Mramba na Yona, Wakabidhiwa vifaa vya usafi Hospitali ya Palestina

Hii nchi ukiifikiria sana unasikia kichefu chefu,angalia hao mawaziri wanaonyesha kama waliwahi kukaa jela?Mramba ana kitambi kabisa.
 
wao waliiba wakaacha traces,wamuulize chenge huwa anafanya nini mpaka hatiwi hatiani?joka lenye mabichwa saba
 
Rais wangu mpendwa narudia tena kwa mara nyingine, HUU SIO MUDA WA SHERIA TENA, huu ni muda wa ubabe, na ukatiri mwingi taifa likae sawa kwa manufaa ya vizazi na vizazi,, "ONA SASA MH RAIS WANGU MAGUFURI WALE JAMAA ETI WANAFAGIA HOSPITALI PALE PALESTINA,." watu wamelitia taifa hasara kubwa ambayo itachukua miaka mingi na vifo vingi kuifidia, hawa watu wameacha familia nyingi kwenye umasikini huku familia zao zikila maisha ndani na nje ya Tanzania, mh Rais wangu ni muda sasa wa familia za hawa watu kulia na kusaga meno... FILISI,UA au FUNGA JELA VIFUNGO VIREFU HAO WATU .... kama ni rahisi tu hivyo unafikiri nani ataogopa kulitia hasara taifa ili aende akafagie pale Mwananyamala????

MH RAIS WANGU MPENDWA NILIKUPIGANIA KWA NGUVU ZANGU ZOTE HUKU MITAANI NIKIWAAMINISHA WATU "YES, YOU ARE THE MAN" fanya kweli usituangushe sio dhambi kuua,kutesa na kufunga wezi wa mali za umma..
 
Mawaziri wa zamani Basil Mramba na Daniel Yona wameripoti katika hospitali ya Sinza Palestina na kukabiziwa vifaa kwa ajili ya kufanya usafi.

img-20160208-wa0013-jpg.321837


yona-png.321844

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu iliridhia waliokuwa Mawaziri wastaafu Basil Mramba na Daniel Yona kutumikia adhabu ya kifungo cha nje kwa kufanya usafi katika maeneo ya kijamii ikiwemo Hospitali ya Sinza Palestina.

Hatua hiyo inatokana na Mramba ambaye alikuwa Waziri wa Fedha na Yona aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, kupitia Mawakili wao kuwasilisha barua mahakamani hapo kutoka Magereza kuhusu kutumikia kifungo cha nje.

Mawaziri hao, Jul 6, 2015, walihukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela na kulipa faini ya Sh milioni tano, baada ya kupatikana na hatia ya matumizi mabaya ya madaraka na kuisababishia serikali hasara ya Sh bilioni 11.7.

Kwa mara ya kwanza washtakiwa hao walifikishwa mahakamani mwaka 2008, wakikabiliwa na mashtaka ya kuisababishia serikali hasara ya kiasi hicho cha fedha kutokana na kutoa msamaha wa kodi kwa Kampuni ya kukagua madini ya dhahabu ya M/S Alex Stewart ya Uingereza.

Hivi, Mafisadi Tanzania Ni Yonah na Mramba na Masamaki tuu? Pamoja na Kuwa siwaonei Huruma Mafisadi, Nachokiona hapa Kuna Mtu alikuwa na Kinyongo na hawa watu. Mimi Naamini Kama Akina Chenge na Kikwete na Wale wa Escrow hawako Lukaranga, basi hawa wanaonewa. Nisieleweke kuwa nawatetea!
 
Hawa Jamaa nasika wamefanya usafi pale palestina siku tatu tuu wakasepa kumbe île yote ilikuwa
Geresha tuuu..hii ndo Tanzania bana
 
Kumbe we ulijua pale watafanya kweli kama inavostahili? Wapumbavu wachache ndio wanaamini kuwa ccm ina nia ya dhati kupambana na mafisadi.. Embu ona watu waizi ila wamefungwa miaka 3 alafu usafi wenyewe siku 3
 
Kumbe we ulijua pale watafanya kweli kama inavostahili? Wapumbavu wachache ndio wanaamini kuwa ccm ina nia ya dhati kupambana na mafisadi.. Embu ona watu waizi ila wamefungwa miaka 3 alafu usafi wenyewe siku 3
Ngoja waliokunywa maji ya kijani waje utatukanwaje?
 
Kwani walitakiwa wafanye siku ngapi. Na kama wamesha ajiri watu wanafanya jee. Si sawa tuu. Kwani umekuta pachafu ??. Ukikuta pasafi ujuwe wamefanya. Hata hivyo kwani wale wa Escrow wao wanafanya wapi.
 
Ni sawa tu... Hawa hata kama walituibia walijenga uchumi imara enzi za Mkapa na ndio vilikuwa vyichwa vyake..

Hawa walioharibu uchumi wetu na ufisadi kutamalaki enzi za JK kuanzia Richmond mpaka Escrow mbona wanakula kuku tu mtaani?? Tena na matusi walitutukana kabisa...
 
Walikwenda pale kupata picha tuu Za Waandishi wa habari kazi ilikua hiyo tu ilitakiwa, si unajua wabongo ni wepesi kuwadanganya?

Sasa hivi watu wameshasahau kila kitu. Wako nyumbani wanakula Mabaki yao.
 
Cha muhimu je wamejifunza kitu kwa maana fedhea waliyoipata ni kubwa,kufanya usafi hata kama wangefanya mpka miaka 20,haisaidi kitu cha muhimu adhabu kama zilikuwa ni kuwarekebisha
 
Ni sawa tu... Hawa hata kama walituibia walijenga uchumi imara enzi za Mkapa na ndio vilikuwa vyichwa vyake..

Hawa walioharibu uchumi wetu na ufisadi kutamalaki enzi za JK kuanzia Richmond mpaka Escrow mbona wanakula kuku tu mtaani?? Tena na matusi walitutukana kabisa...
Enzi za Mkapa uchumi wetu ulikuwa imara...? Hivi tulirank wa ngapi kwa Umaskini? na usikute nawe unajiita msomi, ptyuuuuuuu
 
Waacheni wazee wa watu wapumzike, mbona nkurunzinza na jecha wa zanzibar wamepora ushindi wa maalim Seif hamsemi kitu, acheni hizo bana
 
mimi wanaosema sijui uchumi wetu ulikuwa mzuri enzi za mkapa wanatumia criteria gani UCHUMI HAUJAWAWI KUWA MZURI ZAIDI YA MIAKA YA 70s kipindi kile uzalishaji ulikuwa mkubwa TUNGEENDELEA KWA MWENDO ULE ULE TUNGEKUWA MBALI Mkapa katudidimiza tu kama mwenzie Mwinyi CCM HAMNA ALIYETUSAIDIA ZAIDI YA MATUMBO YAO
NYERERE PEKE YAKE ALIKUWA MZALENDO
ALIKOSA WAZALENDOWENZIE WAMETUPELEKA MPAKA HAPA

TANZANIA MANENO SANA ALIYENACHO NDO ANATHAMINIWA
 
Back
Top Bottom