Safari_ni_Safari
JF-Expert Member
- Oct 5, 2007
- 23,268
- 17,097
BAADA ya kulia na propaganda chafu za Chadema, mgombea ubunge katika Jimbo la Vunjo kwa tiketi ya TLP, Augustino Mrema, amesema anapanga kujibu mapigo kwa kuhamishia nguvu zake katika majimbo matatu ambako Chadema wana matumaini ya ushindi.
Amesisitiza kwamba, haendi kwa bahati mbaya, bali kuwavurugia kama chama hicho kinavyomtibulia mipango yake ya kuingia bungeni, baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31.
Mrema alisema hayo jana kwenye Viwanja vya Majengo Sokoni, mjini hapa, wakati akimnadi mgombea ubunge wa TLP Moshi Mjini, Godfrey Malisa.
Alisema kutokana na kufanyiwa siasa chafu na Chadema, sasa chama chake kitahakikisha kinaelekeza nguvu Hai (Freeman Mbowe), Moshi Mjini (Philemon Ndesamburo) na Vunjo (John Mrema).
Mrema alisema madhumuni ya kuelekeza nguvu katika majimbo hayo, ni kutokana na alichokiita upinzani wa kinafiki unaofanywa na Chadema, ambapo alisema kauli ya Chadema kuwa Mrema atakwenda kufia bungeni, ni matusi huku akisisitiza kwamba hakuna mtu asiyekufa na kutaka aachwe akafie huko.
Aliwaonya mgombea urais wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa, Mwenyekiti Mbowe na Ndesamburo kutokanyaga jimbo la Vunjo.
Alisema wakikaidi, waende kistaarabu, lakini wakiendelea kumchezea rafu za kisiasa, atahakikisha kati yao hakuna anayeshinda katika uchaguzi mkuu, kwani atafanya kampeni za nguvu kuhakikisha anagawa kura za Hai na Moshi Mjini.
Kama wao wanadai kuwa mimi ni mzee eti niwaachie vijana, sasa mimi niulize kati ya Kikwete na Dk. Slaa, nani mzee?... inatakiwa Slaa amwachie Kikwete uongozi, kama Slaa anataka kwenda Ikulu atafia huko nami nifie bungeni, mbona kuna wabunge wanafia humo?
Kama Chadema inavyogawa kura zangu Vunjo, vivyohivyo nami nitahakikisha Mbowe, Mrema na Ndesamburo, hawanusi Bunge nitafanya kampeni kubwa katika majimbo yao, kuhakikisha TLP inakuwa na wapiga kura wengi, ili kuzuia ushindi wanaotarajia Chadema, nitahakikisha hadi kinaeleweka, alisema Mrema.
Alisema anashangazwa na upinzani uliopo sasa miongoni mwa vyama vya upinzani, kwani havijalenga kuchukua madaraka ya nchi, bali kushambuliana, jambo linalozidi kuvidhoofisha na kuiacha CCM ikitamba.
Malisa, alisema kwa miaka 10 sasa Chadema imeongoza jimbo hilo, lakini hakuna mabadiliko yoyote yaliyopatikana zaidi ya wananchi kubaki mashabiki wa chama hicho.
Alisema tatizo la wananchi wa Moshi ni kudanganywa na gari la kubebea wagojwa la Hospitali ya Mkoa, Mawenzi, ambalo lilitolewa na Ndesamburo, ambalo kwa sasa alidai ni bovu na halijafanyiwa matengenezo.
Pia aliwataka wananchi wa jimbo hilo kumchagua, akisema akipewa ridhaa atahakikisha viwanda vilivyoshindikana kufufuliwa na Chadema vinafufuliwa, ili kutoa ajira kwa wakazi wa Moshi.
Source: Habari Leo
Amesisitiza kwamba, haendi kwa bahati mbaya, bali kuwavurugia kama chama hicho kinavyomtibulia mipango yake ya kuingia bungeni, baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31.
Mrema alisema hayo jana kwenye Viwanja vya Majengo Sokoni, mjini hapa, wakati akimnadi mgombea ubunge wa TLP Moshi Mjini, Godfrey Malisa.
Alisema kutokana na kufanyiwa siasa chafu na Chadema, sasa chama chake kitahakikisha kinaelekeza nguvu Hai (Freeman Mbowe), Moshi Mjini (Philemon Ndesamburo) na Vunjo (John Mrema).
Mrema alisema madhumuni ya kuelekeza nguvu katika majimbo hayo, ni kutokana na alichokiita upinzani wa kinafiki unaofanywa na Chadema, ambapo alisema kauli ya Chadema kuwa Mrema atakwenda kufia bungeni, ni matusi huku akisisitiza kwamba hakuna mtu asiyekufa na kutaka aachwe akafie huko.
Aliwaonya mgombea urais wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa, Mwenyekiti Mbowe na Ndesamburo kutokanyaga jimbo la Vunjo.
Alisema wakikaidi, waende kistaarabu, lakini wakiendelea kumchezea rafu za kisiasa, atahakikisha kati yao hakuna anayeshinda katika uchaguzi mkuu, kwani atafanya kampeni za nguvu kuhakikisha anagawa kura za Hai na Moshi Mjini.
Kama wao wanadai kuwa mimi ni mzee eti niwaachie vijana, sasa mimi niulize kati ya Kikwete na Dk. Slaa, nani mzee?... inatakiwa Slaa amwachie Kikwete uongozi, kama Slaa anataka kwenda Ikulu atafia huko nami nifie bungeni, mbona kuna wabunge wanafia humo?
Kama Chadema inavyogawa kura zangu Vunjo, vivyohivyo nami nitahakikisha Mbowe, Mrema na Ndesamburo, hawanusi Bunge nitafanya kampeni kubwa katika majimbo yao, kuhakikisha TLP inakuwa na wapiga kura wengi, ili kuzuia ushindi wanaotarajia Chadema, nitahakikisha hadi kinaeleweka, alisema Mrema.
Alisema anashangazwa na upinzani uliopo sasa miongoni mwa vyama vya upinzani, kwani havijalenga kuchukua madaraka ya nchi, bali kushambuliana, jambo linalozidi kuvidhoofisha na kuiacha CCM ikitamba.
Malisa, alisema kwa miaka 10 sasa Chadema imeongoza jimbo hilo, lakini hakuna mabadiliko yoyote yaliyopatikana zaidi ya wananchi kubaki mashabiki wa chama hicho.
Alisema tatizo la wananchi wa Moshi ni kudanganywa na gari la kubebea wagojwa la Hospitali ya Mkoa, Mawenzi, ambalo lilitolewa na Ndesamburo, ambalo kwa sasa alidai ni bovu na halijafanyiwa matengenezo.
Pia aliwataka wananchi wa jimbo hilo kumchagua, akisema akipewa ridhaa atahakikisha viwanda vilivyoshindikana kufufuliwa na Chadema vinafufuliwa, ili kutoa ajira kwa wakazi wa Moshi.
Source: Habari Leo