Mrejesho kuhusu Uwakilishi Wangu katika Mkutano wa pili wa Bunge

mh. John Mnyika, hongera sana.

napenda kukiri kuwa wewe ni mmoja wa wanachadema walio hazina kubwa sana kwa chadema yenyewe na Tanzania kwa ujumla. nafurahishwa sana na umakini wa hoja zako na ujasiri wa hali ya juu unaoambatana na busara ambayo kwa kweli sikuitegemea kutoka kwa kijana wa umri wako na uzoefu wako wa masuala ya bunge. kwa kweli unawashinda kwa mabli wabunge chungu mzima baadhi yao wakiwemo waliokaa bungeni kwa miongo kadhaa. hongera sana mheshimiwa.

pia nimeguswa na aina hii ya uwajibikaji kwa wapiga kura na washabiki wako. yaani hapa umeweka changamoto kwetu sote juu ya kiwango cha uwazi na hulka anayopaswa kuwa nayo mbunge atokanaye na jimbo la uchaguzi kwa wapiga kura wake. ni dhahiri kabisa sasa kuwa wapiga kura wa jimbo la ubungo hawakukosea kukuchagua kwa kura nyingi kuwa mbunge wao. walau sasa wana mwakilishi aliye sauti yao bungeni na mtoto wao arudiye kutoa taarifa kwa kazi aliyotumwa.

mwisho nakuahidi kuwa, kama mmoja wa wabunge wapya wa CCM lakini mwenye ari kuuna uthubutu wa mabadiliko, nitajitahidi tufahamiane kibinafsi ili tuweze kubadilishana mawazo na mikakakti kwa karibu zaidi kwa manufaa ya wananchi wa majimbo yetu tunayowakilisha. mimi japo natokana na CCM ila kwangu taifa ndilo la kwanza kabisa na mamabo mengine yanafuata. wakati mwingine ushabiki husaidia kutawala siasa lakini si mara zote huwa na tija kwa taifa. mfano sasa ni dhahiri kuwa tunapata tabu sana kwa sasa kueleweka na wanachi pale tunapoonyesha mshikamano wa kichama kwa mambo mbalimbali kuliko wakati mwingine wowote. hiii inatokana na ukweli kuwa siasa zetu zimebadilika na wanachi wetu nao wamebadilika. kwa msingi huu ni lazima kujinasua na mtego wa u-chama katika masuala yenye manufaa kwa taifa ili angalau wanachi waendelee kutuamini.

tuko pamoja mkuu. nakutakia kila la heri

MUNGU IBARIKI TANZANIA
MUNGU IBARIKI AFRIKA
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI

Nashawishika kukupongeza. Natamani mtazamo huu ungekuwa wa wabunge wote wa chama chako. Hata hivyo naomba unisamehe nikikuuliza. Ulikuwa wapi siku ile chama chako kilipoungana kubadili kanuni za bunge kuhusu tafsiri ya kambi rasmi? Mbona sikusikia mtu yeyote wa CCM aliyeona hoja hiyo kama ni mwendelezo wa uchakachuaji? Nisamehe kwa swali hili, otherwise naheshimu mawazo yako.
 
Mnyika nakukubali. Ila siamini sana vijana manake unaweza ukabadilika ukawa sawa na yule kijana wetu wa Kigoma. Yule bwana kama mnaweza mtimueni tu maana hata ubunge wake hauna faida kabisa anatujazia impurities tu kwenye chama
 
Nawashukuru sana kwa ushauri na hata ukosoaji. Naamini yote ni katika kuboresha uwakilishi kwenye vyombo vya maamuzi.

Kuna machache baadhi mmenitaka niyajibu:

Mosi, suala la 'mkopo' wa milioni 90 za magari kwa wabunge. Fedha hizi bado sijapatiwa, lakini mimi kama mbunge wa Ubungo sihitaji kuwa na gharama kubwa kiasi hicho. Kukaa kwangu bungeni kwa siku chache kumedhihirisha tofauti kubwa ya kimaslahi baina ya watumishi wa umma wa kada nyingine na viongozi wa umma. Zipo hatua ambazo nimechukua na nitaendelea kuchukua kuhusu suala hili.

Pili, suala la 'udini'- ni kwa bahati mbaya sikuwa na muda wa kutosha kueleza zaidi lakini mimi kwa maoni yangu, wapo viongozi wanaotumia kivuli cha udini kuficha udhaifu wao wa kiuongozi na kufunika mijadala ya msingi ya kitaifa. Kadiri tunavyoachia viongozi wa namna hii wakafanya hivyo wafanyavyo tunaweza tukajikuta tunaruhusu mbegu ya udini ikapandwa zaidi. Nilisema vyombo vya usalama vishauri viongozi wetu, sio kwa sababu tu ya hotuba ya Rais bungeni, bali kuna kauli nyingi za kabla, wakati na baada ya kampeni zinazodhihirisha haja hiyo. Naamini kwamba masuala haya yangeweza kushughulikiwa kwa kadiri yalivyoanza kujitokeza kwa hatua za kiusalama na kiuongozi badala ya kupigiwa baragumu.

