Basil Mramba aelezea maisha ya jela na faida za kifungo cha nje

Ashura9

JF-Expert Member
Oct 21, 2012
739
484
MRAMBA AELEZEA MAISHA YA JELA NA FAIDA ZA KIFUNGO CHA NJE

Aliyekuwa Waziri wa Fedha katika Serikali ya awamu ya tatu, Basil Mramba, ameishauri Serikali kuhakikisha inawatumia wafungwa kutumikia jamii badala ya kuwarundika magerezani kwani maisha ya gerezani si salama na si njia pekee ya kumrekebisha mhalifu aliyehukumiwa na mahakama.

Kutokana na hali hiyo, alisema kuna haja kwa Serikali kuanza kutumia sheria namba 6 ya huduma kwa jamii kuwaangalia wafungwa wenye taaluma kutumika adhabu zao katika fani au taasisi za umma ili kupunguza gharama kuwahudumia watu ambao wanaweza kuisaidia jamii.

Mramba alitoa kauli hiyo jana, wakati yeye na mwenzake aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Daniel Yona, walipomaliza kufanya usafi katika Hospitali ya Sinza Palestina, Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya kutumikia adhabu ya kifungo chao cha nje baada ya wiki iliyopita Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuridhia kuwa wanastahili kutumikia jamii kwa kipindi cha miezi sita hadi Novemba 5.

“Jamii inaamini jela ni sehemu salama na mtu akishikwa na hatia kwa kosa lolote, mahala sahihi ni jela tu, kule anakutana na watu wa kila aina, wenye makosa tofauti, hali ambayo inamfanya ajifunze mambo mengine mapya.

“Unakuta mtu amefanya uhalifu wa kuiba kitu, anafungwa na kupelekwa gerezani, anakutana na majambazi sugu wanaompa mbinu zaidi, sasa akitoka jela anakuja akiwa ameiva, anarudia kwenye matukio akiwa amekamilika,” alisema Mramba.




Chanzo Dar 24
 
kweli hii ni point, watu wanalundikwa kule kwa gharama kubwa, hadi wanakosa nafasi hata za kusimama, wakati kuna kazi kibao za kufanya
kazi sio za kufanya usafi tuu, kuna mitaro ya maji hapa dar ya kuzibua, mvua Ikinyesha shida zipungue, majalala ya kuweka sawa, pia serikali ingeanzisha mashamba makubwa ya umwagiliaji yenye fence na ranch halafu hawa wafungwa wakaenda kutumikishwa huko, kulundika wahalifu sehemu moja halafu hawafanyi kazi bali ni kupiga soga kweli ni kuzidi kuwaongezea mbinu
 
Jk hakuwaga na mchezo kabisa.....
Waziri wa fedha mzima akala mvua,,,,,,,,,
 
Jk hakuwaga na mchezo kabisa.....
Waziri wa fedha mzima akala mvua,,,,,,,,,
Fitna tu!Hasara aliyoliletea Taifa yeye ni kubwa mara mia lakini anapeta tu!Unaweza kulinganisha Escrow tu na hasara iliyowapeleka jela kina Mramba?Kama wangekuwa wanahukumu kwa haki,hakuna jiwe lingesalia juu ya jiwe!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
MRAMBA AELEZEA MAISHA YA JELA NA FAIDA ZA KIFUNGO CHA NJE

..alisema kuna haja kwa Serikali kuanza kutumia sheria namba 6 ya huduma kwa jamii kuwaangalia wafungwa wenye taaluma kutumika adhabu zao katika fani au taasisi za umma ili kupunguza gharama kuwahudumia watu ambao wanaweza kuisaidia jamii.

Wataalamu Wahalifu kama walishindwa kutumia taaluma zao vema ktk mazingira stahili tusitegeemee watazitumia vizuri kataika kifungu cha nje. Kifungo ni adhabu na itagharamiwa na serikali hata km ni kupasua mawe maisha yao yote ili mradi kupeleka funzo kwa jamii.
 
Wataalamu Wahalifu kama walishindwa kutumia taaluma zao vema ktk mazingira stahili tusitegeemee watazitumia vizuri kataika kifungu cha nje. Kifungo ni adhabu na itagharamiwa na serikali hata km ni kupasua mawe maisha yao yote ili mradi kupeleka funzo kwa jamii.
Siamini kama walioko jela wote ni wahalifu
 
“Jamii inaamini jela ni sehemu salama na mtu akishikwa na hatia kwa kosa lolote, mahala sahihi ni jela tu, kule anakutana na watu wa kila aina, wenye makosa tofauti, hali ambayo inamfanya ajifunze mambo mengine mapya.

Kwa mawazo yangu magereza yetu yako kwenye makundi ya uhalifu kumbe ni mrundikano bila kujali Kosa lipi limekufikisha huko!
Kuna haja hili likapewa kipaumbe na kufanyiwa uchanganuzi!. Muaji kukaa na aliyefungwa kwa matusi siyo sahihi na kweli tutakuwa hatujengi jamii .
 
Mwingereza aliamua kwenda kuwatupa wahalifu sugu kule Australia. Sasa wamekuwa werevu kuliko wao. Sisi tunawarundika wote bila kuchagua Maximum prison. Hatujali kosa lake wala athari zake. Walioonewa na wenye makosa ya kweli, inategemea na alivyo amka hakimu/Jaji.
Nadhani, Mramba alijifunza kitu kule, tuufuate ushauri wake. Pole zake hata hivyo, amefanywa tu kondoo wa Pasaka kupisha upepo upite.
 
Back
Top Bottom