu umeniacha hoi sana, kuna siku nilikuwa naongea na mzee mmoja kuhusu afya na hali ya mrema hakunichelewesha alinipa jibu moja tu nikabaki mdomo wazi kisha baadae nikakauka kucheka, aliniambia "KUNUTI HIYO", kwa waumini wa kiislam ukiwatajia dua ya KUNUTI wanaijua madhara yake, yaani ni dua ya kumshitakia mwenyezi mungu na kwa wakati huo wale masheikh wa zamani waliosoma dini wanakwambia kama una jambo na unataka kusoma dua hiyo sharti utangaze mwezi mzima kuwa una nia ya kusoma kama kuna mtu amefanya jambo either kaiba au kafanya jambo baya kiuficho ajitokeze. Walikuwa wakiisoma hiyo dua muhusika lazima alipuke, watu walikuwa wanaogopa kuiba misikitini kwa kuhofia dua hiyo. Ila siku hizi imani imepungua masheikh wamekuwa wanasiasa na propaganda sana ndiyo maana hawasikilizwi maombi yao. Si dhani mtu kama Sheikh mkuu wa kwanza Hemed bin Jumaa bin Hemed angekubali leo hii kuwa vuvuzela la wanasiasa.
 
[FONT=ArialMT, sans-serif]Mbunge wa Vunjo (TLP), Augustine Mrema, ametoa malalamiko bungeni akiitaka serikali kumlipa posho zake za kustaafu cheo cha Naibu Waziri Mkuu alichopewa na Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi katika miaka 1990.[/FONT] [FONT=ArialMT, sans-serif]Mrema, alitoa malalamiko hayo alipokuwa akichangia mjadala wa bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, bungeni, mjini hapa jana.[/FONT] [FONT=ArialMT, sans-serif]Alisema ili aweze kuwa mdau mzuri wa kutetea amani ya Tanzania ana kila sababu ya kulipwa stahiki zake kutokana kuwa na cheo hicho.[/FONT] [FONT=ArialMT, sans-serif]Asilimia 80 ya mafao yako, nipeni basi hata asilimia 20, alisema Mrema na kusababisha karibu ukumbi mzima wa Bunge kulipuka kwa kicheko. [/FONT] [FONT=ArialMT, sans-serif]Alisema kuna hoja zinazojaribu kutolewa kutaka kuzuia apewe stahiki yake hiyo kwamba, cheo cha Naibu Waziri Mkuu alichopewa na Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi, hakimo kwenye Katiba ya nchi.[/FONT] [FONT=ArialMT, sans-serif]Mrema, ambaye amewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani sambamba na cheo hicho na baadaye Waziri wa Kazi na Maendeleo ya Vijana katika serikali ya awamu ya pili ya Mwinyi, alisema anavyofahamu ni kwamba, Rais ndiye anayeanzisha cheo hivyo, hoja za watu hao hazina msingi.[/FONT] [FONT=ArialMT, sans-serif]Alisema anashangaa kuona posho za majenerali wa jeshi zinapojaribu kuguswa kunakuwa hapakaliki na kuhoji Kwanini Mrema mkimnyima mnaona sawasawa?. [/FONT] [FONT=ArialMT, sans-serif]Msije mkaona Simba amenyeshewa mkafikiri nyani. Nyinyi mmenifundisha mambo mengi najua vitu vingi. Sasa kwanini haki zangu hamnipi? alisema Mrema.[/FONT] [FONT=ArialMT, sans-serif]Aliongeza: Kwa hiyo, naomba serikali hii na hasa Waziri Mkuu ili niendelee kutetea mambo mengi ya nchi hii, naomba haki yangu mnipe.[/FONT] CHANZO: NIPASHE
Hicho cheo alichopewa kilikuwa cha bandia. Sikumbuki kuwahi kukisoma kwenye Katiba.
 
Back
Top Bottom