Tatu, suala la kuwasilisha miswada na mapendekezo ya kisera; ni wazo ninalo likubali ila izingatiwe kwamba kikao hiki ni cha pili, suala kubwa ambalo nilitarajia kuliwasilisha katika kikao hiki ni la hoja ya katiba mpya. Katika vikao vijavyo itarajiwe miswada, maelezo, hoja nk na pia mchango katika ile itayowasilishwa na serikali na wengine. Ningependa kupata pia mapendekezo kutoka kwenu yapi niyape kipaumbele zaidi pamoja na kuwa ninayo mawazo yangu tayari kuhusu masuala kadhaa nitayoyasukuma katika mikutano ijayo ya bunge.

Nne; kuna wengine wametaja kwamba sijagusa masuala mengine kama barabara za mitaani, kuingia kiundani kuhusu maji nk. Ieleweke tu kwamba hapa niligusia mchango wangu katika kikao husika cha bunge, sijazungumzia kazi zingine za utumishi wa umma na ufuatiliaji wa kushughulikia kero za wananchi ninazozifanya kila siku jimboni na kupitia vyombo vingine vya maamuzi ambavyo mimi ni mjumbe mathalani bodi ya barabara na baraza la madiwani. Katika hatua ya sasa niliona nitoe mrejesho kuhusu masuala mahususi ya kibunge; hata hivyo kila mwaka nitakuwa natoa taarifa ya utekelezaji wa ahadi ambayo itajikita katika sekta zote na wajibu nilioutimiza katika vyombo vyote ambavyo nawakilisha umma; kuhusu maji baadhi ya masuala tuyayoyapa kipaumbele mengine yalitajwa kwenye Kongamano la Maji nililoitisha; rasimu ya taarifa yake kwa ufupi iko hapa: JOHN MNYIKA: RIPOTI YA KONGAMANO LA MAJI JIMBO LA UBUNGO TAREHE 31.01.2010 Ripoti ya Kina ya Kongamano husika bado inakamilishwa. Tutaisambaza kwa wadau wote na kufuatilia utekelezaji wake hatua kwa hatua.

Naombeni tuendelee kushauriana na kushirikiana, na nawashukuru sana kwa pongezi zenu na kunipa moyo

JJ
 
Nawashukuru sana kwa ushauri na hata Pili, suala la 'udini'- ni kwa bahati mbaya sikuwa na muda wa kutosha kueleza zaidi lakini mimi kwa maoni yangu, wapo viongozi wanaotumia kivuli cha udini kuficha udhaifu wao wa kiuongozi na kufunika mijadala ya msingi ya kitaifa. Kadiri tunavyoachia viongozi wa namna hii wakafanya hivyo wafanyavyo tunaweza tukajikuta tunaruhusu mbegu ya udini ikapandwa zaidi. Nilisema vyombo vya usalama vishauri viongozi wetu, sio kwa sababu tu ya hotuba ya Rais bungeni, bali kuna kauli nyingi za kabla, wakati na baada ya kampeni zinazodhihirisha haja hiyo. Naamini kwamba masuala haya yangeweza kushughulikiwa kwa kadiri yalivyoanza kujitokeza kwa hatua za kiusalama na kiuongozi badala ya kupigiwa baragumu.
Mheshimiwa Mbunge, Ahsante sana kwa kutoa maoni yako kuhusiana na hili suala la Udini. Bila shaka kama wewe ni mfuatiliaji mzuri wa historia na siasa za Tanzania kumekuwepo na shutuma na minong'ono mingi sana kuhusiana na udini nchini Tanzania, shutuma hizi wala hazikuanza kipindi cha uchaguzi mkuu uliopita tu, bali zimekuwepo kwa muda mrefu sana.Lipo kundi kubwa sana la wananchi Wanaodhani kwamba kuna mfumo unaowabagua katika nyanja mbalimbali tokea uhuru mpaka sasa, Mimi binafsi sina Ushahidi wa Malalamiko yao, lakini UKWELI NI KWAMBA WAO WANAFIKIRI HIVYO NA WANAAMINI HIVYO. na hali hii ni hatari kwa usalama na Amani ya nchi yetu.Sasa Mheshimiwa Mbunge kufuatia malalamiko hayo ya hao ya sehemu ya wananchi wetu, Unampango gani kuhakikisha Ukweli unawekwa bayana ili kama kweli kuna Ubaguzi FORMAL au INFORMAL basi unaondoshwa na wenye kuhusika nao wanafikishwa katika vyombo vya sheria, lau kama Huo ubaguzi haupo basi Ukweli uwekwe wazi na watu waelimishwe?. kwa maoni yangu DENIAL IS NOT AN OPTION, BALI TRUTH PEKEE NDO ITAONDOA MZIZI HUU WA UDINI NCHINI. AHSANTE
 
Barua ndefu. Tukifanya impact evaluation hapa, hakuna kitu. Chifu, try to accomplish things. And not reiteriating what we have already seen kwenye vikao vya bunge. Come up with ideas and have balls to work with "mafisadi" if you think the cause is worthy it.

And be independent for a minute. Wadau mtaani wanadai whatever Mbowe/Slaa says--John Mnyika doesn't even question it, anatekeleza tu.

....kweli akili zako zinaendana na ufupi wako mkuu! hujayaacha ya Pugu bado tu?
 
Well done John, I wish we had 30MPs of your type! Next Bunge try to do even better. Tumechoka na jinsi nchi hii inavyoendeshwa kibabaishaji! Serikali inaomba bajeti kwa ajili ya matumizi yake halafu katikati wanachukua 79% kutoka idara na wizara zote eti ni kwa ajili ya dharura! Wanawafanya Wabunge muonekane rubber stampers! Hizo hela zinatumika kwa matumizi yasiyo ya lazima na inawezekana nyingi zinaenda mifukoni mwa wajanja!
 
Big Up mheshimiwa, analysis yako ni nzuriiiii saaana! ila naomba tuu uweke ku impart your fellow CDM Mps' waweze pia kutoa tathmini kama yako pindi wanapomaliza vikao vya bunge!! hayo madongo hapo juu uyachukulie kwa kiasi but u did a good job, we have seen it!! Big up
 
Afu next time give the public nafasi kama hii!! i mean online contributions!, it will be the true representation of the people!! Keep it up
 
Kazi nzuri sana. Nadhani huu utaratibu wako wa kutoa update wa yaliyojiri ni mzuri sana maana unasaidia watu kutafakari na hata kutoa ushauri pale penye mapungufu. Kazi nzuri niko pamoja nawe.
 
Ahsante Mh Mnyika kwa majibu yako mazuri kwa baadhi ya maswali yetu hapa JF. Kwa mwanasiasa makini kama wewe hauwezi kuchoka kuitumia JF kupanua na kujiongezea maarifa ili kukabiliana vema zaidi na majukumu yako ya sasa na baadae. Mwenzako Zitto ana "hasira" kidogo. Siku za hivi karibuni amekuwa akipita tu humu na kuchangia kidogo tena kwa yale yanayomgusa tu. Sijui alidhani humu ni kushangiliana tu kama majukwaa mengine ya kisiasa.
Nisaidie kufahamu machache yafuatayo:
- Ofisi yako ya Ubunge iko wapi?
-Muda gani mzuri kwako kuonana na watu wa kawaida kama mimi kwa maongezi na kubadilishana hili na lile.
Ni nini maoni yako juu ya ukubwa wa Bunge letu? Kwa maoni na mtazamo wangu Bunge letu la sasa ni kubwa sana kuliendesha kwa uchumi na nyenzo tulizonazo na kila kukicha majimbo yanaongezwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa vigezo vya hovyo kabisa. Wakati wewe unachaguliwa na watu zaidi ya 50000 mwenzako wa Mchambawima ambako pia kuna Mwakilishi anachaguliwa kwa kura 2000 tu. Tuna viti MAALUM vingi mno. Kwa nini kila Halmashauri/ Manispaa/Mji usingekuwa Mbunge mmoja tu wa kuchaguliwa?
Tumejenga majengo mapya ya Bunge mawili tangu uhuru kwa gharama kubwa sana. Jirani zetu hapa Kenya wamo kwenye mjengo uleule kama Karimjee yetu ya zamani. Nasikia sasa mnataka kujengewa nyumba zaidi ya 350. Tunaigharamia sana siasa wakati chaguzi zenyewe ni za hovyo kabisa.
 
Dear Mnyika,

Its a good approach to people representation in the house. I am doing just about the same, but back in Nzega to the people who sent me there. Next time I am also gonna post it in the social networks and share it with fellow Tanzanians. I commend you for your efforts as a responsible young statesman. You should also do the same before you go to Dodoma next time for a session, I did it before the last session. people were really contented with this approach. Its time and resource consuming but worth doing.

Best regards,
HK.
 
Barua ndefu. Tukifanya impact evaluation hapa, hakuna kitu. Chifu, try to accomplish things. And not reiteriating what we have already seen kwenye vikao vya bunge. Come up with ideas and have balls to work with "mafisadi" if you think the cause is worthy it.

And be independent for a minute. Wadau mtaani wanadai whatever Mbowe/Slaa says--John Mnyika doesn't even question it, anatekeleza tu.

Peke yako na "fake comments" za kwako... daah pole saana hongera zimezidi uzito ujumbe wako nimeona mimi peke yangu... Nashukuru peke yangu nimeamua kukupa pole..

BIG UP JJ MNYIKA
WE LOVE U
 
Back
Top Bottom